Rais William Ruto atashinda muhula wa pili 2027 kirahisi sana, ikiwa atafanikisha ajira ya Raila African Union (AU)

Tlaatlaah

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2023
Posts
24,665
Reaction score
25,388
hii ni kutokana na namna alivyofanikiwa kushughulikia na kuzima hasira za vijana wa gen z na kuwanyakua baadhi waandamizi machachari wa Raila Odinga na kuwapa kazi ndani ya serikali yake ya muungano wa Kenya Kwanza, huku nje akiwaacha viongozi wa upinzani ambao ni dhaifu, wepesi na wasio na nguvu, ufuasi au ushawishi mkubwa...

Mathalani, Kalonzo Musyoka, Eugene Wamalwa, Jorge Wajackoyah, Matha Karua, Mwangi wa Iria Jimmy Wanjigi, Gideon Moi n.k ambao kwakweli hawana ufuasi au ushawishi kabisaa nje ya maeneo yao.

Hiyo itakua fursa nyingine ya Rais Dr William Ruto kushinda uchaguzi huo kirahisi sana2027, kwasabb vijana wa gen z, hivi sasa maelfu kwa mamilioni yao, wameanza kumuelewa tena Ruto, na sasa ndio wanajaza mikutano yake maeneo mbalimbali anayodhuru nchini Kenya...

Unadhani ni kiongozi gani wa upinzani mwenye nguvu na ushawishi, anaweza kumpa changamoto kwenye nafasi ya Urais wa Kenya 2027?πŸ’
 
Haituhusu wapambane na maisha yao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…