Rais Samia Suluhu, matatizo waliyonayo Watanzania ni ajira kwanza na siyo nyongeza kwa watumishi wa umma ambao ni 0.6% ya Watanzania

Hiyo laki nne unaitoa wapi? Ni jumla ya watumishi wote walioajiriwa kwenye private na public sector ambao wanakatwa PAYE?
 
Haya ya kumpigania yametoka wapi ?!. Ndiyo kujipendekeza kwenyewe huko !!.
 
Mtoa mada ni hopelessly, hongezeko la mshahara au cheo ni suala la kisheria sio hisani , kingine serikali mbona ishasema inaajiri walimu na watumishi wengine
 
Sasa unaonaje kuhudumiwa na daktari hana nauli ya kumrudisha nyumbani kwake na hajui atakula nini akiwa kazini au baada yakurudi nyumbani,wakati huo anawaza ada ya mwanae.
 
Hiyo ajira unayoiomba ndiyo watumishi wenyewe wa Umma.
 
Watu mnaosema serikali haiwezi kuajiri watu wote ni kweli. Lakini ukweli ni kwamba Tanzania bado inahitaji kubwa la watumishi wa umma kwahiyo suala kuajiri halikwepeki.

Itakapofikia serikali inawatumishi wa kutosha kila idara hapo ndyo tutakubaliana kwamba haina haja ya kuajiri au haiwezi kuajiri wengine, lakini kwasasa serikali inauhaba wa watumishi.

Labda tu niwaulize swali watu mnaosema serikali haiwezi kuajiri kila mtu; mnasema hivyo kwasababu serikali haina pesa au inawatumishi wa kutosha?

Kama sababu inawatumishi wa kutosha basi watanzania ni watu wanafiki sana. Kuna watu wapo vijijini huko zahanati hazina watumishi wa kutosha, kuna shule hazina walimu, kuna halmashauri hazina wataalamu mbalimbali. Hawa watu wa vijijini wanakosa huduma nyingi muhimu huku nyinyi mkineng'eneka kuwa serikali haiwezi kuajiri kila mtu.
 
Hii vita ni kali jamani!😂😂😂

Wakati kuna kijana ana miaka 6 mtaani hajawahi kukanyaga ofisi yeyote kulipwa hata hio laki 4.50 walau aweze kujitegemea kimaisha bado ame Tag ubavu nyumbani kwao,,,kuna mtu ambaye toka 2005 yupo ofisini na analilia benefit zaidi ikiwa kashakopa na kujenga kwake na ana kigari cha kutembelea! Maisha yake yamenyooka ila pia anaona haitoshi aongezewe hela hao walioko mtaani watajijua wenyewe! Hii ni level ya ubinafsi ya kiwango cha Chama cha Majambazi! Hapa ndipo tumefikia kama taifa.

Mtu huyu anashupalia vijana wajiajiri ila yeye per diem iongezwe, cheo chake kipande alipwe zaidi 😁😁😁 nimpongeze mama kwa wazo zuri ni bora asie na pakuanzia ndio azingatiwe kwanza.
 
Mataga bana,mbona wakati wa Jiwe hamkuongea haya mlisema mishahara inatosha na vijana wajiajiri na hizo hela ajenge maflyover na barabara kila sehemu.
Vijana wamekuwa vigeugeu kwa kushindwa kutumia akili za darasani hata zile za asili wanakubali kudanganywa na hata kuyumbishwa kamatiara na wanasihasa.
 
Acha uongo wewe si mfuasi wa mama Samia, wewe ni mfuasi kindakindaki wa jiwe na umeibuka humu wakati wake hilo moja,

Pili, Kwanini timu jiwe hampendi wenzenu kupewa nyongeza ya mshahara? Hilo ni takwa la kisheria.

Ajira mpya isiwe mbadala wa wenzenu kuacha kuongezewa mshahara.

Mama afanye jitihada ya kufufua uchumi wa sekta binafsi maana ndio inaajiri watu wengi, wataobaki wataajiriwa serikali, watakaobaki watajiajiri kama uchumi utakua stimulated.
 
Acha hizo!!! Yaani wewe huna ajira kwa hiyo wenye ajira wanyanyaswe tu kila siku. Na wewe ukiajiriwa hutaongezwa mshahara na maisha yanazidi kupanda utaona joto ya jiwe!!!
 
Acha hizo!!! Yaani wewe huna ajira kwa hiyo wenye ajira wanyanyaswe tu kila siku. Na wewe ukiajiriwa hutaongezwa mshahara na maisha yanazidi kupanda utaona joto ya jiwe!!!
Kwanini usitoke ukajiajiri ili mambo yaweze kuwa mepesi zaidi ukaachia walioko mtaani nao waingie kusaka mitaji?
 
Kwanini usitoke ukajiajiri ili mambo yaweze kuwa mepesi zaidi ukaachia walioko mtaani nao waingie kusaka mitaji?
Shida ilikuwa nayo ukitoka huku mtaani Napo ubambikiwe makodi natozo zakukufilisi kabisa.
 
Kwanini usitoke ukajiajiri ili mambo yaweze kuwa mepesi zaidi ukaachia walioko mtaani nao waingie kusaka mitaji?
Waingie kwa fani zao siyo kwa mtu kacha kazi. Mbona serikali inatangaza sana kazi!!!!! Apply tu kupitia utumishi portal. Nilipo hapa wafanyakazi wageni wengi tu wanakuja kwa sifa zao. Kazi zipo na serikali inaajir tu. Siyo kwa mimi kuacha kazi.
 
Waingie kwa fani zao siyo kwa mtu kacha kazi. Mbona serikali inatangaza sana kazi!!!!! Apply tu kupitia utumishi portal. Nilipo hapa wafanyakazi wageni wengi tu wanakuja kwa sifa zao. Kazi zipo na serikali inaajir tu. Siyo kwa mimi kuacha kazi.
Yani pengine huridhishwi na mshahara yani si unaweza toka ukaja pambania kombe mtaani braza?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…