Strong ladg
Senior Member
- Jul 15, 2021
- 170
- 445
Mnamo tarehe 1 Machi 2025, maafisa wa ECOWAS waliotumwa nchini Guinea Bissau kuzungumzia tarehe mpya ya uchaguzi walilazimika kuondoka nchini humo baada ya vitisho kutoka kwa Rais Umaro Sissoco Embalo.
Uchaguzi nchini Guinea Bissau ulipaswa kufanyika Novemba 2024 lakini Rais Embalo ametangaza kuwa uchaguzi utafanyika Novemba 2025. Wakati huohuo wapinzani wanadai utawala wa Rais Embalo ulipaswa kufikia kikomo mnamo mwishoni mwa mwezi Februari 2025 ingawa mahakama kuu imemruhusu akae madarakani hadi mwezi Septemba 2025.
Kutishiwa kwa maafisa wa ECOWAS kunazusha maswali kuhusu nguvu na ushawishi wa jumuiya hiyo ndani ya nchi wanachama huku ikiwa ni miezi miwili pekee imepita tangu Niger, Mali na Burkina Faso wakome rasmi kuwa wanachama wa ECOWAS.
Hadi sasa Rais Embalo hajazungumzia tukio hilo na ECOWAS haijatangaza hatua zitakazochukuliwa ili kurejesha demokrasia nchini Guinea Bissau. Jumuiya ya ECOWAS hutumia vikwazo au hata kupeleka wanajeshi ili kurejesha demokrasia ndani ya nchi mwanachama.
Uchaguzi nchini Guinea Bissau ulipaswa kufanyika Novemba 2024 lakini Rais Embalo ametangaza kuwa uchaguzi utafanyika Novemba 2025. Wakati huohuo wapinzani wanadai utawala wa Rais Embalo ulipaswa kufikia kikomo mnamo mwishoni mwa mwezi Februari 2025 ingawa mahakama kuu imemruhusu akae madarakani hadi mwezi Septemba 2025.
Kutishiwa kwa maafisa wa ECOWAS kunazusha maswali kuhusu nguvu na ushawishi wa jumuiya hiyo ndani ya nchi wanachama huku ikiwa ni miezi miwili pekee imepita tangu Niger, Mali na Burkina Faso wakome rasmi kuwa wanachama wa ECOWAS.
Hadi sasa Rais Embalo hajazungumzia tukio hilo na ECOWAS haijatangaza hatua zitakazochukuliwa ili kurejesha demokrasia nchini Guinea Bissau. Jumuiya ya ECOWAS hutumia vikwazo au hata kupeleka wanajeshi ili kurejesha demokrasia ndani ya nchi mwanachama.