SI KWELI Rais wa Senegal amekataa picha yake kuwekwa ofisini

SI KWELI Rais wa Senegal amekataa picha yake kuwekwa ofisini

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Source #1
View Source #1
Source #2
View Source #2
SIKWELI.jpg
Rais wa Senegal, Bassirou Diomaye Faye amewataka Watumishi wa Umma kuacha kuweka picha yake kwenye ofisi zao akisema kuwa yeye sio Mungu anayetaka kusujudiwa badala yake amewataka watumishi hao kuweka picha za watoto wao maofisini mwao ili wawe wanazitazama pale wanapofanya maamuzi.
 
Tunachokijua
Kumekuwa na nukuu inayosambaa kwenye mitandao ikidaiwa Rais wa Senegal, Bassirou Faye amekataza watu kuweka picha yake maofisini mwao na badala yake waweke picha za familia zao. (Hapa na hapa)

“Sitaki mbandike picha zangu kwenye ofisi zenu kwa kuwa mimi siyo Mungu na wala siyo kielelezo cha utumishi isipokuwa ni mtumishi tu kwa Taifa badala yake bandikeni picha za watoto wenu ili muwe mnazitazama wakati wa kufanya maamuzi”

Ufuatiliaji wa JamiiCheck.com umebaini nukuu hiyo inayosambaa ni potoshi na haikuwahi kusemwa na Rais huyo kama inavyodaiwa.

Aidha, JamiiCheck imebaini kuwa nukuu hiyo anayohusishwa nayo Faye iliwahi kutolewa na Volodymyr Zelenskyy Rais wa Ukraine mwaka 2019, na iliwahi kuandikwa na mmojawapo wa watumiaji wa JamiiForums.

Endelea kutembelea Jukwaa la JamiiCheck ili uwe karibu na taarifa zilizohakikiwa.
hiv naona hata huko dunian naonaga kila mtu ofiscen ana picha za familia yake
 
Kauli zurisana , watumishi wachukue tahadhari wakati wanachukua rushwa wawe wanawatazama wanao ili kujiridhisha , ukifika muda wa kujitetea mahakamani msiaze kusema mpunguziwe adhabu mnawatoto wanawategemea
 
Tanzania:

Kituo Cha basi MAGUFULI, mji was serikali MAGUFULI, stendi ya SGR MAGUFULI, daraja la busisi MAGUFULI....uwanja was mpira Samia, kituo Cha sgr Samia......


KUNA VIONGOZI WANAPENDA SANA KUABUDIWA....
 
Huku kwetu visiwa vya Malta watu wanampigia magoti malkia kwa kumshukuru eti ametoa fedha za kujenga shule,zahanati na barabara wakati hizo fedha zimetolewa na wananchi wenyewe kupitia kodi na mikopo ambayo watailipa wananchi wenyewe pamoja na cha juu kinachopigwa na jamaa mmoja wakuitwa migulu baja akishirikiana mama yake maarufu kama sululu.
Ingewezekana tungemuomba huyo Rais wa huko aje huku kwetu aje kutoa semina elekezi.
 
Hello JC,

Nimeona baadhi ya media zinaripoti kuwa Rais wa Senegal kapiga marufuku picha yake kuning'inizwa maofisini. Aina kama hii ya viongozi tunawahitaji sana Afrika.
 
Back
Top Bottom