Rais Wa Congo na Rwanda Wakwepana

Rais Wa Congo na Rwanda Wakwepana

Movic Evara

Senior Member
Joined
Jan 31, 2018
Posts
197
Reaction score
431
Hii ngoma ya DRC bado mbichi. Na moja kati ya mambo yanayozorotesha maridhiano ni pande zinazotuhumiana kugoma kukutana. Wataalamu wa Conflict resolution & mediation wanasema ukiweza kuzikutanisha pande mbili zinazosigana, tayari umeshasolve mgogoro kwa 50%. Sasa shida kubwa ya mgogoro wa DRC ni kwamba wale Key Stakeholders wanakwepana. Kagame akihudhuria kikao cha maridhiano, Tshisekedi anakula chocho. Na Tshisekedi nae akihudhuria Kagame anaweweseka na kuyeyuka kiwendawazimu kama ndugu yangu @joramnkumbi. Sasa mgogoro utaishaje?

Tangu walipokutana Nairobi mwezi December 2022, hadi leo hawajakutana tena uso kwa uso. Wanatuhumiana lakini wanakwepana. Na hii inafanya mgogoro kuwa tete zaidi. Sasa leo ndo ilikua siku ya kuvunja fitna. Wengi walikua wanajiuliza je watakutana? Media kubwa duniani kama BBC, DW na Aljazeera zimesubiri kwa bashasha kuona kama mafahali hawa wawili watakutana leo jijini Dar Es Salaam. Kagame na Tshisekedi wote walidhibitisha kushiriki mkutano wa leo.

Lakini kama ilivyo destiri, Kagame katinga Dar, Tshisekedi katuma mwakilishi. Ikumbukwe Mkutano wa Nairobi ambao ulishindikana kufanyika, Tshisekedi alikua tayari kwenda lakini Kagame akasusa. Je nani atafanikiwa kuwakutanisha mafahali hawa uso kwa uso ili kuokoa damu zisiendelee kumwagika mashariki mwa Congo? Je kikao cha leo kinaweza kuleta matumaini yoyote ya amani bila uwepo wa Tshisekedi? Tukutane saa 1 tuendee na simulizi yetu kuhusu mgogoro wa DRC. Andaa popcorn, zisiungue sana.!
 
Naombea kagame aendelee kuiunga mkono M23 ili kuwalinda watu jamii ya kinyamlenge ndani ya congo japo kuwa viongozi wa congo wanadai hao banyamulenge siyo wakongo madai ambayo ni ya uongo.safi sana mzalendo kagame Kwa kulinda amani ya banyamulenge kutoka udhalimu wa tshisheked
 
Hii ngoma ya DRC bado mbichi. Na moja kati ya mambo yanayozorotesha maridhiano ni pande zinazotuhumiana kugoma kukutana. Wataalamu wa Conflict resolution & mediation wanasema ukiweza kuzikutanisha pande mbili zinazosigana, tayari umeshasolve mgogoro kwa 50%. Sasa shida kubwa ya mgogoro wa DRC ni kwamba wale Key Stakeholders wanakwepana. Kagame akihudhuria kikao cha maridhiano, Tshisekedi anakula chocho. Na Tshisekedi nae akihudhuria Kagame anaweweseka na kuyeyuka kiwendawazimu kama ndugu yangu @joramnkumbi. Sasa mgogoro utaishaje?

Tangu walipokutana Nairobi mwezi December 2022, hadi leo hawajakutana tena uso kwa uso. Wanatuhumiana lakini wanakwepana. Na hii inafanya mgogoro kuwa tete zaidi. Sasa leo ndo ilikua siku ya kuvunja fitna. Wengi walikua wanajiuliza je watakutana? Media kubwa duniani kama BBC, DW na Aljazeera zimesubiri kwa bashasha kuona kama mafahali hawa wawili watakutana leo jijini Dar Es Salaam. Kagame na Tshisekedi wote walidhibitisha kushiriki mkutano wa leo.

Lakini kama ilivyo destiri, Kagame katinga Dar, Tshisekedi katuma mwakilishi. Ikumbukwe Mkutano wa Nairobi ambao ulishindikana kufanyika, Tshisekedi alikua tayari kwenda lakini Kagame akasusa. Je nani atafanikiwa kuwakutanisha mafahali hawa uso kwa uso ili kuokoa damu zisiendelee kumwagika mashariki mwa Congo? Je kikao cha leo kinaweza kuleta matumaini yoyote ya amani bila uwepo wa Tshisekedi? Tukutane saa 1 tuendee na simulizi yetu kuhusu mgogoro wa DRC. Andaa popcorn, zisiungue sana.!
Kiafrika suluhu haijawahi fanywa mbele ya kina mama hasa pale wanaume wanapotofautiana
Kimsingi, Watu wote kabisa ambao wapo kwenye hiyo Kamati ya Usuluhishi wa Mgogoro huo wa huko Goma DRC hawana uhalali wowote ule wa kuweza kutatua Mgogoro huo. Kwa kifupi ni kwamba hakuna hata Mtu mmoja kwenye hiyo Timu ya Usuluhishi inayokutana huko Dsm Tanzania ambaye mwenye nguvu ya ushawishi ya kuweza kusitisha Mgogoro huo, they do not have a moral authority ya kuweza kutatua tatizo hili. Kila mmoja ambaye yupo kwenye Kamati hiyo nchini mwake ana makandokando yake ya kuwepo kwa migogoro sawa na hiyo iliyopo huko Goma na Bukavu, DRC.

Doctrine of equity states that "he who goes for equity must go with clean hands."

Kati ya hao Viongozi waliopo huko Dsm kwenye mkutano huo wa utatuzi wa Mgogoro huo, Je, nani ana mikono misafi?
 
Suluhu hapa mbona nyepesi.Mataifa yote yenye majeshi ya kulinda amani yaondoke Congo.Kama wakongo wanadai Kagame ndio kikwazo basi wakae nae meza moja wayajenge(wakiona hii option si sawa watwangane mshindi achukue kila kitu)

Huu ni upumbafu wenye unafiki ndani yake(unajiita taifa huru lakini kulinda mipaka yako bado ni changamoto?Uhuru wako sasa unamanisha nini?wakongo inabidi wajifunze hili katika namna ngumu).Hakuna mtu ateleta amani Congo bila wakongomani wenyewe kuamua kuwe na amani(ndio kuna influence kutoka capitalist nations(bado inaweza kuwa speculation) but nani alitoa huo mwanya?(Jibu ni jepesi,wakongomani ndio sababu,sasa kama ndio acha waonje chungu ya uzembe wao)
 
Back
Top Bottom