Raisi Putin atoa kauli kuhusiana na kifo cha Prigozhin na atoa salamu za rambirambi

Raisi Putin atoa kauli kuhusiana na kifo cha Prigozhin na atoa salamu za rambirambi

Richard

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2006
Posts
15,692
Reaction score
23,038
Raisi wa Urusi Vladimir Putin jioni ya jana ametoa salamu za pole kwa familia ya Yevgevy Prigozhin ambae alifariki katika ajali ya ndege ndogo binafsi akiwa na abiria wengine 9.

Raisi Putin amesema alimfahamu Prigozhin kwa tangu miaka ya 90 na kwamba kiongozi huyo wa Kundi la askari wa kukodi la Wagner alikuwa ni mtu mwenye historia yenye utata.

Putin aliendelea kumuelezea Prigozhin kwamba ni mfanyabiashara mwenye kipaji ambae alipata mafanikio binafsi na kwamba alikuwa na maslahi barani Afrika.

Raisi huyo wa Urusi akasema kwamba ni kutokana na mafanikio hayo ya Prigozhin akamuomab asaidie harakati za kuipigania Urusi na kwamba jana Prigozhin alikuwa Moscow kuzungumza baadhi ya watu kabla ya tukio hilo la kuanguka kwa ndege.

Hata hivyo Putin amesema Prigozhin amefanya makosa makubwa maishani mwake.

Na huo ukawa mwisho wa mahojiano ya Raisi Putin.

Msikilize Raisi Vladimir Putin.

 
wahuni hao walisema Wagner anakwenda Moscow akaishia Belarus kwa kuwa training majeshi ya huko.
Juzi alitoa video akiwa Afrika jana wanasema amekufa, mimi naona jamaa amehamia Africa rasmi kwa kufanya mapinduzi zaidi.

Kwanini nikasema hivyo kwasababu USA na Europe utajiri wao mkubwa unatoka barani Africa. Russia ameangushwa kiuchumi kwa saction sasa na yeye analipiza kwa mapinduzi.
 
wahuni hao walisema Wagner anakwenda Moscow akaishia Belarus kwa kuwa training majeshi ya huko.
Juzi alitoa video akiwa Afrika jana wanasema amekufa, mimi naona jamaa amehamia Africa rasmi kwa kufanya mapinduzi zaidi.

Kwanini nikasema hivyo kwasababu USA na Europe utajiri wao mkubwa unatoka barani Africa. Russia ameangushwa kiuchumi kwa saction sasa na yeye analipiza kwa mapinduzi.
Nimeeleza humu kwamba Wagner imepokonywa kutoka mikono ya Prigozhin na wenzake ili iwe chini ya command ya GRU kupitia wizara ya Ulinzi na jeshi la Russia.

Prigozhin hakuwa tayari kuona hiyo kitu yafanywa na hapo ndipo mfarakano ulipokuwa.

Pia nilieleza huko nyuma zaidi kwamba Putin ataka Wagner iwe ndani ya jeshi rasmi na iwe na kinga ya kisheria ambayo haukuwa nayo ilipokuwa kule Donbas kwenye vita ya Crimea 2008 -2014.

Ilipofika mwisho wa mwezi ulopita wa Julai wale wanajeshi wa Wagner walotaka kuendelea kuwa chini ya Wagner mpya chini ya uongozi wa GRU walirasimishwa na sasa wafuata maagizo ya Shoigu na Gerasimov.

Kwanza kabla ya kwenda kwa Putin Prigozhin ataanzaje kutaka kuwashinda hao mazee wawili ambao ni watu wazito kijeshi nchini Russia?
 
Hata kama ningekuwa mimi. Huyu ndg alifanya kosa kubwa sana. Kama leo ameteka ngome za jeshi, na anashangiliwa na raia kila anapokwenda, unadhani nini kingetokea baadae. Kafa kijinga huyu, bora angekufa vitani akitaka kumpindua shetani.
 
Raisi wa Urusi Vladimir Putin jioni ya jana ametoa salamu za pole kwa familia ya Yevgevy Prigozhin ambae alifariki katika ajali ya ndege ndogo binafsi akiwa na abiria wengine 9.

Raisi Putin amesema alimfahamu Prigozhin kwa tangu miaka ya 90 na kwamba kiongozi huyo wa Kundi la askari wa kukodi la Wagner alikuwa ni mtu mwenye historia yenye utata.

Putin aliendelea kumuelezea Prigozhin kwamba ni mfanyabiashara mwenye kipaji ambae alipata mafanikio binafsi na kwamba alikuwa na maslahi barani Afrika.

Raisi huyo wa Urusi akasema kwamba ni kutokana na mafanikio hayo ya Prigozhin akamuomab asaidie harakati za kuipigania Urusi na kwamba jana Prigozhin alikuwa Moscow kuzungumza baadhi ya watu kabla ya tukio hilo la kuanguka kwa ndege.

Hata hivyo Putin amesema Prigozhin amefanya makosa makubwa maishani mwake.

Na huo ukawa mwisho wa mahojiano ya Raisi Putin.

Msikilize Raisi Vladimir Putin.


Huyo Putin nimempenda.

Kaweka pembeni unafiki, kausemea ukweli.

Hapa Afrika na baadhi ya viongozi duniani, mtu hata ni mbaya wake akifa hujifanya kumsifia marehemu kwa maneno mengi ya uongo na unafiki wa kutosha.

Mtu anakuroga, halafu eti anahudhuria na mazishi kabisa huku akimwaga machozi kuzuga kinafiki!

Hapo Putini kwa hotuba hiyo kajidhihirisha kwamba mhusika wa kifo hicho ni yeyebila kuuma uma maneno.
 
Back
Top Bottom