Rais wa chuo cha KCMC asimamishwa masomo mwaka mzima akipigania maslahi ya wanafunzi

Rais wa chuo cha KCMC asimamishwa masomo mwaka mzima akipigania maslahi ya wanafunzi

GIBA KB

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2012
Posts
367
Reaction score
110
Rais wa chuo kikuu cha udaktari cha KCMC Moshi ndugu Telesphory Mula amesimamishwa masomo na uongozi wa chuo icho.

Sababu za yeye kusimamishwa masomo ni kupigania maslahi ya wanafunzi hasa wale wa mwaka wa kwanza MD1 ambao waliongezewa ada.

Rais aliwaandikia barua wanafunzi hao wa mwaka wa kwanza kwamba walipe ada ya zamani kama wanafunzi wanaoendelea.Ikumbukwe TCU ndio inapanga ada za vyuo kupitia STUDENT UNIT COSTS ambao mwongozo huo haujatoka na sababu za kutotoka hazieleweki.

Barua iyo iliwakasirisha sana viongozi wa chuo na kusema amejipa mamlaka ambayo sio yake.Baada ya kukaa kikao cha kamati ya nidhamu,waliamua kumsimamisha masomo kwa mwaka mmoja.

Huyu alikuwa kiongozi wa chuo na kiongozi mwenzetu wa TAHLISO
 
In africa doing adultery is not a sin, a sin comes when u are trying to open the blind to understand whats the truth.
Najua tokea mwaka jana media zilitoa taarifa za President mullah kupinga ongezeko hilo kubwa ambalo halikufata utaratibu wa tume ya vyuo vikuu.
Mamlaka tulizonazo zinaandaa watu watakaokuwa waoga na watumwa kwa watawala.
 
Kiukweli vyuo vya private ubaya wke hapo tu, watu walijaza kwa kuangalia ada ya wakati huo.Sasa unapopandisha katikati ya masomo inakua shida kwa wanafunzi
 
Rais wa chuo kikuu cha udaktari cha KCMC Moshi ndugu Telesphory Mula amesimamishwa masomo na uongozi wa chuo icho.

Sababu za yeye kusimamishwa masomo ni kupigania maslahi ya wanafunzi hasa wale wa mwaka wa kwanza MD1 ambao waliongezewa ada.

Rais aliwaandikia barua wanafunzi hao wa mwaka wa kwanza kwamba walipe ada ya zamani kama wanafunzi wanaoendelea.Ikumbukwe TCU ndio inapanga ada za vyuo kupitia STUDENT UNIT COSTS ambao mwongozo huo haujatoka na sababu za kutotoka hazieleweki.

Barua iyo iliwakasirisha sana viongozi wa chuo na kusema amejipa mamlaka ambayo sio yake.Baada ya kukaa kikao cha kamati ya nidhamu,waliamua kumsimamisha masomo kwa mwaka mmoja.

Huyu alikuwa kiongozi wa chuo na kiongozi mwenzetu wa TAHLISO

Hakuwaandikia barua wanafunzi wa mwaka wa kwanza kuwataka walipe ada ya zamani...yeye hana mandate hiyo. Alichofanya ni kucite barua ya TCU kwa chuo inayowaagiza wasipandishe ada hadi system ya kukadiria ada itapokamilika....baas
 
Kama wanafunzi wenzake mmeamua nn sasa? Gomeni atarudishwa tuu tena mnagoma wote
 
Ha ha mimi naijua sana KCMC ni chuo changu nilifuzu hiyo fani mwaka juzi pale kuna udictator sana huyo Rais ahame tuu kwani lazima wata mdisco tuu wale sio watu kuna vijana wengi walijaribu kufunua vinywa hawakumaliza
 
Back
Top Bottom