Rais Samia Suluhu, usiige yote aliyofanya mtangulizi wako, wala ushauri wa wachache ndani ya chama chako. Fanya matakwa ya Wananchi na sheria

Rais Samia Suluhu, usiige yote aliyofanya mtangulizi wako, wala ushauri wa wachache ndani ya chama chako. Fanya matakwa ya Wananchi na sheria

nguruka wa kig0ma

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2020
Posts
2,946
Reaction score
2,932
Saalam,

Wewe ni Rais wa Watanzani wote, waliona vyama na wasionavyo walio na dini na wasio nazo. Wenye elimu, na wasio na elimu ambao ni wengi. Matajiri na masikini ambao ni wengi.

Wananchi wa Tanzania wanahitaji Katiba mpya ambayo itawahakikishia Uhuru wa kweli wa kuamua mambo yao na kupata haki zao.

Wapo wakubwa ndani ya chama chako hawataki kabisa kusikia neno katiba mpya au tume huru ya uchaguzi, wanajali matumbo yao na siyo ya masikikini walio wengi.

Alipoingia Magufuli watu wengi tulimtegemea na kutegemea kuwa atarejesha mchakato wa katiba iliyokwamishwa na CCM kwa masilahi yao.

Kuamini kule kulitokana na kama tuliona uchungu aliokuwa nao magufuli juu ya wanyonge na pesa za umma, kumbe alikuwa anatuchezea Karata tatu.

Tulio na akili nyingi tulipoona ameanza na kununua midege kwa pesa taslim,akaanza kujenga reli nk,tukajua katiba mp ya bye bye.

Nae alisema Kama ulivyosema wewe tofauti yenu ni sentensi tu,lakini maana ni moja.

NUKUU
Magufuli alisema Katiba mpya siyo kipaumbele chake. Tumuuache anyooshe nchi. Akasahau mabilioni ya fedha zetu zilizotafunwa kwenye kukusanya maoni na bunge la Katiba, ULE NI UFISADI

Wewe umesema tukuache urekebishe nchi. Je, jasho letu tulilovuja wakati tunatafuta pesa zilizokusanywa na kutumika kwenye mchakato ule limedondoka bure chini ya ardhi?

Kwa bahati mbaya sana watanzania wengi hawajui kuwa pesa zinazotumika na serikali zinatokana na wao,wangejua wangedai

Nakushauri
Yapo mambo ya kuwapendeza CCM, pia yapo mambo yakupasa kufuata matakwa ya wananchi bila kushauriwa. Turudishie rasimu ya Warioba ambayo ni maoni na matakwa yetu. Kwa kufanya hilo utakuwa umerekebisha nchi hii kizazi hiki na vizazi vijavyo.
 
Hiyo ya warioba ipitie vizuri mkuu na yenyewe haijakaa vizuri. Inawezekanaje mbunge akihanama chama kama alikuwa mbunge ahame na ubunge wake huoni ni kuwasaliti wananchi kutokana na sera alizonadi kupitia chama chake.
 
Lipumba akawaita CCM interahamwe halafu wakatoka nje na ukawa ukazaliwa, baadae anakwenda kuonana na Magu ikulu kama vile hajashiriki kuuharibu mchakato wa katiba.

Wanasiasa ni watu hatari sana muda wowote wanaweza kufanya maamuzi yanayoathiri mamilioni ya watu.
 
Hiyo ya warioba ipitie vizuri mkuu na yenyewe haijakaa vizuri ! Inawezekanaje mbunge akihanama chama kama alikuwa mbunge ahame na ubunge wake huoni ni kuwasaliti wananchi kutokana na sera alizonadi kupitia chama chake
Siyo kwamba haina mapungufu Bali kwa kiasi kikubwa inamfanya mwananchi kushiriki maamuzi.

Mapungufu yarejebishwe
 
Samia ana uchaguzi binafsi, ama awe rais wa CCM au rais wa Tanzania.

Akiamua kuwa rais wa CCM atapiga marktime na urais wake utakuwa hauna impact yoyote.

Akiamua kuwa rais wa Tanzania, urais wake utatusaidia kupiga hatua moja mbele, ataisadia nchi na tutakuwa na maendeleo.

Kama ni rais wa Tanzania anapaswa aangalie mahitaji halisi ya watanzania katika nyakati hizi na zijazo!

Kama kwenye ishu ya katiba anahofu ishu ya serikali mbili au tatu, hilo linazungumzika..

Aitishe bunge la katiba liboreshe rasimu ya Warioba tupate mifumo bora zaidi ya haki, halafu hilo la serikali tatu tuliache mpaka muda wenyewe utakapoamua!
 
Kuna maoni kuwa SSH achague kuwa Rais wa Tanzania au wa CCM
Tatizo huwezi tengenisha taasisi ya urais na ccm...yuko pale kutimiza matakwa ya MACCM
Ili awe Rais wa Watanzania wote lazima ashupaze shingo kweli kweli,
Anaweza kuwa na nia njema lakini siwaoni ccm wakimpa hiyo nafasi
 
Back
Top Bottom