Rais Samia athibitisha mmoja kugundulika na maambukizi ya virusi vya Marburg nchini

Rais Samia athibitisha mmoja kugundulika na maambukizi ya virusi vya Marburg nchini

Torra Siabba

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2016
Posts
243
Reaction score
287
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema mtu mmoja amekutwa na maambukizi ya virusi vya Marburg (MVD) katika Wilaya ya Biharamuro mkoani Kagera.

Taarifa hiyo inakuja siku sita tangu Shirika la Afya Duniani (WHO) liweke wazi kuhusu watu wanane kufariki dunia kutokana na ugonjwa unaoshukiwa kuwa wa virusi vya Marburg mkoani humo.

Rais Samia ameyasema hayo leo Jumatatu, Januari 20, 2025 alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dk Tedros Adhanom Ghebreyesus.

Rais Samia amesema Serikali ilituma timu ya wataalamu Januari 11 mwaka huu mkoani humo na kufanya uchunguzi kuhusu ugonjwa huo na katika sampuli zilizochukuliwa ni mgonjwa mmoja pekee aliyekutwa na maambukizi hayo.

“Mpaka kufikia Januari 20, 2025 sampuli 25 zilizopimwa maabara ni mgonjwa mmoja pekee amekutwa na maambukizi na hivyo kuifanya nchi kupata mlipuko huo kwa mara ya pili. Lakini mpaka sasa nchi ipo salama na hakuna mambukizi mengine yaliyobainika,” amesema Rais Samia.

Taarifa iliyochapishwa mtandaoni na WHO Januari 13, 2025 imewajulisha nchi wanachama wake na vyombo vya kusimamia Kanuni za Afya za Kimataifa (IHR) kuhusu mlipuko wa ugonjwa unaoshukiwa kuwa Marburg katika wilaya mbili za mkoa huo uliopo Kaskazini mwa Tanzania.

Pia soma:
~
WHO: Watu nane wamefariki Kagera kwa ungojwa unahisiwa kuwa ni Marburg
~ Serikali yasema inafuatilia taarifa za uwepo wa Virusi vya Marburg Mkoani Kagera
 
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema mtu mmoja amekutwa na maambukizi ya virusi vya Marburg (MVD) katika Wilaya ya Biharamuro mkoani Kagera.

Taarifa hiyo inakuja siku sita tangu Shirika la Afya Duniani (WHO) liweke wazi kuhusu watu wanane kufariki dunia kutokana na ugonjwa unaoshukiwa kuwa wa virusi vya Marburg mkoani humo.

Rais Samia ameyasema hayo leo Jumatatu, Januari 20, 2025 alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dk Tedros Adhanom Ghebreyesus.

Rais Samia amesema Serikali ilituma timu ya wataalamu Januari 11 mwaka huu mkoani humo na kufanya uchunguzi kuhusu ugonjwa huo na katika sampuli zilizochukuliwa ni mgonjwa mmoja pekee aliyekutwa na maambukizi hayo.

“Mpaka kufikia Januari 20, 2025 sampuli 25 zilizopimwa maabara ni mgonjwa mmoja pekee amekutwa na maambukizi na hivyo kuifanya nchi kupata mlipuko huo kwa mara ya pili. Lakini mpaka sasa nchi ipo salama na hakuna mambukizi mengine yaliyobainika,” amesema Rais Samia.

Taarifa iliyochapishwa mtandaoni na WHO Januari 13, 2025 imewajulisha nchi wanachama wake na vyombo vya kusimamia Kanuni za Afya za Kimataifa (IHR) kuhusu mlipuko wa ugonjwa unaoshukiwa kuwa Marburg katika wilaya mbili za mkoa huo uliopo Kaskazini mwa Tanzania.
Marburg... Mabugi.... Mabagi!
Hivi kila mtu ameelewa ulichokiongelea katika hilo andishi lako refu?

Umeshindwaje kuelezea hao vimelea wanasababisha mripuko wa ugonjwa gani, ili hata lay man auelewe ugonjwa unaoongelewa?
 
Ametaja measures zipi ambazo watanzania wanatakiwa kuzingatia ili ugonjwa huo usisambae zaidi ?
 
Marburg... Mabugi.... Mabagi!
Hivi kila mtu ameelewa ulichokiongelea katika hilo andishi lako refu?

Umeshindwaje kuelezea hao vimelea wanasababisha mripuko wa ugonjwa gani, ili hata lay man auelewe ugonjwa unaoongelewa?
Naunga mkono hoja. Anatuletea alichokiongea mama yake badala ya kuelezea huo ugonjwa ukoje na dalili zake
 
Na kule pande za Yombo Dovya jijini Dar es Salaam, wale wakaazi kunapopita malori ya mizigo kwenda Rwanda, DR Congo, Burundi kutoka bandari kavu ni nini kiliwakumba...? Bado vipimo havijatoka baada ya kuchukua sampuli mbalimbali?



View: https://m.youtube.com/watch?v=p_T6HzRmyp8
 
Yombo Dovya bandari kavu Dar es Salaam Tanzania kwa malori ya nchi za Burundi, Rwanda na DR Congo, je hakuna uwezekano safari hizi ndefu za madereva na ma utingo wanaofika nchi za maziwa makuu kuleta ugonjwa ?
1737382811777.jpeg

Last week African countries reported 2,532 new mpox cases, mostly in the Democratic Republic of the Congo (DRC) and Burundi, pushing the total since the first of the year to 50,840 cases, officials from Africa Centres for Disease Control and Prevention (Africa CDC) said today...

The officials also reported 32 more deaths from the virus. At the briefing, Jean Kaseya, MD, MPH, Africa CDC's director-general, said cases continue to rise in Uganda and the outbreak has spread to one more district of Central African Republic (CAR), Paoua, which is on the border with Chad.....source : Cases top 50,000 in Africa's mpox outbreak


Mpox Situation in Rwanda
  • Cumulative suspected cases: 5486.
  • New suspected cases: 122.
  • Total confirmed cases: 78.
  • New confirmed cases: 4.
  • Cases under follow-up: 20.
  • Total discharged cases: 58.
  • New discharged cases: 11.

RBC: Home › mpox
 

WHO inasema mlipuko unaoshukiwa kuwa wa ugonjwa wa Marburg umeua watu 8 katika maeneo ya mbali ya Tanzania​

Januari 15, 2025 9:00 AM
FILE - Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Ulimwenguni Tedros Adhanom Ghebreyesus akihutubia mkutano na waandishi wa habari kuhusu mlipuko wa virusi vya Marburg katika Kituo cha Mikutano cha Kigali huko Kigali, Rwanda, Oktoba 20, 2024.

Picha maktaba FILE - Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO), Dr. Tedros Adhanom Ghebreyesus akihutubia mkutano na waandishi wa habari kuhusu mlipuko wa virusi vya Marburg katika Kituo cha Mikutano cha Kigali huko Kigali, Rwanda, Oktoba 20, 2024.

ARUSHA, Tanzania —
Shirika la Afya Ulimwenguni lilisema Jumatano mlipuko wa ugonjwa unaoshukiwa kuwa wa Marburg umeua watu wanane katika sehemu ya mbali ya kaskazini mwa Tanzania.


"Tunafahamu kuhusu kesi 9 kufikia sasa, ikiwa ni pamoja na watu 8 ambao wamefariki," mkuu wa WHO Tedros Adhanom Ghebreyesus alisema katika taarifa yake.

"Tungetarajia kesi zaidi katika siku zijazo kadiri uchunguzi wa magonjwa unavyoboreka."


Kama vile Ebola, virusi vya Marburg huanzia kwa popo wa matunda na huenea kati ya watu kwa kugusana kwa karibu na maji maji ya mwili ya watu walioambukizwa au kwa nyuso, kama vile shuka zilizochafuliwa na mgonjwa.

Bila matibabu, Marburg inaweza kuwa mbaya katika hadi 88% ya watu ambao wanaugua ugonjwa huo. Dalili ni pamoja na homa, maumivu ya misuli, kuhara, kutapika na wakati fulani kifo kutokana na kupoteza damu nyingi. Hakuna chanjo iliyoidhinishwa au matibabu ya Marburg.


WHO imesema tathmini yake ya hatari kwa mlipuko unaoshukiwa kuwa nchini Tanzania iko juu katika ngazi za kitaifa na kikanda lakini chini duniani. Hakukuwa na maoni ya mara moja kutoka kwa mamlaka za afya ya Tanzania.


Mlipuko wa Marburg nchini Rwanda, ulioripotiwa kwa mara ya kwanza Septemba 27, 2024 ulitangazwa kuwa umekwisha Desemba 20, 2024.

Maafisa wa Rwanda waliripoti jumla ya vifo 15 na visa 66, huku wengi wa wale walioathiriwa wahudumu wa afya ambao walihudumia wagonjwa wa kwanza.

Mlipuko wa mwaka 2023 wa Marburg huko Kagera, mkoa ambao una mpaka na nchi ya Rwanda, uliua takriban watu watano.
 
Hela za donors zinakuja kuendeleza kampeni za uchafuzi.
 
  • Thanks
Reactions: apk
20 January 2025

Tanzania Confirms First Case of Marburg Virus in 2025 in Northeastern Region


View: https://m.youtube.com/watch?v=jUfkaS3acOs

Tanzania has confirmed its first case of the Marburg virus in 2025, which occurred in Biharamulo district in Kagera region, located in the northeastern part of the country. This marks the second outbreak of the deadly disease in Tanzania.Speaking at a press briefing after a meeting with World Health Organization (WHO) Director-General, Dr. Tedros Adhanom Ghebreyesus, Tanzanian President Samia Suluhu Hassan stated that the government took numerous measures following rumors of the outbreak. These included investigating suspected individuals, working with local authorities, and establishing emergency response teams...

Source : The Chanzo
 
Wasipo chukua tahadhari ya dharula na kuidhibiti kama mwaka juzi basi tutegemee litakuwa janga litakalomtesa huyu mama kwa kumbukumbu Kagera ni sehemu ambapo kila rais wa nchi hii alipata janga au changamoto katika utawala wake

Nyerere ilikuwa ni vita na Idd Amin
Mwinyi ilikuwa ni ukimwi
Mkapa ajali ya Mv bukoba
Kikwete ni mnyauko wa migomba
Magufuli tetemeko


Samia....? Marburg huwa ipo miaka yoote kwa jirani zetu Uganda na Congo pamoja na ukaribu wao kijiografia eneo hilo lakini haikuwahi kusambaa mkoani humo, ni kwenye awamu ya huyu mama .....ni muhimu walitilie maanani la sivyo story ya 2014 huko Liberia na Guinea kuhusu ebola itajirudia
 
  • Thanks
Reactions: apk
Kwann wanatuficha hawasemi ukweli wanasubir Hali iwe mbaya
 
Back
Top Bottom