Rais Samia, tunahitaji uruhusu nasi tupokee pesa kutoka Paypal kama wanavyofanya wakenya

Rais Samia, tunahitaji uruhusu nasi tupokee pesa kutoka Paypal kama wanavyofanya wakenya

McMahoon

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2017
Posts
1,353
Reaction score
1,639
Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan,

Pole na majukumu ya kuongoza nchi na pia hongera kwa kazi nzuri unayofanya kuifanya nchi yetu inakua kiuchumi na kuwa na amani.

Kwa sasa dunia ni kijiji, unaweza kufanya kazi na mtu yoyote aliyeoko nje ya nchi.
Tuna tatizo la ajira kwahiyo vijana wengi wamekimbilia kujiajiri wenyewe na wengine kutoa huduma mtandaoni.

Ila ugumu unakuja kwenye kupokea malipo, tunahangaika sana. Nimekosa hela nyingi sana mpaka moyo unauma.

Mfano mtu yupo Ghana, India au Hungary anahitaji huduma yako na gharama yake ni fedha za kitanzania ni shiling 8,000 kila moja. Huyu mtu anahitaji kukulipa, atafanyaje ili akulipe? Sidhani kama mtu ataenda Western Union akutumie fedha yenye thamani ya shiling 8,000 za kitanzania.

Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, tunahitaji usikie kilio chetu, uruhusu nasi, tupokee pesa kutoka paypal kama wanavyofanya wakenya. Wewe ni mama mwenye upendo, unawapenda wananchi wako na nchi yako. Na imani utasikia kilio chetu na utalifanyia kazi.

Kama wakenya wameweza, nasi tunaweza.
 
ungetumia mfano wa nchi nyingine huwa hatupendi kuambiwa kenya wamefanya nasi tuige😀😀😀

Hili swali ilulizwa Bungeni naibu waziri wa fedha alijibu bila kupepesa macho-Pay Pal hawajaomba kusajiliwa Tanzania
 
Acha kusubiri hadi hao wajinga wafanye nenda Nairobi Moi avenue pale sajili safaricom yako kwa passport yako Kisha lipia 20k TSH itakuwa active mwaka mzima bila kuzimwa na baada ya hapo fanya mihamala kama kawaida kuweka na kutoa PayPal bila shida yoyote Ile ukisema usubiri watatuchelewesha hawa

IMG_20230801_165301.jpg
 
Hapa nimepata mteja kutoka Guinea. Amehangaika kutafuta njia ya kunilipa km masaa mawili. Hatimaye amepata njia ya kuongeza salio.

Imeingia 5,000 kama salio la kawaida kama vile unapoenda kwa Mangi ukatoa hela, ukapewa vocha ukajaza. Bado haijanisaidia.

Hii hela ingeingia kwenye paypal nikatoa kwenye mpesa ingesaidia hata kununua umeme.

Utafute mtu wa kumuuzia salio la kawaida nayo ni kazi ngumu sana.
 
Back
Top Bottom