Ladslaus Modest
JF-Expert Member
- Jun 27, 2008
- 635
- 27
Shambulio la kufyatuliana risasi nyumbani kwa rais wa Guinea-Bissau kumesababisha mtu mmoja kuuawa na wengine wengi kujeruhiwa, sasa chache baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa.
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa uliopo nchini humo umethibitisha kuwa JRais Joao Bernardo Vieira hakudhuriwa katika shambulio hilo liliotokea usiku.
Shambulio hilo lilihusisha askari kufyatua risasi katika nyumba ya mkuu huyo wa nchi.
Umoja wa Afrika umetoa onyo dhidi ya jaribio lolote la kuchukua madaraka kwa nguvu katika nchi yenye historia ya kufanya mapinduzi katika siku za hivi karibuni.
Iliyokuwa chama tawala nchini humo kimeshinda nafasi za ubunge kwa kiasi kikubwa.
Mwandishi wa BBC wa masuala ya Afrika ya Magharibi, Will Ross alisema shambulio hilo linaonyesha kuwa ni jaribio lilioshindikana la kupindua serikali hiyo.
chanzo: BBCSwahili.com | Habari | Rais wa G-Bissau ashambuliwa nyumbani
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa uliopo nchini humo umethibitisha kuwa JRais Joao Bernardo Vieira hakudhuriwa katika shambulio hilo liliotokea usiku.
Shambulio hilo lilihusisha askari kufyatua risasi katika nyumba ya mkuu huyo wa nchi.
Umoja wa Afrika umetoa onyo dhidi ya jaribio lolote la kuchukua madaraka kwa nguvu katika nchi yenye historia ya kufanya mapinduzi katika siku za hivi karibuni.
Iliyokuwa chama tawala nchini humo kimeshinda nafasi za ubunge kwa kiasi kikubwa.
Mwandishi wa BBC wa masuala ya Afrika ya Magharibi, Will Ross alisema shambulio hilo linaonyesha kuwa ni jaribio lilioshindikana la kupindua serikali hiyo.
chanzo: BBCSwahili.com | Habari | Rais wa G-Bissau ashambuliwa nyumbani