Chachu Ombara
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 6,067
- 10,938
“Maandamano ni haki ya kisheria kama mtu anataka kupiga kapige wale wabunge waliotunga sheria sio mlaji wa ile sheria kama unafikiri maandamano ni uhalifu yaharamishe kisheria jenga hoja yaharamishe kisheria tutofautishe ghasia na maandamano unajau kuna vitu viwili watu hawatofautishi ghasia na maandamano.
Maandamano ni njia bora tu ya kueleza lakini watu ambayo wanazungumza kuonyesha hisia kwa pamoja kwa kutumia miguu mikono na wale wasiokuwa na miguu wanatembea lakini nia yao ni wafike mahala kueleza hisia kwa pamoja kwa hiyo maandamano siyo uhalifu ndio maana kwenye sheria ya vyama vya siasa ni moja ya haki ya chama cha siasa kufanya maandamano na polisi hawaruhusiwi kujiingiza kwenye usimamizi wa shughuli za kisiasa.
Anayeweza kuwambia polisi hiki kiko juu na zaidi ni msajili, sijamsikia mimi msajili akizungumza kwa sababu msajili anajua hivi vyama ni vyake na anajua sheria hizi ni zake na anaweza akasema kwamba kwa mwenendo huu hii siyo dhumuni la kile kifungu.
Lakini vilevile inabidi uangalie sababu hawa CHADEMA wanalalamikia watu kupotea wanataka kuandamana kwa ajili watu wanapotea hii sio sababu kisheria?.Je ile kutafuta watu waliopotea au kuandamana kushinikiza watu waliopotea hatua zichukuliwe wapatikane au tujue wako wapi kazi haramu? siyo kazi haramu ni kazi halali ya kulinda uhai wa mtu ambayo ndiyo jukumu la msingi la kwetu.
Nguvu kubwa ilitakiwa itumike kuwatafuta kina Azory Gwanda akina Ben Saanane, akina Simon Kaguye akina Soka na wenzake na wengine wote sisi tulitoa majina ya zaidi ya watu 84 na imeongezeka saivi kule ndiyo tupeleke nguvu huwezi kupeleka nguvu kumdhibiti anayelia bila kutafuta chanzo kinachomsababisha aliye”
Jambo Tv
Pia soma
Maandamano ni njia bora tu ya kueleza lakini watu ambayo wanazungumza kuonyesha hisia kwa pamoja kwa kutumia miguu mikono na wale wasiokuwa na miguu wanatembea lakini nia yao ni wafike mahala kueleza hisia kwa pamoja kwa hiyo maandamano siyo uhalifu ndio maana kwenye sheria ya vyama vya siasa ni moja ya haki ya chama cha siasa kufanya maandamano na polisi hawaruhusiwi kujiingiza kwenye usimamizi wa shughuli za kisiasa.
Anayeweza kuwambia polisi hiki kiko juu na zaidi ni msajili, sijamsikia mimi msajili akizungumza kwa sababu msajili anajua hivi vyama ni vyake na anajua sheria hizi ni zake na anaweza akasema kwamba kwa mwenendo huu hii siyo dhumuni la kile kifungu.
Lakini vilevile inabidi uangalie sababu hawa CHADEMA wanalalamikia watu kupotea wanataka kuandamana kwa ajili watu wanapotea hii sio sababu kisheria?.Je ile kutafuta watu waliopotea au kuandamana kushinikiza watu waliopotea hatua zichukuliwe wapatikane au tujue wako wapi kazi haramu? siyo kazi haramu ni kazi halali ya kulinda uhai wa mtu ambayo ndiyo jukumu la msingi la kwetu.
Nguvu kubwa ilitakiwa itumike kuwatafuta kina Azory Gwanda akina Ben Saanane, akina Simon Kaguye akina Soka na wenzake na wengine wote sisi tulitoa majina ya zaidi ya watu 84 na imeongezeka saivi kule ndiyo tupeleke nguvu huwezi kupeleka nguvu kumdhibiti anayelia bila kutafuta chanzo kinachomsababisha aliye”
Jambo Tv
Pia soma