Rais wa Ufaransa agoma kuomba msamaha baada ya kuitusi NATO

Rais wa Ufaransa agoma kuomba msamaha baada ya kuitusi NATO

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
120e9e4ba81f87e0dc52e6286487a8bc


PARIS, UFARANSA

RAIS Emmanuel Macron wa Ufaransa amesema kuwa kauli yake kwamba Shirika la Kijeshi la Nchi za Magharibi (NATO) limepatwa na kifo cha ubongo ilipiga kengele ya hatari kwa nchi wanachama na kwamba hataomba radhi kwa kutoa matamshi hayo.

Matamshi hayo makali ya Rais Ufaransa yamepokewa kwa hisia kali na viongozi wenzake wa nchi za Ulaya wanaosisitiza kwamba, nchi za bara hilo zingali na haja ya kutegemea muungano huo wa kijeshi katika masuala ya ulinzi.

Hata hivyo Emmanuel Macron ambaye alikuwa akizungumza kandokando ya Katibu Mkuu wa NATO Jens Stoltenberg amesema hataomba samahani kwa matamshi yake ambayo amesema yalihitajika baada ya wanachama wa NATO kuelekeza mazingatio yao zaidi katika masuala ya bajeti ya shirika hilo badala ya masuala ya jiografia ya kisiasa.

Amesema aliuliza maswali ambayo hayakupatiwa majibu ambayo ni pamoja na kuhusu amani barani Ulaya, hali ya baada ya kuvunjika Makubaliano ya Silaha za Nyuklia za Masafa ya kati (INF), uhusiano na Russia na kadhia ya Uturuki na kuhoji ni nani adui?

Rais wa Ufaransa amesisitizia kuwa hataomba samahani kwa kusema kuwa Shirika la Kijeshi la Nchi za Magharibi NATO limepatwa na kifo cha ubongo.

Itakumbukwa kuwa mapema mwezi huu Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa alieleza wasiwasi wake kuhusiana na iwapo Marekani itaendeleza kutekeleza majukumu yake katika Shirika la Kijeshi la Nchi za Magharibi NATO na kusema kuwa, shirika hilo limekumbwa na kifo cha ubongo.

Macron alisema kwamba nchi wanachama wa Shirika la Kijeshi la Nchi za Magharibi NATO pamoja na nchi za Umoja wa Ulaya haziwezi kuendelea kuitegemea Marekani kwa ajili ya kujilinda.

Vilevile aliikosoa serikali ya Washington kwa kutokuwa na mawasiliano na wanachama wengine wa shirika hilo katika kuchukuliwa maamuzi ya kistratijia.

Chanzo: ParsToday
 
NATO inaelekea kufa,marekani wamechoka kutoa hell,wanataka kujitoa,uturuki hawaeleweki msimamo wao,ulaya nayo wanafikiria kuunda umoja wait was ulaya wa kujilinda na ndo kids huyo mfaransa kuiponda NATO
Hili nisuala la MUDA tu Ase Nakama UK Itafanikiwa Kutoka Katika EU Basi Kifo Cha NATO Kitakua Haraka Zaidi Ya Ifikiriwavyo
 
Inabidi urusi Pia ijiunge NATO.
Juhudi nzima za NATO ni kujilinda na Urusi!.

Lakini juhudi hizo kwa sasa hazina maana, Urusi ndio anawasupply EU Gesi sasa adui gani anayeweza risk biashara zake!?. Jibu linakuja USA muda wake EU umepitwa hakuna haja ya kumtegemea wakati yeye kakaa kistratajia zaidi sio kiuchumi!.

Uturuki kashashtuka sasa hivi anajiweka karibu na Urusi, UK ambaye ndio mchangiaji mkubwa wa EU/NATO naye anajitoa kwenye shirikisho. Ina maana kinachofuata ni either Ujerumani au Ufaransa ndio awe kaka mkubwa wa EU/NATO.

Kifo cha WARSAW kinainyemelea NATO!.
 
UK hajawahi kuku kaka wa EU, German ndo kiranja wa umoja huo na ndiye anayetoa pesa mingi ya Bajeti
Juhudi nzima za NATO ni kujilinda na Urusi!. Lakini juhudi hizo kwa sasa hazina maana, Urusi ndio anawasupply EU Gesi sasa adui gani anayeweza risk biashara zake!?. Jibu linakuja USA muda wake EU umepitwa hakuna haja ya kumtegemea wakati yeye kakaa kistratajia zaidi sio kiuchumi!.
Uturuki kashashtuka sasa hivi anajiweka karibu na Urusi, UK ambaye ndio mchangiaji mkubwa wa EU naye anajitoa kwenye shirikisho. Ina maana kinachofuata ni either Ujerumani au Ufaransa ndio awe kaka mkubwa wa EU/NATO.
Kifo cha WARSAW kinainyemelea NATO!.
 
Urusi anawameza taratibu nchi za EU, hazina pesa na biashara waliyokuwa wanafanya Mchina ameshawameza, walitegemea kunyonya sana Asia na America kusini
Simuoni akirudi tena alipo.

EU bila NATO wanakufa. Maana yake US ataanza iharibu EU ili ajiunge na nchi 1 1 na sio jumuiya
 
UK hajawahi kuku kaka wa EU, German ndo kiranja wa umoja huo na ndiye anayetoa pesa mingi ya Bajeti
UK anaongoza kwa kuchangia budget kubwa ya Ulinzi na Usalama akifuatiwa na Ufaransa. Ujerumani hana/hajawahi kuwa na bajeti kubwa kuwazidi hao wawili.

Sitegemei utaniuliza NATO bila UK itakuwaje iwapo Muingereza ndio mchangiaji mkubwa Ulaya nzima (NATO)!.
Kwa maana nyingine ile 40% iliyokuwa inachangiwa na UK itabidi France aibebe yote mwenyewe na huo ndio UKAKA wa UK kwenye NATO!.
 
Ufaransa na hususani Macron alikuja na Idea ya kutaka Umoja wa Ulaya uwe na Jeshi lake ama kwa kifupi EU Army.

Angela Merkel naye akaunga mkono 'juhudi' ingawa hivi karibuni Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani alimpa 'za uso' Macron na kuweka wazi kuwa bado NATO ni muhimili mkubwa wa ulinzi na usalama wa EU.

Tayari kuna mpango wa European Military Intervention Force ambayo itakuwa ikitekeleza majukumu yake ya kijeshi Duniani kote.

Wakati Macron anaendelea kushinikiza hilo, huko nchini Uingereza kuna 'mnyama' Brexit, ambayo itamuondoa Uingereza katika umoja huo.

Hivyo, inabaki Ufaransa sasa kama kinara katika masuala la kijeshi pia ikiwa na uchumi imara sambamba na Ujerumani. Hili la 'EU Army' litaifanya sasa Ufaransa kuwa na nguvu na ushawishi mkubwa sana hapo barani Ulaya na ndiyo jicho la Macron linapotazama.

Lakini hii mbinu ya ndugu Macron bado ni 'changa'. Anahitaji jitihada nyingine zaidi ili kuweza kuuondoa ushawishi wa NATO barani Ulaya kwa sasa.
 
Back
Top Bottom