kipara kipya
JF-Expert Member
- May 2, 2016
- 18,833
- 23,276
Mambo yanaendelea huko tufuatilie kasi ni ile ile kazi iendelee.
========
Rais Samia Suluhu ameongoza shughuli za kuzindua Mitambo na kwa sasa zoezi linaloendelea salamu za watu mbali mbali. Alianza Professa Janabi ambae ametambulisha watu wote anaofanya nao kazi kila siku. Dkt. Janabi ametambulisha madaktari Bingwa wa Moyo nchini na kuelezea 'succession plan' kwenye taasisi yao endapo yeye ataondoka ama baadhi ya watu katika taasisi hiyo.
Baada ya Dkt. Janabi alifata Mkuu wa Mkoa wa Dar, Amos Makalla ambae ameongea kwa mara ya kwanza leo mbele ya Rais tangu kuteuliwa. Amos Makalla amemshukuru Rais Samia kumteua kuwa mkuu wa Mkoa wa Dar na kusema kwake ni nyumbani sehemu aliyozaliwa na kukulia. Makalla ameahidi kuendelea kukomesha Ujambazi Dar es Salaam.
Kisha akafata mkuu wa bodi ya Taasisi ya Jakaya Kikwete na kuelezea ndoto zake za kutibu magonjwa ya Moyo nchini na wengine kumkejeli mpaka ndoto zake kuwa kweli. Mwenyekiti ameelezea ndoto yake ya kuweza kuwa na watu mikoani watakaokuwa na uwezo wa kutibu magonjwa ya Moyo.
Anaongea Rais Samia na anasema kazi anayozindua leo ilifanyika awamu ya Tano na kumpongeza Hayati Rais Magufuli. Rais Samia amesema ameona uchawi unaofanyika ndani ya taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete. Amesema Tanzania inajisifu kwa kupunguza vifo vya watoto.
Rais Samia amesema eneo la Jakaya Kikwete limesaidia kupunguza vifo vya watoto. Amesema wagonjwa 5959 wamepata matibabu na watu 11 pekee wamefariki baada ya Upasuaji ikiwa ni asilimia 0.2 pekee. Ameongeza kusema mitambo pekee haitoshi kwani inaongozwa na watu na kuitumia ipasavyo.
Anasema ukisikia kusimamishwa moyo unakufa kabla haujasimamishwa lakini ndani ya taasisi ya Jakaya Kikwete unasimamishwa mpaka masaa sita.
Ameeleza kuzibeba changamoto zao na wanaenda kuzifanyia kazi.
Rais Samia amesema mcheza kwao hutuzwa na serikali itaangalia Maslahi yao.
Rais Samia Suluhu amewaahidi Bilioni mbili kutoka Serikalini kama walivyoomba kwa ajili ya kujenga jengo jipya, wao Taasisi ya moyo watatoa bilioni 2 kukamilisha bilioni 4 kwa ajili ya ujenzi huo
========
Rais Samia Suluhu ameongoza shughuli za kuzindua Mitambo na kwa sasa zoezi linaloendelea salamu za watu mbali mbali. Alianza Professa Janabi ambae ametambulisha watu wote anaofanya nao kazi kila siku. Dkt. Janabi ametambulisha madaktari Bingwa wa Moyo nchini na kuelezea 'succession plan' kwenye taasisi yao endapo yeye ataondoka ama baadhi ya watu katika taasisi hiyo.
Baada ya Dkt. Janabi alifata Mkuu wa Mkoa wa Dar, Amos Makalla ambae ameongea kwa mara ya kwanza leo mbele ya Rais tangu kuteuliwa. Amos Makalla amemshukuru Rais Samia kumteua kuwa mkuu wa Mkoa wa Dar na kusema kwake ni nyumbani sehemu aliyozaliwa na kukulia. Makalla ameahidi kuendelea kukomesha Ujambazi Dar es Salaam.
Kisha akafata mkuu wa bodi ya Taasisi ya Jakaya Kikwete na kuelezea ndoto zake za kutibu magonjwa ya Moyo nchini na wengine kumkejeli mpaka ndoto zake kuwa kweli. Mwenyekiti ameelezea ndoto yake ya kuweza kuwa na watu mikoani watakaokuwa na uwezo wa kutibu magonjwa ya Moyo.
Anaongea Rais Samia na anasema kazi anayozindua leo ilifanyika awamu ya Tano na kumpongeza Hayati Rais Magufuli. Rais Samia amesema ameona uchawi unaofanyika ndani ya taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete. Amesema Tanzania inajisifu kwa kupunguza vifo vya watoto.
Rais Samia amesema eneo la Jakaya Kikwete limesaidia kupunguza vifo vya watoto. Amesema wagonjwa 5959 wamepata matibabu na watu 11 pekee wamefariki baada ya Upasuaji ikiwa ni asilimia 0.2 pekee. Ameongeza kusema mitambo pekee haitoshi kwani inaongozwa na watu na kuitumia ipasavyo.
Anasema ukisikia kusimamishwa moyo unakufa kabla haujasimamishwa lakini ndani ya taasisi ya Jakaya Kikwete unasimamishwa mpaka masaa sita.
Ameeleza kuzibeba changamoto zao na wanaenda kuzifanyia kazi.
Rais Samia amesema mcheza kwao hutuzwa na serikali itaangalia Maslahi yao.
Rais Samia Suluhu amewaahidi Bilioni mbili kutoka Serikalini kama walivyoomba kwa ajili ya kujenga jengo jipya, wao Taasisi ya moyo watatoa bilioni 2 kukamilisha bilioni 4 kwa ajili ya ujenzi huo