Rais Samia, hatua zaidi zinahitajika kukabiliana na COVID-19

Rais Samia, hatua zaidi zinahitajika kukabiliana na COVID-19

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Mama Samia rais wetu, umetufahamisha rasmi uwepo wa ugonjwa huu mbaya hapa nchini. Umetaka maelekezo yote yanayotolewa na wataalamu kufuatwa. Kwa mioyo mikunjufu yote tumeyakubali na tutayazingatia.

Tunaamini maelekezo yako ndiyo ulio msimamo rasmi wa Serikali na kuwa hayatakuwa maneno matupu yasiyoweza kuvunja mfupa.

Si nia yangu kuyarejelea yote wanayotutaka wataalamu kuyazingatia. Bali yale ambayo yanahitaji msukumo wako wewe kama kiongozi wetu.

Ndani ya wiki moja Hospitali ya Bugando imepoteza madaktari bingwa 2. Kwa hakika mpambano na ugonjwa huu si mwepesi hata kidogo. Msukumo wako zaidi unahitaji utakaosaidia kuyaweka mambo kuwa sawa zaidi ikiwamo kuokoa muda.


Tumefika je hapa tulipo? Hakuna mwenye akili zake asiyejua. Hofu ya watawala ilikuwa imetamalaki. Huu utakuwa ni muda wa kusukuma vilivyo hali ile kubadilika. Kwenye maeneo yao watu wahimizwe kutekeleza wajibu wao kikamilifu bila ya kukusubiria wewe kuingilia kati.

Katika maelekezo ya wataalamu kuhusiana na ugonjwa huu, inafahamika kuwa:

1. Takwimu za ugonjwa zinapaswa kutolewa na kwa wakati.
2. Misongamano isiyo ya lazima kusitishwa.
3. Social distancing na barakoa kutumika kote inapobidi.

Itifaki rasmi za kuyafanikisha haya zinapaswa kuwapo na kujulikana wazi wazi na kila mtu. Ambapo:

#1. Itaweka dira na msisitizo zaidi wa namna ya kujihami na kuwahami wengine, kwa maeneo kulingana na kiwango cha uathirika.

#2. Mikusanyiko yote isiyo ya lazima zikiwamo sherehe, misiba, ibada nk kufuata itifaki rasmi zinazofahamika.

#3. Hili na yote hapo juu hayawezi kuwa hiari tena. Hii ikiwa ni kwa mustakabala mwema tu wa maisha yetu sote.

Mama umethubutu na kwa kwa pamoja tutavuka.

Nisiache kukusalimu kwa jina la JMT.

Ninawasilisha.
 
Takwimu zinasaidia nini?

Takwimu haziwezi kusaidia kupambana n korona.

Muhimu ni kuhimiza watu kuendelea kuchukua tahadhari.

Seychelles ndio nchi imechanja 99% watu sake lakini maambukizi ya Covid yako juu balaa, sasa maambukizi yanatoka wapi kama 99% ya watu wamechanjwa?
 
Takwimu zinasaidia nini?

Takwimu haziwezi kusaidia kupambana n korona.

Muhimu ni kuhimiza watu kuendelea kuchukua tahadhari.

Seychelles ndio nchi imechanja 99% watu sake lakini maambukizi ya Covid yako juu balaa, sasa maambukizi yanatoka wapi kama 99% ya watu wamechanjwa?

Ingependeza zaidi kujikita kwenye mada. Uzi huu ni kwa ajili ya hatua zaidi kama ilivyo ainishwa.

Uwepo wa takwimu ni muhimu kwani zitaonyesha viwango vya uathirika kwa maeneo, ili hatua mahsusi (specific) ziweze kuchukuliwa:

IMG_20210626_063944_426.jpg


Kwa mfano, kama Changanyikeni au Msewe (Dar) kumeathirika zaidi, kwanini kuendelea kukusanya watu huko kwa ajili ya mbio za mwenge?

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Umeambiwa maiti inaambukiza hadi mnataka kunyima wananchi uhuru wao kuzikwa wapendwa wao ? Mnapenda mambo ya kichoko sana.

Mama katuelekeza kufuata maelekezo ya wataalamu.

Kwenye red ni yale maelekezo ya tume ya wataalamu (tu), ambayo Mama anahitajika kuyapa msukumo:

IMG_20210626_065035_652.jpg


Kwenye blue ni mahitajio ya itifaki rasmi ya namna ya kushughulika na mikusanyiko ikiwamo misiba.

Wapi unayasoma ya mtu kuzuiliwa kuzika mpendwa wake kwa uhuru?

Nisiache kusema hili, "Ninaamini hata wewe hujaambiwa kama maiti haiambukizi."
 
Mwanzo Mataga walikuwa wanasema Corona ni Hoax, halafu wakaja na kuwa Corona imeletwa na Mabeberu ili kuhujumu Sgr ya Magufuli katika Vita vya Kiuchumi, halafu wakaja na Barakoa za kutoka China na Ulaya zimejaa Sumu na Covid 19 ili kutumaliza Watanzania,sasa hivi wamekuja na Mpya kuwa kuna Mabilioni ya fedha za Covid19 ndio maana Raisi wa Awamu ya sita anakubali kutangaza takwimu na kufuata guidelines za WHO

Kali zaidi ni Raisi aliyepita kufikiria Mkuu wake wa Mkoa wa Dar ati anasambaza Covid19 kwa kupulizia kwenye Mitaa ya Dar😆🤣

Hawa Mataga ni Mazezeta sana trust me.
 
Mwanzo Mataga walikuwa wanasema Corona ni Hoax, halafu wakaja na kuwa Corona imeletwa na Mabeberu ili kuhujumu Sgr ya Magufuli katika Vita vya Kiuchumi, halafu wakaja na Barakoa za kutoka China na Ulaya zimejaa Sumu na Covid 19 ili kutumaliza Watanzania,sasa hivi wamekuja na Mpya kuwa kuna Mabilioni ya fedha za Covid19 ndio maana Raisi wa Awamu ya sita anakubali kutangaza takwimu na kufuata guidelines za WHO

Hawa Mataga ni Mazezeta sana.

Wana tatizo kubwa la kutokuwa na elimu. Yaani wamegubikwa zaidi na ujinga. Kwa sababu hiyo hawajui wanataka nini au hawataki nini na kwa nini.

Wamekuwa wanajaribu kujifunza majina mapya kila uchao. "Na sasa wanaitwa vipusa." Alisisitiza mwanamziki huyo.

Kwa mujibu wa mwenzao huyu:


Kimsingi wako kama wanafanya maigizo tu.
 
Corona haipo, njoo kkoo

Kuna nduguyo hapa Bemendazole hakukufikishia ujumbe bado?

IMG_20210626_091339_865.jpg


Sisi alitukumbusha nasi tukamhimiza asikusahau na wewe utapwelewa.

Wenzako kambi wanahama kimya kimya.

😂😂😂😂😂😂😂!

Habari ndiyo hiyo.
 
Tunasonga mbele. Heko mama Samia:


Ila bwana yule ....! Basi tu hatutamsahau.
 
Tunasonga mbele. Heko mama Samia:


Ila bwana yule ....! Basi tu hatutamsahau.
Uliangalia Jana mama akipiga simu kwa nandy? Ulipata ujumbe gani?
 
Mama Samia rais wetu, umetufahamisha rasmi uwepo wa ugonjwa huu mbaya hapa nchini. Umetaka maelekezo yote yanayotolewa na wataalamu kufuatwa. Kwa mioyo mikunjufu yote tumeyakubali na tutayazingatia.

Tunaamini maelekezo yako ndiyo ulio msimamo rasmi wa serikali na kuwa hayatakuwa maneno matupu yasiyoweza kuvunja mfupa.

Si nia yangu kuyarejelea yote wanayotutaka wataalamu kuyazingatia. Bali yale ambayo yanahitaji msukumo wako wewe kama kiongozi wetu.

Ndani ya wiki moja Hospitali ya Bugando imepoteza madaktari bingwa 2. Kwa hakika mpambano na ugonjwa huu si mwepesi hata kidogo. Msukumo wako zaidi unahitaji utakaosaidia kuyaweka mambo kuwa sawa zaidi ikiwamo kuokoa muda.


Tumefika je hapa tulipo? Hakuna mwenye akili zake asiyejua. Hofu ya watawala ilikuwa imetamalaki. Huu utakuwa ni muda wa kusukuma vilivyo hali ile kubadilika. Kwenye maeneo yao watu wahimizwe kutekeleza wajibu wao kikamilifu bila ya kukusubiria wewe kuingilia kati.

Katika maelekezo ya wataalamu kuhusiana na ugonjwa huu, inafahamika kuwa:

1. Takwimu za ugonjwa zinapaswa kutolewa na kwa wakati.
2. Misongamano isiyo ya lazima kusitishwa.
3. Social distancing na barakoa kutumika kote inapobidi.

Itifaki rasmi za kuyafanikisha haya zinapaswa kuwapo na kujulikana wazi wazi na kila mtu. Ambapo:

#1. Itaweka dira na msisitizo zaidi wa namna ya kujihami na kuwahami wengine, kwa maeneo kulingana na kiwango cha uathirika.

#2. Mikusanyiko yote isiyo ya lazima zikiwamo sherehe, misiba, ibada nk kufuata itifaki rasmi zinazofahamika.

#3. Hili na yote hapo juu hayawezi kuwa hiari tena. Hii ikiwa ni kwa mustakabala mwema tu wa maisha yetu sote.

Mama umethubutu na kwa kwa pamoja tutavuka.

Nisiache kukusalimu kwa jina la JMT.

Ninawasilisha.
Rais wako mwenyewe kapiga simu live kwa Nandy ndani ya tamasha lililoshona nyomi. Maana yake kalipatia baraka. Afu wewe unatusumbua hapa na nyuzi za tahadhari ya korona...jilinde wewe na mke inatosha
 
Rais wako mwenyewe kapiga simu live kwa Nandy ndani ya tamasha lililoshona nyomi. Maana yake kalipatia baraka. Afu wewe unatusumbua hapa na nyuzi za tahadhari ya korona...jilinde wewe na mke inatosha
Umempiga bonge la jiwe kichwani, lazima avuje damu.
Mama Samia anajuakuwa corona haipo ila ni jinsi ya kuwaridhisha wajinga huko. Na ndio maana jana alipiga simu kwenye festival, na hakuna aliyevaa barakoa wala barakohoa
 
Ni lijinga, mama Samia anajua kabisa kuwa corona haipo ila anawaridhisha tu wajinga flani.
Ndio maana unaona jana Wala hajastuka na ule mkusanyiko bila hayo mabarakoa

Jinga liko hapo:

IMG_20210625_093922_275.jpg
 
Umempiga bonge la jiwe kichwani, lazima avuje damu.
Mama Samia anajuakuwa corona haipo ila ni jinsi ya kuwaridhisha wajinga huko. Na ndio maana jana alipiga simu kwenye festival, na hakuna aliyevaa barakoa wala barakohoa

Ujinga ni shida. Umemwona Mama Samia bila barakoa tena?

IMG_20210625_121904_739.jpg


IMG_20210627_213938_504.jpg


Wewe ndiye mjuzi zaidi kuliko yeye?

Tulikuwa na shujaa asiyevaa barakoa kuliko aliyepumzika chattle?

Hao nao je, uliwahi kuwasikia?

IMG_20210418_164416_802.jpg


IMG_20210507_212540_605.jpg


Kumbe unadhani ni urembo?

Karagabaho!
 
Back
Top Bottom