Rais Samia zingatia Sheria kwenye teuzi za Wakurugenzi wa Halmashauri, Miji, Manispaa na Majiji

Rais Samia zingatia Sheria kwenye teuzi za Wakurugenzi wa Halmashauri, Miji, Manispaa na Majiji

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Mh. Rais, umekamilisha teuzi za wakuu wa mikoa na wilaya. Na sasa bado nafasi za wakurugenzi wa Halmashauri, miji, manispaa na majiji.

Teuzi zilizotangulia, zilikuwa ni teuzi za ulaji na shukrani kwa sababu kimsingi wakuu wa wilaya na mikoa, tangu enzi za mkoloni, walitumika kama vikaragosi wa mtawala. Kazi yao kubwa ilikuwa kulinda maslahi ya mtawala na siyo wananchi. Hali hiyo, kwa kiasi kikubwa imebakia kuwa hivyo mpaka leo, ndiyo maana wananchi wengi wenye uelewa, wangependelea nafasi hizi zifutwe.

Sasa zimebakia nafasi za wakurugenzi. Hizi ni nafasi muhimu sana maana zinahusu maendeleo ya wananchi. Hizi ni nafasi za kitaalam na kiutendaji. Ndiyo maana sheria zinamwelekeza Rais kuteua wakurugenzi kutoka miongoni mwa watumishi wa umma waliofikia daraja fulani.

Marehemu Magufuli, kwa kiasi kikubwa aliharibu na wala hakuzingatia kanuni za uteuzi. Akazigeuza nafasi za wakurugenzi kuwa za kisiasa, na hivyo sehemu nyingi akawaweka makada badala ya kuwaweka wataalam.

Ombi letu ni kukuasa Mh. Rais, kurudi kwenye kanuni na sheria inayokutaka kumteua mtu kuwa mkurugenzi kwa kufuata vigezo vilivyowekwa kisheria kuliko kuangukia kwenye dimbwi la uchafu lililoachwa na marehemu, la kutofkufuata sheria na kanuni.

Kiongozi makini huonesha njia. Kiongozi ni lazima uoneshe mfano katika kuzingatia sheria na kanuni kabla ya kuwataka wanaokufuata kufanya hivyo.
 
Azingatie sheria zipi? Nyie watu mbona wabinafsi sana? Wenzangu wakiteuliwa, uteuzi ni mbaya, ila nyie mlioteuliwa..

Acheni ujinga!
 
Maoni yako ni Mazuri. Lakini sio kila aliyeko kwenye siasa hawezi kuwa mkurugenzi. Wengine wengi tu wameingia kwenye siasa baada ya kuacha Kazi zao za kiserikali na bado wanafaa kurudishwa.
 
Mama ana tafuta huruma ya 2025 hata amini majicho pale mwenyekiti mwenyewe atakavyo katwa
 
Et anadai ameteua vijana.

Sawa ni Vijana, ila Vijana wa aina gan?

Unateua Kijana ambaye, RAS na DED siku zote wataendelea kumfanya Hayawani?

Ukiingia Bungeni karibu 90% ya wabunge wa CCM ni vilazaaaaaa kupindukia nandio watunga Sheria

Unakuja kwa Ma DC na ma RC, vilaza vilazaa

Et watu kama akina Pascal Mayalla hawaonwi?? Watu ambao wanaupeo wa kuona Miaka mitatu, mitano mbele?

HAKA KAMAMA, KATIBA TU NDO IMEKABEBA, ILA HAMNA KITUUUUUUU.
 
Kwa hiyo wewe ndo unaakili sana sio? unampangia Rais cha kufanya na kuwaita wateuliwa wa Rasi Magufuli kama uchafu Unamawazo mazuri lakini ufahamu kila mtu na mapungufu yake ustarajie kila atakaye teuliwa atakuwa perfect.

Nyie ndo mmegeuka kuwa wapiga mapambio huku mkitukana marehemu na kukashifu kila alichofanya kana kwamba Rais Samia yeye ni mwema na mkamilifiu sana. Mimi naona kitu kikubwa ni uzalendo bila uzalendo hata kama ukuwa naujuzi kiasi gani huwezi kutoa matokeo na itabaki ni ubabaishaji tu.
 
Azingatie sheria zipi? Nyie watu mbona wabinafsi sana? Wenzangu wakiteuliwa, uteuzi ni mbaya, ila nyie mlioteuliwa..

Acheni ujinga!
Nebuchadinezzer ungekaa kimya tusingejuwa kuwa wewe popoma. Rudi soma andiko tena. Mtoa mada anamtahadharisha Rais SSH kuwa atakapoteua Wakurugenzi wa Majiji, Miji na Halmashauri asifanye kosa alilofanya Mwendazake kwa kuwaweka makada kwenye nafasi hizo.

Kwa mujibu wa Sheria ya Utumishi Namba 8 ya mwaka 2002, nafasi ya DED na DAS ni ya Utumishi na siyo ya uteuzi. Mtanzania anaye kuwa na sifa za kitaalamu ndiye anateuliwa aidha kwa m mchakato ndani ya TAMISEMI au kwa kutangaza kwenye public notice
 
Sheria inamruhusu Rais kummteua mtanzania yeyote anayejua kusoma na kuandika kushika nafasi yeyote ndani ya serikali. Musukuma ni mbunge lakini pia anaweza kuteuliwa kuwa waziri au naibu waziri.
 
Kwa hiyo wewe ndo unaakili sana sio? unampangia Rais cha kufanya na kuwaita wateuliwa wa Rasi Magufuli kama uchafu Unamawazo mazuri lakini ufahamu kila mtu na mapungufu yake ustarajie kila atakaye teuliwa atakuwa perfect. Nyie ndo mmegeuka kuwa wapiga mapambio huku mkitukana marehemu na kukashifu kila alichofanya kana kwamba Rais Samia yeye ni mwema na mkamilifiu sana. Mimi naona kitu kikubwa ni uzalendo bila uzalendo hata kama ukuwa naujuzi kiasi gani huwezi kutoa matokeo na itabaki ni ubabaishaji tu.
Hebu jitathmini Ubongo wako kama upo maana unaropoka tu. Hii mada siyo ya hadhi yako soma upite au uliza ueleweshwe.

Haina ubishi, Mwendazake aliteua makada wa CCM waliokuwa namba 2 kwenye kura za maoni ndani ya CCM au walioshidwa na upinzani kwenye uchaguzi mkuu wa 2015 na kuwafanya ma DED na ma DAS.

Hiyo siyo sawa na ni kinyume cha Katiba ya JMT ya mwaka 1977 toleo la 2000 inayosema Mtumishi wa Umma hatakuwa mwanachama wa Chama cha Siasa.
 
Et anadai ameteua vijana.

Sawa ni Vijana, ila Vijana wa aina gan?

Unateua Kijana ambaye, RAS na DED siku zote wataendelea kumfanya Hayawani?

Ukiingia Bungeni karibu 90% ya wabunge wa CCM ni vilazaaaaaa kupindukia nandio watunga Sheria

Unakuja kwa Ma DC na ma RC, vilaza vilazaa

Et watu kama akina Pascal Mayalla hawaonwi?? Watu ambao wanaupeo wa kuona Miaka mitatu, mitano mbele?

HAKA KAMAMA, KATIBA TU NDO IMEKABEBA, ILA HAMNA KITUUUUUUU.
Pascal mayala yupi huyoo? Huyoo anaerusha makala kwenye magazeti kila uchao! Huyuu asiekuwa na msimamo katika taaluma yake? Binafsi nilimkubal alipoenda ikulu na kipind jpm anaanza kaz..aliuliza swal makini sana..ila baada ya njaa kumzid na kupima upepo wa teuzi akaanza kuimba mapambio..hapo ndipo pascal wangu niliekuwa namjua alitokomea kusikojulikana hadi leo hii..
 
Nafasi za ukurungezi awakumbuke watumishi wa umma walio makada wa chama. Mfano watumishi wa umma waliogombea nec Taifa mwaka 2017 na ubunge mwaka 2020 hao wanatosha kuwa wakurungenzi. Watumishi hao pamoja na kugombea walikichagia chama na walikatwa mishahara yao kwa miezi mitatu . Na sifa za kuwa wakurungenzi wanazo. Waliopo kwa sasa hawaña sifa
 
Back
Top Bottom