Rais Samia kuhudhuria Mkutano wa 44 wa SADC na kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama

Rais Samia kuhudhuria Mkutano wa 44 wa SADC na kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama

Influenza

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2018
Posts
1,509
Reaction score
3,756

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI​

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hasan anatarajia kuhudhuria Mkutano wa 44 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) utafakaonyika tarehe 17 Agosti 2024 mjini Harare, Zimbabwe.

Rais Dkt. Samia anatarajia kuondoka chini leo tarehe 15 Agosti, 2024 kuhudhuria Mkutano huo wenye kauli mbinu: "Kukuza ubunifu ili kufungua fursa za ukuaji wa uchumi na maendeleo endelevu kuelekea SADC yenye viwanda".

Katika Mkutano huo, Rais Dkt. Samia anatarajia kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC akipokea kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Zambia Hakainde Hichilema anayemaliza muda wake.

IMG_0908.jpeg
 
Katika Mkutano huo, Rais Dkt. Samia anatarajia kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC akipokea kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Zambia Hakainde Hichilema anayemaliza muda wake.
Isemwe tu anakwenda kupewa uenyekiti siyo kuchaguliwa kwani anagombea kiti na nani?
 
Back
Top Bottom