Rais Uhuru hadi sasa ametimiza kura 7,263,496 kidogo zifikie idadi yake ya mwanzo

Rais Uhuru hadi sasa ametimiza kura 7,263,496 kidogo zifikie idadi yake ya mwanzo

MK254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
32,408
Reaction score
50,809
Kwa mujibu wa matokeo yanayotiririka kutokea maeneo mbali mbali ya nchi, tarakimu zinaonyesha rais Uhuru ametimiza 7,263,496, idadi hii imebakia kidogo tu kufikia milioni nane alizokua nazo kwenye uchaguzi wa mwanzo.

Japo pia inaeleweka changamoto za kutotimiza ni kwamba
- Kwenye kinyang'anyriro maalum cha mwanzo, maelfu ya Wakenya walisafiri kwenda vijijni kupiga kura, lakini ni wachache walisafiri kwenye zoezi hili la marudio.
- Kuna wengi pia hawakua na hamasa ya kujitokeza kupiga kura kwa kauli kwamba mshindani alikua mmoja, hawakuona haja ya kuhangaika kwenye mafoleni.
- Maeneo yenye wafuasi wa Raila yalishuhudia uhuni wa kila aina. Vijana walifunga kabisa gatuzi nne zenye wapiga kura zaidi ya milioni
- Pia kuna maeneo kama Bungoma ambapo waliopiga kura waliamka na kukuta nyumba zao zimetiwa alama ya rangi nyekundu kama ishara kwamba wajiandae kwa mtiti ujao

Lakini pia pamoja na yote hayo, wafuasi wa Raila nje ya Nyanza walisusia kabisa na hawakupiga kura, hivyo nchi imegawanyika. Juzi Raila ameagiza wakae mkao wa mapambano na kwamba wasusie huduma zote za makampuni yenye ushirikiano wa aina yoyote na serikali.

Kwa kifupi, mapambano haya ya siasa hayataisha hivi karibuni, wananchi wa chini kama kule Kibera wajiandae kwa hali na mali maana kuna mikimbio ya kila siku hadi mmoja wa hawa mafahali wawili atakapochoka na kuiachia nchi iendelee mbele.


Kenya Elections 2017 - Daily Nation
 
Jubilee= Ccm.


Jana Nilimtazama mwanamama mmoja wa kisumu akinena .." UHURU MUST GO"
 
Nchi iliyojaa ukora huku wakijinadi na katiba nzuri
 
Kama turnout ilikuwa kidogo hivyo, hizo kura zaidi ya million 7 zimetoka wapi?maswali ni mengi
Si walikuwa vituoni wenyewe? Walikuwa na wakati hata kumpa kila mtu karatasi kumi ajaze peke yake
 
Kwa hapa Africa Laila ndiyo imetoka aliemwambia asishiriki marudio si jui ninani ama kweli akili za mwenzio changanya na zako.
 
Muhimu kwa sasa ni utengemani na amani ya Kenya, hayo ya kura hayatokua na maana kama jamii zitaendelea kuvutana na nchi kugawanyika, kumbukeni kwa sasa nchi ni kama vile imesimama, huwezi kujua kesho itakuaje.
 
Hivi matatu zinaendelea na kazi barabarani??.... Kwa walipofikia, bora kumpumzisha kiongozi mmoja ili wananchi waweze kupata settlement ya kudumu. Tamaa ya kuongoza nchi ndio isababishe watu kupoteza maisha...halikubariki huku Africa...mfyuuuum
 
Aljeezira na CNN si wajinga wakisema turnout ilikuwa less than 35 per cent
tangu lini ukasikia CNN au Aljeezira wakaripoti mema juu ya bara letu tukufu...hawa hata sasa utawakuta mahala oenye fujo kama Kawangware, Kisumu,Migori n.k...huwezi kuwakuta mahala kama Thika, Embu n.k...kwao habari mbaya wakizirusha ni mtaji kwao...mpaka sasa naona tume portal yao ya kura Uhuru ana 4m+ na bado wanaedelea kuhakiki matokeo na ku update
 
Fanya hesabu kama unajua kukokotoa, waliojiandikisha ni milioni 19, waliojitokeza kupiga ni milioni saba.
Hivyo ni wazi turnout ilikua ndogo.... Maana ilikua ya upande mmoja tu, ni hesabu hata mtoto wa chekechea anaweza kukusaidia kukotoa.
....Hivi mshindi anatakiwa apate asilimia ngapi?
 
wacha jamaa aapishwe tuendelee na kazi....wabongo kaeni na maoni yenu ya kipumbavu..pambaneni na magufuli, lowesa lisu na kadhalika....7million votes almost the 8 million that he got in August...
 
Back
Top Bottom