Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Jacob Zuma amejisalimisha kwa Polisi ili kuanza kutumikia kifungo cha miezi 15 jela

Mdogo mdogo tutafika Kuna siku kaburi la jamaa fulani litafukuliwa mifupa ifungwe pingu
 
Ni Zuma huyo,
Kwa hiyo analazimishwa kulala na kuamka.
Askari magereza hawampigii salute tena.

Ama kweli dunia duara,ikitokea hapa Tz nadhani hata idadi ya watia nia itapungua
Urais utakuwa wakuogopa
 
Kwahiyo unataka kumaanisha kujisalimisha kwake hakuna maana yoyote? Bali ni sawa na kwenda kituo cha polisi kumpelekea mtu wako chai?
 
Kwahiyo unataka kumaanisha kujisalimisha kwake hakuna maana yoyote? Bali ni sawa na kwenda kituo cha polisi kumpelekea mtu wako chai?
Sasa hivi nyupo ndani na anajuta kujisalimisha. Point ni kwamba angegoma kujisalimisha police wasingeweza kumkamata kwa nguvu la sivyo wangeua watu wengi sana kitu ambacho hawakukitaka. So Zuma kujisalimisha aliamini kwamba atatoka baada ya maombi yake ya kupinga hukumu ya kumfunga kutenguliwa. Sasa mahakama imetupilia mbali maombi yake na hana ujanja zaidi maana supporters wake sidhani kama wanauwezo wa kwenda kumtoa gerezani kwa nguvu. Kwa nyongeza ni kwamba Zuma aliombwa ajisalimishe ili aonekane anaiheshimu katiba maana kama angekataa kujisalimisha angeweka historia mbaya sana kwenye utawala wa sheria wa South Africa, so kwa muktadha huo aliamini akijisalimisha ataonekana ni muungwana, na pia atatoka jela baada ya maombi yake kusikilizwa. Sasa hivi yupo ndani na maombi yake yametupiliwa mbali na hana nguvu tena ya kutoka, laiti angeota kuwa maombi yake yatatupiliwa mbali asingejisalimisha na polisi wasingemfanya chochote maana supporters wake walikuwa wanasafiri kutoka majimbo mbalimbali ya SA kwenda kuhakikisha hakamatwi, na siku moja kabla ya muda wa kujisalimisha haujaisha Nkandla ambako ndiko nyumbani kwakwe kulikuwa kumezingirwa na supporters wake wenye mapanga na mikuki huku wakiimba nyimbo za kuhamasishana kumlinda Zuma. So unaweza kuona kwa jinsi gani damu ingemwagika kama nguvu ingetumika kumkamata.
 
Ungeliweka huo ushahidi ili sisi wenyewe tujisomee,bila hivyo nitafananisha hizi hadithi zako kama Ngonjera na Ngano za Vikongwe.
 
Kwa ufupi tu, hiyo ni intelijensia ya polisi ilifanya kazi vilivyo wala kwenda polisi hayakuwa matakwa yake, alishawishiwa kwa kudanganywa mpaka akakubali na hiyo ni kawaida ya polisi inapotaka kukama raia na wakagundua maali ulipo wakikukamata hovyo watazua vurugu.
 
Ungeliweka huo ushahidi ili sisi wenyewe tujisomee,bila hivyo nitafananisha hizi hadithi zako kama Ngonjera na Ngano za Vikongwe.
Unataka ushahidi gani? Huwa unafuatilia siasa za South africa wewe?
 
Kabisa mkuu! Walimwamnisha hatakaa ndani zaidi ya siku ya kusomwa rufaa yake. Ameingia kwenye kumi na nane zao wakapiga bao hapo hapo.
 
Ila waafrika haya mambo ya demokrasia yanatuchanganya sana. Nakona yule mzee wa America aliyetoka angekuwa huko Sauzi kwa vile vibweka vyake angekuwa jela mda huu! Vitu vingine ni kujidhalilisha tuuu!
 
Hao watu wangepuliziwa gasi na kizimia kiulaini kabisa.
 
Unadhani katiba ya south afrika nikama yenu tz.poleyako
Usikute katiba yenyewe ilitungwa kipindi cha apartheid police na wazungu,coz Africa bado tunatumia sheria za wazungu.Hivyo basi lazima itambana mtu mweusi tu
 
Wapo watu walikua wanadanganyana kuwa eti Zuma watamlinda jana police imetoa Tangazo siku ikiisha bila kujisalimisha atakamtwa kwa nguvu wahuni wote wamerudi nyuma ambao walisema damu itamwagika Zuma hawawezi kukamatwa...

Lazima miongoni mwa waliokuwa wanadanganyana watakua akina johnthebaptist Kinuju Crimea jingalao @kigogoodi MsemajiUkweli na ng’ombe wengine wa kandarasi legacy
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…