Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wakuu,
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepongeza utendaji wa Mbunge wa Jimbo la Muheza ambaye pia ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamisi Mwinjuma (Mwana FA), na Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Nickson John Simon (Nikk wa Pili), akieleza kuwa wamekuwa msaada mkubwa serikalini.
Akihutubia wananchi wa wilaya ya Muheza, Rais Samia alisema kuwa uteuzi wa wasanii hao wawili ulizua maswali kwa baadhi ya watu, lakini sasa wameonesha uwezo wao mkubwa wa kiuongozi na kujituma katika majukumu yao.
"Nilipomteua Mwana FA (Hamisi Mwinjuma, Mbunge wa Jimbo la Muheza) na yule Mkuu wangu wa Wilaya ya Kibaha anaitwa Nikk wa Pili (Nickson John Simon) watu hawakuelewa lakini kwa faraja kubwa, hawa wananisaidia sana," amesema Rais Samia.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepongeza utendaji wa Mbunge wa Jimbo la Muheza ambaye pia ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamisi Mwinjuma (Mwana FA), na Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Nickson John Simon (Nikk wa Pili), akieleza kuwa wamekuwa msaada mkubwa serikalini.
Akihutubia wananchi wa wilaya ya Muheza, Rais Samia alisema kuwa uteuzi wa wasanii hao wawili ulizua maswali kwa baadhi ya watu, lakini sasa wameonesha uwezo wao mkubwa wa kiuongozi na kujituma katika majukumu yao.
"Nilipomteua Mwana FA (Hamisi Mwinjuma, Mbunge wa Jimbo la Muheza) na yule Mkuu wangu wa Wilaya ya Kibaha anaitwa Nikk wa Pili (Nickson John Simon) watu hawakuelewa lakini kwa faraja kubwa, hawa wananisaidia sana," amesema Rais Samia.