Rais wa Sudan Kusini atangaza bunge jipya

Rais wa Sudan Kusini atangaza bunge jipya

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191

Chama cha Rais Kiir na Makamu wa Rais wa kwanza, Machar kwa pamoja vinawakilishwa kwenye bunge jipya


Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amefungua njia kwa wabunge wapya na kuunda bunge lililovunjwa siku ya Jumamosi.

Majina ya wabunge walioteuliwa yalitangazwa kwenye chombo cha habari cha taifa hilo, Shirika la Utangazaji la Sudani Kusini, Jumatatu usiku.

Bunge la sasa linahusisha wabunge kutoka kundi la waasi wa zamani, Sudan People’s Liberation Movement linaloongozwa na Makamu wa Rais wa kwanza Riek Machar na kutoka vyama vingine vya kisiasa.

Kwa mujibu wa makubaliano ya amani ya mwezi Septemba mwaka 2018, vyama mbalimbali vilitakiwa kuchagua wawakilishi wao ili waweze kuteuliwa na rais.

Bunge la Kitaifa la Mpito (TNLA), ambalo lilipanuliwa Jumatatu kutoka wabunge 400 hadi 550, lina wabunge 332 kutoka chama cha SPLM cha Rais Kiir na viti 128 kutoka SPLM-IO cha Bw Machar.

Huku vya ma vingine kama cha South Sudan’s Opposition Alliance (SSOA) viti 50, vyama vingine viti 30 na wafungwa wa zamani viti 10.
Kwa mujibu wa makubaliano hayo, 35% ya viti vinapaswa kwenda kwa wanawake.
 
Hii nchi sudani sijawahi ielewa,

Sudan Kaskazini Ni waarabu na wamestaarabika Sana

sudani kusini Ni pure blacks na Ni vurugu vurugu TU Kila kukicha.

Nini chanzo Cha migogoro yao, Ni Nini kilisababisha watengane Kaskazini na kusini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Walidangannywa kuwa hawa waarabu wanawanyonya jitengeni ili mjitawale nyie ni waafrika.Walivojitenga sasa wao wakaja na kampuni za mafuta wakajenga Plant kubwa,Waafrika wakapewa silaha ni kuuwana tu.
 
Back
Top Bottom