Rais wa Shirikisho la Soka Afrika Kusini (SAFA) Mbaroni kwa Kutumia Pesa za Shirikisho Kujinufaisha Binafsi

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Rais wa Shirikisho la soka la Afrika Kusini (SAFA) Danny Jordaan amekamatwa kufuatia madai ya kutumia pesa za Shirikisho hilo kujinufaisha binafsi, kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo.

Jordaan, ambaye alichukua jukumu kubwa katika kuandaa Kombe la Dunia la 2010 nchini Afrika Kusini, alijaribu kuzuia kukamatwa kwake siku ya Jumanne, lakini jana alikamatwa.

Kukamatwa huko kulifuatia uvamizi wa polisi katika ofisi za SAFA mwezi Machi, ambapo msemaji wa polisi Katlego Mogale alisema kuwa”kati ya 2014 na 2018, Rais wa SAFA alitumia rasilimali za shirika hilo kujinufaisha binafsi, ikiwa ni pamoja na kuajiri Kampuni binafsi ya ulinzi kwa ajili ya ulinzi binafsi na kampuni ya mahusiano ya umma , bila idhini kutoka kwa bodi ya ya SAFA.

Jordaan (73) na watuhumiwa wenzake, Mkurugenzi wa Fedha wa SAFA Gronie Hluyo na mfanyabiashara Trevor Neethling, wanatarajiwa kufikishwa Mahakamani.
 
Yani huyu jamaa mpaka leo bado ni Rais wa SAFA? Yaleyale ya king'ang'a kama Issa Ayatou Caf.
 
Sisi ndiyo Simba SC AKA;

1. Makolokolo SC.
2. Mbumbumbu SC.
3. Mipang'ang'a SC.
4. Malalamiko (Lialia) SC.
5. Makelele SC.
6. Madunduka SC.
7. Manyaunyau (mapaka) SC.
8. Mwakarobo SC.
9. Mikia SC.
10. Miso Misonda SC.
11. Manyang'au SC.
12. Mazumbukuku SC.
13. Mazombi SC.
14. Kinyume nyume SC.
15. Ngada SC.
16. Kolowizard SC
17. Zuwena SC.
18. Bebwabebwa (Mbeleko) SC.
19. Panya roads SC.
20. Kikanuni SC.
21. Kufa Kiume SC
22. Ubaya ubwege SC.
23. 5imba SC.
24. Visingizio SC (Visababu)
25. Manguruwe SC.
 
Huyo ni mla rushwa hatari!
 
Crap
 

Attachments

  • Screenshot_20240908-075933.jpg
    162.6 KB · Views: 4
Yani huyu jamaa mpaka leo bado ni Rais wa SAFA? Yaleyale ya king'ang'a kama Issa Ayatou Caf.
Miafrica mijinga tuu. Nakwambia soka la africa kusini ningeshikwa na makaburu leo sauz angesha shinda world cup
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…