Hili kwakweli halikubaliki hata kidogo.Ndio maana vijana tunakimbilia mijini na kukidharau kilimo kuona kama hakina tija mana MTU unatumia nguvu nyingi,mtaji mkubwa na unachokuja kukipata hakiendani na uhalisia wa gharama ulizozitumia.
Vijana kukimbilia mijini sio kuwa wanapenda sana Bali ni walau kutafuta unafuu wa maisha.Huwezi kuwafukuza Machinga halafu hujawawekea mpango mbadala wa kuwafanya waendelee kufanya shughuli zao.Serikali ikitaka kuwaondoa bila bughdha waboreshe Kilimo kwa ujumla wake waone kama kuna watu watabaki mjini.