Rais wa TLS Mwabukusi aangalie na Ubora wa Sheria za Michezo kwani Nchi yetu ni kubwa lakini Olympic tumepitwa na Burundi

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Nimuombe tu Rais wa TLS mh Mwabukusi aangalie na Ubora wa Sheria za Michezo

Olympic tumetia aibu Mno

Mlale Unono πŸ˜€
 
Alafu na waziri mzimaaaaa wa michezo alienda eti!

Hii nchi ina undezi mwingi sana yaani. Gen Z wenyewe tunaowategemea watupiganie ndio kina Mwijaku na Steve Nyerere
 
Nimuombe tu Rais wa TLS mh Mwabukusi aangalie na Ubora wa Sheria za Michezo

Olympic tumetia aibu Mno

Mlale Unono πŸ˜€
Tena vzr umelileta hili..kutokuwa na uwakilishi unaolingana na umri wa nchi toka kupata uhuru, idadi na ukubwa wa nchi kwenye michezo mikubwa km Olympics ni kielelezo kuwa tuna taifa Mfu! na serikali yenye dhamana ya uongozi kwenye mambo yote yanayolipatia taifa sifa, kuheshimiwa, mapato, marafiki haijui ilifanyalo na haijui inakoelekea! Mpira wenyewe hakuna popote umelifikisha taifa! Mpira wa mdomoni..kila mtu ni mchambuzi na afisa habari wa kujitakia kwa timu anayopenda..Eti nchi tunapeleka waogeleaji Olympics..r we serious? tumeshindwa kujua potential yetu iko kwenye michezo gani..? Nchi km Botswana ina watu million 3 tu tunawazidi mara 20, wmefanya homework yao vzr wamejipata, leo wanashiriki Olympics na kushinda medali! Michezo siyo futbal peke yake, na watu wa dar es salaam wanapaswa wafahamu jambo hili! Miaka ya 70, 80 na 90 nchi hii ilikuwa bora sana kimataifa kwenye riadha na netball..sijui ni wapumbavu gani waliingia na kuhamisha attention kwenye netball na riadha ikaenda kwenye uigizaji na u-miss! It's terrible! Tumekuwa km taifa lote tuna asili ya Pwani..maneno meeengi..na ushabiki wa kijinga! Leo tunashindwa na Burundi..kweli?? Nini tumebaki nacho sasa..ignorance na usimba na uyanga..???nini taifa linapata?? nguvu nyingi kwenye mambo nonsense kabisa km simba au yanga day..na media yetu ndio inaua mambo mazuri na kupandikiza ujinga kwa wananchi..!
TUJIREKEBISHE!
 
nimesoma mistali miwili tu ,ila nakubaliana na ww
 
Mama anaupiga mwingi.

Maendeleo hayana chama
 
Tumwombe pia afuatilie na kuchunguza miradi ya serikali na utekelezaji wake.

Nadhani tumwike mifupa yote migumu iliyoshindikanika kwa wazalendo waliopita.
 
Alafu na waziri mzimaaaaa wa michezo alienda eti!

Hii nchi ina undezi mwingi sana yaani. Gen Z wenyewe tunaowategemea watupiganie ndio kina Mwijaku na Steve Nyerere
Yule waziri mtazame vizuri head morphology yake vizuri.
 
mbona hatupati medali jamanii

Mbio za marathon ni tarehe 10 August 2024 siku ya Jumamosi , karata ya mwisho kama nchi itakota kapa au kurudi na medali nyumbani Tanzania... mkimbiaji Gabriel Geay atakuwa mmojawapo anayewania medali ya Olympics katika marathon ... mwingine ni Alphonce Simbu wakati Magdalena Shauri na Jackline Sakilu ambao watakimbia mbio za wanawake . .

Toka maktaba:
Paris 2024 Olympics
olympics.com
Boston marathon 2024: Gabriel Geay on beating Eliud Kipchoge ...

11 Apr 2024 β€” Boston marathon 2024: Gabriel Geay on beating Eliud Kipchoge, his friendship with Kelvin Kiptum, and making history for Tanzania: "I am among...

Picha : mkimbiaji Gabriel Geay kutoka Tanzania
 
100m finalist from Botswana Letsile Tebogo..!
Halafu sisi tuko busy na yanga day..nani anaitangaza nchi yake kimataifa ni huyu kijana mmoja kuingia fainali za mita 100 kwenye Olympic au tukio la yanga day?
Halafu siku majini yakipanda tunaanza kuulizana kwa nini hatupati watalii wengi kuja Tanzania..tunatafuta mchawi wakati wachawi ni sisi wenyewe na viongozi wetu!
 

Attachments

  • Letsile Tebogo 100m heat - highlights - Olympics Athletics, Paris 2024.mp4
    6.7 MB
Hili kitu kinachoitwa soka Tanzania, kama hakitakemewa ni janga. Watu wanaamini mchezo pekee ni soka, viwanja vya michezo vyote vimebaki vya soka, hata hao viongozi wa michezo mwingine unakuta wanaojiita Mimi ni Simba Mimi YANGA. Tumezidiwa na Uganda na sudani ya kusini?
 
SIJASOMA ULICHOANDIKA, NIMESOMA HEADING TU, TATIZO KUBWA NI NEPOTISM, LIPO KWA NGAZI ZOTE ZA KIUTAWALA, WENYE SIFA HAWAPEWI NAFASI BALI WENYE USHAWISHI WENYE BABA ZAO, WENYE MAJINA YAO, WENYE UWEZO WAO.

HILI NI TATIZO KUBWA SANA TUNALO KAMA NCHI NA DUNIA WA UJUMLA, UKIWEZA KUMKANDAMIZA KWA NAMNA YOYOTE ILE YULE ASIEANACHO WEWE NI MSHINDI.
 
Nchi yenye zaidi ya watu million 60 inawakilishwa na muogeleaji mmoja..matokeo ni wa 8 kati ya 8 yaani wa mwisho! Lini sisi michezo km ya kuogelea ni fani yetu..tunaiga iga tu vitu tusivyoviweza!
 

Attachments

  • Screenshot_20240804_191115_Chrome.jpg
    639.1 KB · Views: 3
Nchi zenye serikali inayofahamu kufanya homework yake vzr..kijana Tebogo Letsilie wa Botswana ameshinda medali ya dhahabu mbio za mita 200 wanaume Olympic 2024, Paris France..halafu Tanzania ambayo inaizidi Botswana mara 20 kwa idadi ya watu tuko busy kubishana mambo ya uchaguzi tu na habari za watu kupotea!
Tanzania watu wengi elimu ni ya makaratasi tu, practical sifuri..hasa viongozi! Kwenye mambo yote mazuri yanayoleta sifa ya nchi sisi hatupo pamoja na uwepo wa potential hasa kwa riadha na netball..na leo maalum kabisa niwataje WANAWAKE Kama factor kubwa ya Taifa hili kuwa hapa lilipo kwa kuwa na ushabiki uliozidi mipaka kiasi cha kuididimiza nchi hii kwenye kila eneo! Safari ni ndefu..!
 

Attachments

  • Screenshot_20240808_222408_Chrome.jpg
    313.8 KB · Views: 2
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…