Rais wa Mali aifananisha ECOWAS na kikundi cha kigaidi

Rais wa Mali aifananisha ECOWAS na kikundi cha kigaidi

Strong ladg

Senior Member
Joined
Jul 15, 2021
Posts
170
Reaction score
445
Rais wa Mali Jenerali Assimi Goita amesema jumuiya ya kiuchumi ya nchi za Afrika Magharibi ( ECOWAS) ni sawasawa na kikundi cha kigaidi.

Rais Goita alitoa kauli hiyo mnamo tarehe 6 Januari 2025 alipokuwa akiwahutubia viongozi wa kimila, kidini pamoja na wale wa asasi za kiraia.

Jenerali Assimi Goita alisema kuwa magaidi wanapokwenda kushambulia mji fulani huzuia watu kutoka na kuingia katika mji huo, vilevile huzuia uingiaji wa vyakula, maji pamoja na dawa.

Kutokana na kwamba nchi za ECOWAS zilifunga mipaka yake pamoja na kuweka vikwazo vilivyokwamisha uingiaji wa bidhaa muhimu kama chakula na dawa katika nchi za Niger pamoja na Mali mara baada ya nchi hizo kukumbwa na mapinduzi ya kijeshi, Rais Goita alisema kwamba ECOWAS walifanya vitendo vinavyofanywa na magaidi huku tofauti pekee ikiwa ni ECOWAS kutotumia silaha kama ambavyo magaidi hutumia.

Rais Goita alihoji iweje vyakula na dawa kwa ajili ya matibabu vizuiwe kuingia kwenye nchi fulani ilihali hata mateka wa vita hupewa chakula, maji na pia hutibiwa pale wanapougua.

Mali, Niger pamoja na Burkina Faso zilitangaza kujitoa kwenye jumuiya ya kiuchumi ya nchi za Afrika Magharibi ( ECOWAS) mwishoni mwa Januari 2024 mara baada ya kuunda umoja wao waliouita " Alliance of Sahel states"( AES kwa Kifaransa)na kulingana na kanuni za ECOWAS uanachama wao utakoma rasmi mwishoni mwa Januari 2025 ikiwa ni takribani mwaka mmoja tangu nchi hizo zitoe tangazo la kujitoa kwenye jumuiya hiyo.

Vilevile ,mwezi Disemba mwaka 2024, viongozi wa ECOWAS katika mkutano wao uliofanyika Abuja- Nigeria, walitoa taarifa ya kukubali kujitoa kwa nchi za AES kutoka kwenye jumuiya hiyo ingawa walitoa muda wa ziada wa miezi 6 kwa nchi hizo kukubaliwa kuendelea kuwa wanachama wa ECOWAS endapo watabadili mawazo.
Hata hivyo, nchi za Niger, Mali na Burkina Faso zilitoa taarifa ya pamoja ya kupinga muda huo wa ziada wa miezi 6 kwa madai kuwa viongozi wa ECOWAS wanataka kutumia muda huo "kuvuruga amani na usalama" kwenye nchi zao.

Source: YOUTUBE CHANNEL YA SHIRIKA LA HABARI LA MALI( ORTM).

Pichani: Jenerali Assimi Goita
 

Attachments

  • 1726688565173.jpg
    1726688565173.jpg
    186.2 KB · Views: 4
Kinachoshangaza ni kwamba nchi hizo za Burkina Faso, Mali na Niger ni miongoni mwa nchi zilizo maskini sana duniani na hata hao wanajeshi waliotwaa madaraka ktk nchi hizo hawana kabisa mpango wa kuziondoa nchi zao kwenye lindi la umaskini unaozikabili na hata Russia kamwe hawezi kuwasaidia ili waondokane na umaskini wao.
 
Kinachoshangaza ni kwamba nchi hizo za Burkina Faso, Mali na Niger ni miongoni mwa nchi zilizo maskini sana duniani na hata hao wanajeshi waliotwaa madaraka ktk nchi hizo hawana kabisa mpango wa kuziondoa nchi zao kwenye lindi la umaskini unaozikabili na hata Russia kamwe hawezi kuwasaidia ili waondokane na umaskini wao.
Na hutosikia kobaaz waki-comment chochote hapa similar to Sudan wanajifanya viziwi hawajui what's going there! Mnafiki ni zaidi ya shwaitwan.
 
Kinachoshangaza ni kwamba nchi hizo za Burkina Faso, Mali na Niger ni miongoni mwa nchi zilizo maskini sana duniani na hata hao wanajeshi waliotwaa madaraka ktk nchi hizo hawana kabisa mpango wa kuziondoa nchi zao kwenye lindi la umaskini unaozikabili na hata Russia kamwe hawezi kuwasaidia ili waondokane na umaskini wao.
mbona haoa Tanzania kuna umasikini pia tena wa kutisha? nenda huko vijijiki ,nenda kanda ya ziwa huko uoje umasikini ulivyo. nenda kanda ya kati kwa kina ndugai kule. Kwani na nyie mnaikumbatoa Urusi? By the way kwani Mataifa yanayo kumbatia Marekani ba Mataifa mengibe ya Ulaya ni Tajiri sana?

Ujinga ni mtaji wa CCM
 
Kinachoshangaza ni kwamba nchi hizo za Burkina Faso, Mali na Niger ni miongoni mwa nchi zilizo maskini sana duniani na hata hao wanajeshi waliotwaa madaraka ktk nchi hizo hawana kabisa mpango wa kuziondoa nchi zao kwenye lindi la umaskini unaozikabili na hata Russia kamwe hawezi kuwasaidia ili waondokane na umaskini wao.
Mali baada ya Mapinduzi wameongeza sana Export ya Pamba nje na Pia Dhahabu na wanaanza kue export yale madini ya kutengenezea Betri.

Nyie kilimo Cha Pamba kisha kufa wajinga nyie CCM.
 
Sentensi isomeke mtawala wa kijeshi wa mali na si rais wa mali. Aliingia madarakani kwa mapinduzi ya kijeshi bila kufanyika uchaguzi wa kidemokrasia kumpata rais
 
Wanapiga sana kazi, hawsshikiwi akilj kama nyie Tanzania mnao shikiwa akili na CCM,
 
Mali mwaka 2024 wamevuna tani 765,000 za pamba.

Tanzania tumevuna tani kama laki 3 na. hivi.
 
Mali baada ya Mapinduzi wameongeza sana Export ya Pamba nje na Pia Dhahabu na wanaanza kue export yale madini ya kutengenezea Betri.

Nyie kilimo Cha Pamba kisha kufa wajinga nyie CCM.
Wao wanazalisha korosho tani laki ngapi kwa mwaka?
 
Kinachoshangaza ni kwamba nchi hizo za Burkina Faso, Mali na Niger ni miongoni mwa nchi zilizo maskini sana duniani na hata hao wanajeshi waliotwaa madaraka ktk nchi hizo hawana kabisa mpango wa kuziondoa nchi zao kwenye lindi la umaskini unaozikabili na hata Russia kamwe hawezi kuwasaidia ili waondokane na umaskini wao.
Siku tawala za kiraia zikirudi madarakani kwenye hizo nchi huenda watarejea tena ndani ya ECOWAS.
 
Rais wa Mali Jenerali Assimi Goita amesema jumuiya ya kiuchumi ya nchi za Afrika Magharibi ( ECOWAS) ni sawasawa na kikundi cha kigaidi.

Rais Goita alitoa kauli hiyo mnamo tarehe 6 Januari 2025 alipokuwa akiwahutubia viongozi wa kimila, kidini pamoja na wale wa asasi za kiraia.

Jenerali Assimi Goita alisema kuwa magaidi wanapokwenda kushambulia mji fulani huzuia watu kutoka na kuingia katika mji huo, vilevile huzuia uingiaji wa vyakula, maji pamoja na dawa.

Kutokana na kwamba nchi za ECOWAS zilifunga mipaka yake pamoja na kuweka vikwazo vilivyokwamisha uingiaji wa bidhaa muhimu kama chakula na dawa katika nchi za Niger pamoja na Mali mara baada ya nchi hizo kukumbwa na mapinduzi ya kijeshi, Rais Goita alisema kwamba ECOWAS walifanya vitendo vinavyofanywa na magaidi huku tofauti pekee ikiwa ni ECOWAS kutotumia silaha kama ambavyo magaidi hutumia.

Rais Goita alihoji iweje vyakula na dawa kwa ajili ya matibabu vizuiwe kuingia kwenye nchi fulani ilihali hata mateka wa vita hupewa chakula, maji na pia hutibiwa pale wanapougua.

Mali, Niger pamoja na Burkina Faso zilitangaza kujitoa kwenye jumuiya ya kiuchumi ya nchi za Afrika Magharibi ( ECOWAS) mwishoni mwa Januari 2024 mara baada ya kuunda umoja wao waliouita " Alliance of Sahel states"( AES kwa Kifaransa)na kulingana na kanuni za ECOWAS uanachama wao utakoma rasmi mwishoni mwa Januari 2025 ikiwa ni takribani mwaka mmoja tangu nchi hizo zitoe tangazo la kujitoa kwenye jumuiya hiyo.

Vilevile ,mwezi Disemba mwaka 2024, viongozi wa ECOWAS katika mkutano wao uliofanyika Abuja- Nigeria, walitoa taarifa ya kukubali kujitoa kwa nchi za AES kutoka kwenye jumuiya hiyo ingawa walitoa muda wa ziada wa miezi 6 kwa nchi hizo kukubaliwa kuendelea kuwa wanachama wa ECOWAS endapo watabadili mawazo.
Hata hivyo, nchi za Niger, Mali na Burkina Faso zilitoa taarifa ya pamoja ya kupinga muda huo wa ziada wa miezi 6 kwa madai kuwa viongozi wa ECOWAS wanataka kutumia muda huo "kuvuruga amani na usalama" kwenye nchi zao.

Source: YOUTUBE CHANNEL YA SHIRIKA LA HABARI LA MALI( ORTM).

Pichani: Jenerali Assimi Goita
Hawa viongozi wa Mali, Niger na Burkina Faso ni washamba wa madaraka na Wana depict the true nature of African political hooligans.
 
Kinachoshangaza ni kwamba nchi hizo za Burkina Faso, Mali na Niger ni miongoni mwa nchi zilizo maskini sana duniani na hata hao wanajeshi waliotwaa madaraka ktk nchi hizo hawana kabisa mpango wa kuziondoa nchi zao kwenye lindi la umaskini unaozikabili na hata Russia kamwe hawezi kuwasaidia ili waondokane na umaskini wao.
Umetafiti historia ya upande mmoja tu; ni suala la muda tu, soon Senegal nayo itajitoa huko, let's wait and see.
 
Sentensi isomeke mtawala wa kijeshi wa mali na si rais wa mali. Aliingia madarakani kwa mapinduzi ya kijeshi bila kufanyika uchaguzi wa kidemokrasia kumpata rais
Mbona hata Tanzania ccm wanatawala kila siku bila kushinda kwenye uchaguzi halali hivyo tofauti tu ni kwamba wale wana magwanda na hawa hawana lkn approach wanayotumia wote kuingia madarakani ni ileile.
 
Back
Top Bottom