SoC01 Rais Samia atumie njia zifuatazo ili kutupatia Katiba Mpya

SoC01 Rais Samia atumie njia zifuatazo ili kutupatia Katiba Mpya

Stories of Change - 2021 Competition

Nawatania

Senior Member
Joined
Jul 13, 2021
Posts
148
Reaction score
549
Kwanza naomba niseme mimi sio mwanachama wa chama chochote lakini kama mtu huru ninao uwezo wa kuishauri serikali na Rais wetu njia bora ya kupata Katiba mpya

Kuna watu watauliza je kwanini nimeandika moja kwa moja kwa Rais?

Jibu ni moja tu kwa katiba tuliyonayo Rais ndiye kila kitu kitakachofanyika katika nchi hii ndio maana mambo yakiharibika Watanzania moja kwa moja uwa wanamshutumu Rais aliyepo madarakani.

Nikweli Watanzania wengi wanataka katiba mpya ila vile vile wapo wengine wengi wasiotaka Katiba mpya.

Kundi la kwanza wasiotaka katiba mpya wale wananchi wasio na elimu ya Uraia hawa ni kundi kubwa sana na hawana maslahi yeyote ila hawataki tu! Na ukiwauliza watakwambia hawana faida na katiba.

Kundi la pili ni baadhi ya viongozi wastaafu wa serikali na Ccm wao wanaogopa kuibuliwa kwa mambo yao mabaya yaliyopita.

Kundi la tatu ni waliopo madarakani, Ndugu zao na Rafiki zao wengi wanahisi kuna mambo wameshavuruga hivyo wanataka katiba isipatikane mapema ili wasije wakawajibika.

Haya makundi ndio kikwazo cha katiba mpya

Naomba niende kwenye hoja, Naomba ikuwapendeza wasaidizi wa Rais wafikishe mawazo yangu kwa Rais Samia.

Rais atumie njia zifuatazo ili kufanikisha katiba mpya

Moja; Kuweka kifungu kwenye katiba mpya kwamba pale tu itakapoanza kutumika, Kwa mfano tuchukulie baada ya uchaguzi 2025 watu wote waliofanya makosa yaliyokatazwa kwenye Katiba nyuma wasamehewe na kuachwa ili wawe na amani na wawe sehemu ya mchakato wa kufanikisha kupatikana kwa katiba mpya sasa.

Pili; Wale wote wasio na elimu ya katiba waelimishwe kwa kutumia mitandao ya kijamii, kufuatwa mashambani na kwenye matangazo ya Radio na Television.

Tatu; Vyama vya siasa vielimishwe umuhimu na wagomea wenye uwezo wa kushindana kwenye chaguzi hivyo mtu atateuliwa kwa sababu sio mana Ccm au Chadema atateuliwa kwa sababu ana hoja ya kuleta mabadiliko baada ya yeye kuchaguliwa.

Ziwepo opinion poll kabla ya mgomea ajateuliwa na chama chake kukiwakilisha hii itapunguza hofu ya kushindwa hasa kwa chama Tawala na kupalilia Democrasia kufanya kazi yake vizuri.

Tukifanya hivi tutapata katiba mpya kabla ya 2025 na kila mtu atakuwa na amani.
View attachment 1853300
 
Upvote 5
Leo ndo nimeona mchango mzuri ulio gonga point zote kwa mtazamo wangu. Twna hapo kwenye ishu ya uwelimishaji ndo umegusa hasa.

Na amini watu wengi wakielimishwa kusu nini mana ya katiba na ni sheria zipi zinazo patikana ndani ya katiba basi wengi watafunguka na mungano wa kudai utakuwa mkubwa.

Kupitia gazeti, televisheni, redio na mitandao ya kijami hii kweli itarahisha elimu kufika kwa kasi.

Pia naona kundi la vijana ni zuri sana kama lingeshirikishwa kwenye atuwa zoote za michakato kwamana vijana ndo kizazi kitakacho ongoza maendeleo katika taifa
 
Leo ndo nimeona mchango mzuri ulio gonga point zote kwa mtazamo wangu. Twna hapo kwenye ishu ya uwelimishaji ndo umegusa hasa.

Na amini watu wengi wakielimishwa kusu nini mana ya katiba na ni sheria zipi zinazo patikana ndani ya katiba basi wengi watafunguka na mungano wa kudai utakuwa mkubwa.

Kupitia gazeti, televisheni, redio na mitandao ya kijami hii kweli itarahisha elimu kufika kwa kasi.

Pia naona kundi la vijana ni zuri sana kama lingeshirikishwa kwenye atuwa zoote za michakato kwamana vijana ndo kizazi kitakacho ongoza maendeleo katika taifa
Ndio hatutakiwi kutumia nguvu kukwamisha katiba au kutumia nguvu kutaka kupata katiba tunatakiwa kutumia ushawishi juu ya upatikanaji wake
 
Ndio hatutakiwi kutumia nguvu kukwamisha katiba au kutumia nguvu kutaka kupata katiba tunatakiwa kutumia ushawishi juu ya upatikanaji wake
Hakika marifa ni bora kuliko nguvu.
Naamini utawala kandamizi huwa haudumu uleta mabadiliko kwa mda mfupi ila mabadiliko hayadumu.

Ningeomba tasisi binafsi na wana arakati kwa sasa wangeungana kwa namna yoyote ile na kuanza kutoa elimu juu ya umuhimu wa katiba mpya. Mfano napenda kupendekeza apa JF lingewekwa jukwa la uchambuzi wa vipengele vya katiba.

Naamini sio wote wanapenda kuka na ile katiba na kuanza kusoma mpaka kumaliza ila kungeanzishwa jukwa la kuchambuwa basi lingekusa wengi wanao penda kusoma na wasio penda kusoma.

Ili kuweza kuwasaidia wasio penda kusoma pia kungetumika Audio records.
 
Hakika marifa ni bora kuliko nguvu.
Naamini utawala kandamizi huwa haudumu uleta mabadiliko kwa mda mfupi ila mabadiliko hayadumu.

Ningeomba tasisi binafsi na wana arakati kwa sasa wangeungana kwa namna yoyote ile na kuanza kutoa elimu juu ya umuhimu wa katiba mpya. Mfano napenda kupendekeza apa JF lingewekwa jukwa la uchambuzi wa vipengele vya katiba.

Naamini sio wote wanapenda kuka na ile katiba na kuanza kusoma mpaka kumaliza ila kungeanzishwa jukwa la kuchambuwa basi lingekusa wengi wanao penda kusoma na wasio penda kusoma.

Ili kuweza kuwasaidia wasio penda kusoma pia kungetumika Audio records.
Nafikiri jamii forum wanatusikia naomba walifanyie kazi hili
 
Back
Top Bottom