Rajabu ya $29 yataifishwa

BRAVER

Senior Member
Joined
Jun 23, 2015
Posts
105
Reaction score
95
Shamanic ya $29 yataifishwa


[http

Waziri wa Fedha Dakta Philip Mpango leo amekagua shehene ya Alimasi iliyokamatwa uwanja wa ndege wa Dar es salaam iliyofanyiwa makadirio hafifu ikiwa ni nusu ya makadirio halisi iliyokuwa isafirishwe kwenda nje ya nchi.

Waziri wa fedha Dkt Philip Mpango ameambiwa Almasi ya thamani ya dola za Marekani milioni 29 ilithaminishwa kwa dola milioni 19

Aidha kiwango cha almasi kilichothamishwa na wamiliki mgodi wa Mwadui ni chini ya kiwango ambapo baada ya waziri kupewa taarifa na maafisa wa TRA juu ya sheria ya mali inayokamatwa kwa udanganyifu inatakiwa kutaifishwa na serikali ndipo waziri Mpango aliamuru Almasi hiyo kutaifishwa.

Waziri Mpango ambaye aliongozana na maafisa waandamizi wa serikali ikiwa ni pamoja na Mkurugenzi wa Mashitaka Biswalo Mganga, Msajili wa Hazina Dk. Oswald Mashindano, Kamishna wa Kanda maalumu ya Dar es salam Lazaro Mambosasa, Naibu Mkurugenzi wa Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU Brigedia Generali John Julius Mbungo na maafisa wa Mamlaka ya kodi ya Mapato TRA

$29,000,000=TZS.64,887,231,303. Hii ni kwa mwaka mmoja. Je, tangu mgodi uanze nimepata ngapi?.Karibuni


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi naona kma ilikuwa mchezo vile..!!! Maswali yng machache.

1. Ilipokamatwa, walijuaje kama ilithaminishwa pungufu wakati ilikuwa imefungwa..??

2. Je, wakati wanaikamata pale airport, ni nani pale airport aliyegundua thamani halali ya hyo almasi na kuamuru ikamatwe wakati ilikuwa imefungwa.

3. Mmiliki wa mali alikuwa wapi wakati leo mali yake ilikuwa inataifishwa.

4. Walipata wapi muda wa kuandaa WATU WOTE WALE, wkt serikali ipo bize muda wote..??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jibu ni jepesi sana....FIX

Send via Quan dong fen from north Korea
 
Yaani serikali ikosee yenyewe kukukadiria, inakukamata kwa kosa ililolifanya yenyewe kisha inakutaifisha mali yako!

Nawahakikishieni ujinga huu utasababisha tuzione Bomber F-35 in action.

Zitakujaje na zitatoka wapi subiri muujiza wako.
 
Yaani serikali ikosee yenyewe kukukadiria, inakukamata kwa kosa ililolifanya yenyewe kisha inakutaifisha mali yako!

Nawahakikishieni ujinga huu utasababisha tuzione Bomber F-35 in action.

Zitakujaje na zitatoka wapi subiri muujiza wako.
Hahahahahahaha.

Thanx kwa kuniongezea maswali mkuu.

Hilo linakuwa swali langu la 5 kwamba:

5. Wakadiriaji NI WAO WENYEWE. Kama wao wenyewe walikosea kukadiria, whose fault..???

Swali la jingine.

6. Ni nini CHANZO cha wao kukosea kukadiria..?? Je ni rushwa au kukosa umakini..?? Kma ni rushwa wote tunatakiwa kuwa responsible na kama ni kukosa umakini wao ndo wapo responsible.






Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chezo la kuigiza hilo......tunajitekenya na kucheka wenyewe......hujiulizi kwa nn ikamatwe siku tatu kabla ya report ya Tanzanite na Almasi kutoka?

Sent from my Compaq desktop-1997 Using Jamiiforums desktop app
 
Wasiwasi wangu tunafanya haya mambo kwa pamoja kwa wakati kwa mtindo mmoja wakati tulikosea kwa mtindo mmoja, hivyo tukikosea tu itakula kwetu kwa mtindo mmoja. Kilio kitakuwa kikubwa sana. Mungu tusaidie.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…