Rais Samia, usipofanya haya wewe na chama chako mtaanguka vibaya katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025

Rais Samia, usipofanya haya wewe na chama chako mtaanguka vibaya katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025

Mr Dudumizi

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2020
Posts
7,799
Reaction score
14,215
Kwa heshima na taadhima mama yetu wa Taifa, mkuu wa nchi na amiri jeshi mkuu wa majeshi yote ya ulinzi na usalama napenda kwanza kukusalimu "Kwa Jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania". Ama baada ya salam napenda kutumia nafasi hii kama mtanzania na raia mwema wa nchi yako pendwa ya Tanzania kukushauri mambo fulani, lakini kwa kupenda kwako unaweza ukauchukua ushauri huu wote au baadhi au ukaachana nao kwa jinsi utakavyoona mwenyewe inafaa.

(1) Kitu cha kwanza kabisa ningependa kukushauri mh raisi ni kufuata na kuikamilisha ilani ya chama chenu mliyoahidi kuitekeleza wakati wa kampeni. Mfano kuna miradi mikubwa, yenye tija na faida kubwa kwa nchi ambayo aliekuwa raisi wetu hayati Magufuli alifariki bila kuimaliza, ni vizuri ukaimaliza tena kwa wakati uliopangwa ili wale wananchi wanao nufaika na miradi hiyo waweze kukuchagua au kukichagua tena chama chako mwaka 2025.

Na kumbuka ilani ndio msingi au muongozo wa serikali yoyote iliyopo madarakani, ina maana serikali inayoacha kufuata ilani ya chama chake iliyoahidi mbele ya wananchi, inakuwa kama vile treni inayoacha reli na kutembelea kwenye mchanga. Kwahiyo wewe kama raisi na mwenyekiti wa chama chenu jitahidi sana ukamilishe ahadi ya ilani ili iwe rahisi kuaminiwa tena na wananchi mwaka 2025, na hatimae chama chenu kupata ushindi mnono zaidi ya huu mlioupata mwaka 2020.

(2) Ruhusu mikutano ya vyama vya siasa kwa mujibu wa katiba, lakini vyama hivyo vifanye mikutano yao kwa kufuata sheria, sio mwanasiasa anakosa hoja au sera nzuri za kuwaeleza wanachama wake anaanza kudandia majina ya watu kwa kuwashutumu ufisadi bila kuwa na ushahidi wa tuhuma zake (kama ilivyotokea kwa mh Lowasa, Sumaye nk) unakuta anashutumiwa mtu ufisadi bila ushahidi akienda kuripoti polisi yule mwanasiasa akikamatwa kwa kukosa ushahidi wa tuhuma zake, wafuasi wake wanaingia barabarani kuandamana eti kiongozi wao kaonewa nk.

(3) Lisimamie mwenyewe swala la ajira ili kila anaestahili kupata ajira aipate kwa haki bila kuangaliana undugu, urafiki, ukabila, udini na ukanda.

(4) Simamia haki bila kuangalia huyu anasema nini radioni, gazeti au mitandaoni, maana katika vitu ambavyo huhatarisha usalama wa nchi basi mitandao nayo imo, kwahiyo ni kuwa makini sana na taarifa za mitandaoni.

(5) La mwisho nashauri mh raisi ufanye uteuzi kulingana na taaluma ya mtu ili kuleta ufanisi katika kazi zao. Sina mengi zaidi ya hayo, ni mimi raia wako mwema mr D. Kwa niaba ya TAKWA au kwa kirefu chake "Tanzania Kwanza"
 
Yaani CCM walishaaondoka huko kwenye kuimba kura na kupigiwa kura, wenyewe wsmeshakuwa chama cha kigaidi wezi wa kura na majambazi wa kura daylight robbers.
 
Mbona hamna jipya hapo. anyway mama tutampa tena atake asitake... hivi akiondoka nani atatupa tabasamu?
Mama mikumi tena...au nasema uongo ndugu yangu?
Kweeeeeriiiiiii
 
Mbona hamna jipya hapo. anyway mama tutampa tena atake asitake... hivi akiondoka nani atatupa tabasamu?
Mama 5 tena...au nasema uongo ndugu yangu?
Mama atapata mi5 tena endapo atasimamia katiba, sheria na sera za chama chake kikamilifu. Bila hivyo huenda 2025 ikawa ndo byee byee
 
Wakati wenu nyinyi umeisha.
Kubalini kuwa mfadhili wenu kashawatoka.
 
Mama atapata mi5 tena endapo atasimamia katiba, sheria na sera za chama chake kikamilifu. Bila hivyo huenda 2025 ikawa ndo byee byee
Wewe nani ndani ya watu 60m?

Utakesha ukiwanga hapo kwenu chatou lkn hampewi tena nafasi ng'oooo
 
Hakuna cha ushauri hapo bali ni jitihada za sukuma gang kumkwamisha mama Samia.
Sawa Mrs Mwenyekiti, naona umekuja fasta fasta ukizania kuna sehem nimemchafua au kumtaja mwenyekiti wako au mumeo mtarajiwa ili upate la kuongea. Usijali dada pamoja na kuwa mwenyekiti ashaowa lkn mila zetu zinaruhusu kuowa wake zaidi ya mmoja, so utaolewa tu dada angu, punguza munkari.
 
Sawa Mrs Mwenyekiti, naona umekuja fasta fasta ukizania kuna sehem nimemchafua au kumtaja mwenyekiti wako au mumeo mtarajiwa ili upate la kuongea. Usijali dada pamoja na kuwa mwenyekiti ashaowa lkn mila zetu zinaruhusu kuowa wake zaidi ya mmoja, so utaolewa tu dada angu, punguza munkari.
Lazima safari tuwakamue ipasavyo na kundi lenu la sukuma gang.

Mfadhili wenu kesha tangulia mbele ya haki ,hamna mtu wa kuwafadhili nyinyi kundi haramu.
 
Wakati wenu nyinyi sukuma gang umeisha.
Kubalini kuwa mfadhili wenu kashawatoka.
Hawa lazima twende nao sawa, wakati watu wanatungiwa sheria za retention fee, wananyimwa increment, wanatekwa na kupigwa risasi wao walikuwa wanaimba mapambio huku wanavizia uteuzi. Sasa wanaona waliyekuwa wanamsifia hayupo wanajiugeuza washauri. Ni zamu yao kukerekaa, tutawakeraaaaa.
 
Hawa lazima twende nao sawa, wakati watu wanatungiwa sheria za retention fee, wananyimwa increment, wanatekwa na kupigwa risasi wao walikuwa wanaimba mapambio huku wanavizia uteuzi. Sasa wanaona waliyekuwa wanamsifia hayupo wanajiugeuza washauri. Ni zamu yao kukerekaa, tutawakeraaaaa.
Pamoja sana mamy
 
Mwacheni azidi kuacha njia hata wahenga wanasema "ukila na kipofu usimshike mkono" mwacheni aendelee make kasema anaendelea
 
Back
Top Bottom