Rais Samia Suluhu amteua Jaji Jacob Mwambegele kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)

Haya Zitto , Tume yako hiyo, huru
 
Basi tunataka Tanzania ndo iwe nchi ya kwanza kuwa kuwa mwenye kiti wa tume ya uchaguzi hachaguliwi na mwenyekiti wa CCM.
Sasa hapo Kuna uchaguzi au UCHAFUZI?.
Ni RAIS gani mpumbavu atakubali akuchague yeye alafu uwape HAKI wapinzani?
Wewe unataka wapinzani waongoze vipi wakati jina lenyewe wanaitwa WAPINZANI! Kwani hawa waliopo wakiongoza si watu pia? Au unadhani wapibzani wakipewa dhamana ya kuongoza utapata mwanya wa kukwapua hela mahali! Thubutu yako, bora uje huku kulima pilipili hoho weye!
 
Bila katiba mpya na tume huru ya uchaguzi ni maigizo yale yle tu...
 
ACHA UONGO, Marekani hakuna tume ya uchaguzi inayosimamiwa na Rais, wanaosimamia kura wote ni makatibu wa majimbo waliochaguliwa kwa kupigiwa kura na wananchi.
 
Hongera kwake.
watanzania tunahitaji maendeleo sio kingine.
wanasiasa wanataka madaraka na vyeo kwa kujifanya eti wanataka katiba mpya, kwa sasa tuachane na hizo ngonjera.
 
Sasa kuna haja gani ya kuwa na vyama vingi
 
Venezuela Rais hateui hata mtu mmoja kwenye tume nzima ya uchaguzi. Tume ya uchaguzi ya Venezuela ni tawi linalojitegema la serikali, wajumbe wake wanachaguliwa kutoka taasisi mbalimbali za kiraia na bunge na wajumbe ndio wanamchagua mwenyekiti wa tume.
 
Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi Mexico anateuliwa na BUNGE kwa kipindi cha kisheria cha miaka 9.
 
DR Congo mwenyekiti wa tume ya uchaguzi anateuliwa na muungano wa asasi za kiraia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…