Rais Senegal aagiza leo mapumziko ya taifa kusherekea ubingwa wa AFCON

Rais Senegal aagiza leo mapumziko ya taifa kusherekea ubingwa wa AFCON

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Rais wa Senegal Macky Sall, ametangaza leo Jumatatu Februari 7, 2022 kuwa ni siku ya mapumziko maalum nchini kwake kwa ajili ya kusherehekea ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika #AFCON2021 waliochukua usiku wa kuamkia leo kwa kuifunga Misri kwa penati 4-2.

Sall, alikuwa njiani kwenda katika ziara nchini Comoros ambapo baadaye angeelekea, Misri na Ethiopia, lakini amesitisha ziara hiyo ili awapokee wachezaji hao wanaowasili nchini humo kutoka Cameroon.

Senegal waliongozwa na staa wa Liverpool, Sadio Mane ambaye alifunga penati ya ushindi katika ushindi wa penati 4-2 dhidi ya Misri iliyokuwa ikiongozwa na Mohamed Salah katika fainali, usiku wa kuamkia leo.

Copy-of-.jpg
 
Aisee! Mwaka 1993 Mzee Mwinyi ilibaki kidogo atangaze Jumatatu siku ya mapumziko kama Simba SC wangeifunga Stella Abidjan ya Ivory Coast na kubeba ndoo ya Kombe la Washindi Barani Afrika wakati huo likiitwa Kombe la Mashood Abiola.

Lakini waapi banaaa. Ng'ombe wa masikini hazai! Simba ilipigwa na kitu kizito kichwani mashabiki na nchi nzima tusijue kilichotupata! Jean Boli Zozo akakatisha furaha yetu. Anyways Azim Dewji anajua zaidi alichokifanya
 
Mwinyi Yanga lia lia alifurahi kimoyo moyo sana siku ile
Aisee! Mwaka 1993 Mzee Mwinyi ilibaki kidogo atangaze Jumatatu siku ya mapumziko kama Simba SC wangeifunga Stella Artois ya Ivory Coast na kubeba ndoo ya Kombe la Washindi Barani Afrika wakati huo likiitwa Kombe la Mashood Abiola.

Lakini waapi banaaa. Ng'ombe wa masikini hazai! Simba ilipigwa na kitu kizito kichwani mashabiki na nchi nzima tusijue kilichotupata! Jean Boli Zozo akakatisha furaha yetu. Anyways Azim Dewji anajua zaidi alichokifanya
 
Back
Top Bottom