DOKEZO Rais Samia tupia jicho Mamlaka ya TBS, WMA wawajibike, vifaa vingi vya ujenzi vinavyozalishwa Viwandani havina ubora

DOKEZO Rais Samia tupia jicho Mamlaka ya TBS, WMA wawajibike, vifaa vingi vya ujenzi vinavyozalishwa Viwandani havina ubora

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Nyakijooga

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2018
Posts
276
Reaction score
473
Mimi kazi zangu zinahusisha biashara chuma, bati n.k kwa ufupi vitu vinavyoendana na material hayo, ujumbe wangu huu uwafikie wahusika wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na Wakala wa Vipimo (WMA), najua wao wapo kwa ajili ya kutusaidia Watanzania lakini inavyoonekana baadhi ya maafisa wao wanachofanya ni kama kushibisha matumbo yao.

Nasema hivyo kutokana na kinachoendelea kwenye Ulimwengu wa taaluma yetu hii, hawa Wamiliki wa viwanda vya Chuma na bati wengi wao wanatengeneza vitu vingi vyenye ubora wa chini.

Zamani bomba zilikuwa zina urefu wa Mita 6 au Futi 20 na ujazo wake ulikuwa mzito tofauti na ilivyo sasa.

Kwa sasa hata Mita 5 hazifiki, unakuta bomba in Sentimita 470 mpaka 480, hapo inategemeana na kiwanda, istoshe ni vyepesi kupita maelezo.

Swali ninalojiuliza hawa TBS hawajui haya yanayoendelea au wanachofanya ni kuangalia tu kwa macho bila kujali vipimo?

Nimemtaja Rais Samia kwa kuwa najua ana nguvu ya kutoa kauli kwa faida ya Taifa, watendaji wake wengi wa chini wakiwemo TBS na WMA, kwa kuwa najua baadhi ya Maafisa wao wanajua kila kitu kinachoendelea.

Upande wa nondo napo hali ni hiyohiyo, inatakiwa kuwa futi 40 lakini urefu haufiki huo, hakuna ubora mzuri, mizigo mingi imekuwa ikingizwa katika mzunguko lakini ubora wake haufai, matokeo yake tunajenga miundombinu isiyokuwa na ubora.

Hali hii inafanywa na viwanda vingi vilivyopo Dar es Salaam, mimi sisemi haya kwa kuwa nasikia bali kwa kuwa ndio maisha ninayoyaishi, ninafanya biashara na ninaona mizigo inayoingia na tunaowauzia wengi hawajui masuala ya ubora.

Nimeamua kusema hayo ili kuokoa Nchi yangu, kwani mimi nikianza kusema inamaanisha hata biashara yangu itakufa na ninaweza kuwa hatarini.

Wananchi wa kawaida hawajui ila mafundi wengi wanajua kinachoendelea lakini nao hawafanyi chochote kwa kuwa ndio ajira zao.

Namuomba Rais Samia atume watu wake wafuatilie kinachoendelea, inawezekana tukaona madaraja, nyumba na hata miundombinu ya ofisi ikichoka mapema au kuharibika mapema, lakini shida ni vifaa vilivyotumika wakati wa ujenzi.

Wito wangu kwa Rais Samia, elekeze ufanyike uchunguzi wa suala hili na baadhi ya maafisa wa taasisi hizo wachunguzwe kwa kuwa wengi wao wanaoingia ‘field’ kufanya ukaguzi wanajua kinachoendelea.

Pia soma ~ Wakala wa Vipimo (WMA) kufanya uhakiki wa Mita za Umeme, Maji na Mabando ya Simu
 
Mimi kazi zangu zinahusisha chuma, bati n.k kwa ufupi vitu vinavyoendana na material hayo, ujumbe wangu huu uwafikie Shirika la Viwango Tanzania (TBS),Wakala wa Vipimo (WMA) najua wao wapo kwa ajili ya kutusaidia Watanzania lakini inavyoonekana baadhi ya maafisa wao wanachofanya ni kama kushibisha matumbo yao.

Nasema hivyo kutokana na kinachoendelea kwenye Ulimwengu wa taaluma yetu hii, hawa Wamiliki wa viwanda vya Chuma na bati wengi wao wanatengeneza vitu vingi vyenye ubora wa chini.

Zamani bomba zilikua zina urefu wa Mita 6 au Futi 20 na mm yake ya ujazo ilikuwa nzito tofauti na ilivyo sasa.

Kwa sasa hata Mita 5 hazifiki, unakuta bomba in Sentimita 470 mpaka 480, hapo inategemeana na kiwanda, istoshe ni vyepesi kupita maelezo.

Swali ninalojiuliza hawa TBS hawajui haya yanayoendelea au wanachofanya ni kuangalia tu kwa macho bila kujali vipimo.

Upande wa nondo napo hali ni hiyohiyo, inatakiwa kuwa futi 40 lakini urefu haufiki huo, hakuna ubora mzuri, mizigo mingi imekuwa ikingizwa katika mzunguko lakini ubora wake haufai, matokeo yake tunajenga miundombinu isiyokuwa na ubora.

Hali hii inafanwa na viwanda vingi vilivyopo Dar es Salaam, mimi sisemi haya kwa kuwa nasikia bali kwa kuw andio Maisha ninayoyaishi, ninafanya biashara na ninaona mizigo inayoingia na tunaowauzia wengi hawajui masuala ya ubora.

Nimeamua kusema hayo ili kuokoa Nchi yangu, kwani mimi nikianza kusema inamaanisha hata biashara yangu itakufa na ninaweza kuwa hatarini.

Wananchi wa kawaida hawajui ila mafundi wengi wanajua kinachoendelea lakini nao hawafanyi chochote kwa kuwa ndio ajira zao.

Namuomba Rais Samia atume watu wake wafuatilie kinachoendelea, inawezekana tukaona madaraja, nyumba na hata miundombinu ya ofisi ikichoka mapema au kuharibika mapema, lakini shida ni vifaa vilivyotumika wakati wa ujenzi.

Wito wangu kwa Rais Samia, elekeze ufanyike uchunguzi wa suala hili na baadhi ya maafisa wa taasisi hizo wachunguzwe kwa kuwa wengi wao wanaoingia ‘field’ kufanya ukaguzi wanajua kinachoendelea.
TBS imepata kigugumizi, chura kiziwi,ni shida,naye TBS hana
 
Mpaka apatikane mtu wa kuminya gololi wahindi ndio mambo yatakaa sawa inchi hii

Kwa vibaraka wanaotegemea mpaka pesa za uchaguzi kutoka kwao sahau

Dah, ukweli mchungu.

Ukishaona uchumi wa nchi uko chini ya Indians na Arabs tambua tu kwa kiasi kikubwa watu wa hiyo nchi watakuwa wako utumwani.

Bahati Mbaya ndio wafadhili wa chama chetu CCM.
 
Tatizo likingine liko kwa wanywaji wa pombe, pombe nyingi mtaani hasa pombe kali + imported beers, nyingi ni feki.
 
Hongera kwa kuliibua Hili
Nondo ya 16mm BS300 local made inaweza kulingana hiko kipimo na Na 12mm BS500 imported

Fundi chuma hawalalamiki kwasababu kwao kazi ya kukunja inakua rahisi kwa chuma chepesi,
Kwa wakati huu ni bora uwe unanunua BS500 nafsi yako itaridhika, TBS na WMA sidhani kama wana wataalamu na mashine za kupimia hizi indifference na low quality
 
Hongera kwa kuliibua Hili
Nondo ya 16mm BS300 local made inaweza kulingana hiko kipimo na Na 12mm BS500 imported

Fundi chuma hawalalamiki kwasababu kwao kazi ya kukunja inakua rahisi kwa chuma chepesi,
Kwa wakati huu ni bora uwe unanunua BS500 nafsi yako itaridhika, TBS na WMA sidhani kama wana wataalamu na mashine za kupimia hizi indifference na low quality
Maabara zipo Mkuu pale Udsm, C lab Magomeni, Central laboratory pale Keko n.k tena Wana vifaa vya kisasa, kwa Sasa Tanroads na Tarura pia Wana vifaa
 
Nami nakwambia kwamba


Ukitaka kijana wako atoboe mapema, basi mfanyie mpango apate ajira WMA, TBS, TRA, EWURA, TPDC
 
Ogopa sana nchi viongozi wakisimama kazi Ni kumsifia rais kama vile wao hawana la kufanya,
Kwa bati kiwanda kilichobaki kwa uaminifu Ni Alaf tu.
 
Wito wangu kwa Rais Samia, elekeze ufanyike uchunguzi wa suala hili na baadhi ya maafisa wa taasisi hizo wachunguzwe kwa kuwa wengi wao wanaoingia ‘field’ kufanya ukaguzi wanajua kinachoendelea.
POLE sana Mkuu.

FYI, Kwasasa hii nchi Rais ndio anapewa maelekezo na sio yeye ndio anatoa maelekezo.

Tanzania imekuwa Taifa la Kambare, kila mtu ana NDEVU.

Be a Man, tunashukuru kwa kutuamsha ambao tulikuwa hatujui. Na huo ni Uzalendo.
 
Mimi kazi zangu zinahusisha chuma, bati n.k kwa ufupi vitu vinavyoendana na material hayo, ujumbe wangu huu uwafikie Shirika la Viwango Tanzania (TBS),Wakala wa Vipimo (WMA) najua wao wapo kwa ajili ya kutusaidia Watanzania lakini inavyoonekana baadhi ya maafisa wao wanachofanya ni kama kushibisha matumbo yao.

Nasema hivyo kutokana na kinachoendelea kwenye Ulimwengu wa taaluma yetu hii, hawa Wamiliki wa viwanda vya Chuma na bati wengi wao wanatengeneza vitu vingi vyenye ubora wa chini.

Zamani bomba zilikua zina urefu wa Mita 6 au Futi 20 na mm yake ya ujazo ilikuwa nzito tofauti na ilivyo sasa.

Kwa sasa hata Mita 5 hazifiki, unakuta bomba in Sentimita 470 mpaka 480, hapo inategemeana na kiwanda, istoshe ni vyepesi kupita maelezo.

Swali ninalojiuliza hawa TBS hawajui haya yanayoendelea au wanachofanya ni kuangalia tu kwa macho bila kujali vipimo.

Upande wa nondo napo hali ni hiyohiyo, inatakiwa kuwa futi 40 lakini urefu haufiki huo, hakuna ubora mzuri, mizigo mingi imekuwa ikingizwa katika mzunguko lakini ubora wake haufai, matokeo yake tunajenga miundombinu isiyokuwa na ubora.

Hali hii inafanwa na viwanda vingi vilivyopo Dar es Salaam, mimi sisemi haya kwa kuwa nasikia bali kwa kuw andio Maisha ninayoyaishi, ninafanya biashara na ninaona mizigo inayoingia na tunaowauzia wengi hawajui masuala ya ubora.

Nimeamua kusema hayo ili kuokoa Nchi yangu, kwani mimi nikianza kusema inamaanisha hata biashara yangu itakufa na ninaweza kuwa hatarini.

Wananchi wa kawaida hawajui ila mafundi wengi wanajua kinachoendelea lakini nao hawafanyi chochote kwa kuwa ndio ajira zao.

Namuomba Rais Samia atume watu wake wafuatilie kinachoendelea, inawezekana tukaona madaraja, nyumba na hata miundombinu ya ofisi ikichoka mapema au kuharibika mapema, lakini shida ni vifaa vilivyotumika wakati wa ujenzi.

Wito wangu kwa Rais Samia, elekeze ufanyike uchunguzi wa suala hili na baadhi ya maafisa wa taasisi hizo wachunguzwe kwa kuwa wengi wao wanaoingia ‘field’ kufanya ukaguzi wanajua kinachoendelea.
Naunga mkono hoja ni ukweli mtupu, wasiojua watabisha
 
Mimi kazi zangu zinahusisha chuma, bati n.k kwa ufupi vitu vinavyoendana na material hayo, ujumbe wangu huu uwafikie Shirika la Viwango Tanzania (TBS),Wakala wa Vipimo (WMA) najua wao wapo kwa ajili ya kutusaidia Watanzania lakini inavyoonekana baadhi ya maafisa wao wanachofanya ni kama kushibisha matumbo yao.

Nasema hivyo kutokana na kinachoendelea kwenye Ulimwengu wa taaluma yetu hii, hawa Wamiliki wa viwanda vya Chuma na bati wengi wao wanatengeneza vitu vingi vyenye ubora wa chini.

Zamani bomba zilikua zina urefu wa Mita 6 au Futi 20 na mm yake ya ujazo ilikuwa nzito tofauti na ilivyo sasa.

Kwa sasa hata Mita 5 hazifiki, unakuta bomba in Sentimita 470 mpaka 480, hapo inategemeana na kiwanda, istoshe ni vyepesi kupita maelezo.

Swali ninalojiuliza hawa TBS hawajui haya yanayoendelea au wanachofanya ni kuangalia tu kwa macho bila kujali vipimo.

Upande wa nondo napo hali ni hiyohiyo, inatakiwa kuwa futi 40 lakini urefu haufiki huo, hakuna ubora mzuri, mizigo mingi imekuwa ikingizwa katika mzunguko lakini ubora wake haufai, matokeo yake tunajenga miundombinu isiyokuwa na ubora.

Hali hii inafanwa na viwanda vingi vilivyopo Dar es Salaam, mimi sisemi haya kwa kuwa nasikia bali kwa kuw andio Maisha ninayoyaishi, ninafanya biashara na ninaona mizigo inayoingia na tunaowauzia wengi hawajui masuala ya ubora.

Nimeamua kusema hayo ili kuokoa Nchi yangu, kwani mimi nikianza kusema inamaanisha hata biashara yangu itakufa na ninaweza kuwa hatarini.

Wananchi wa kawaida hawajui ila mafundi wengi wanajua kinachoendelea lakini nao hawafanyi chochote kwa kuwa ndio ajira zao.

Namuomba Rais Samia atume watu wake wafuatilie kinachoendelea, inawezekana tukaona madaraja, nyumba na hata miundombinu ya ofisi ikichoka mapema au kuharibika mapema, lakini shida ni vifaa vilivyotumika wakati wa ujenzi.

Wito wangu kwa Rais Samia, elekeze ufanyike uchunguzi wa suala hili na baadhi ya maafisa wa taasisi hizo wachunguzwe kwa kuwa wengi wao wanaoingia ‘field’ kufanya ukaguzi wanajua kinachoendelea.
Kweli kabisa,ngojea waje wakupinge wajaa laana
 
Back
Top Bottom