Ramadhani Kingai, sasa urudi Moshi CCP, urudie somo la PGO

Ramadhani Kingai, sasa urudi Moshi CCP, urudie somo la PGO

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
16,419
Reaction score
26,594
1658389510702.png


Ramadhani Kingai sasa ndio DCI wetu!

Kama alipitia somo la GPO(General Police Orders) kule Moshi CCP(Chuo Cha Polisi) , basi ni wazi kuwa hakufaulu lakini akaingia kazini hivyo hivyo.

Nasema hivi kutokana na track record yake , hasa katika kesi iliyomuumbua kitaaluma, kesi ya Ugaidi wa Mbowe.

Tuna mshukuru Mama Samia kuwa kesi ile iliwapa waandishi wa habari uhuru unaohitajika.

Na katika uhuru ule waandishi wa habari waliweza kubaini na kuandika mapungufu makubwa kitaaluma yana yo mkabili ndugu yetu Ramadhani Kingai.

Pengine kuna sababu nyingine nje ya hizi tunazo ziona zilizo sababisha Ramadhani Kingai kupandishwa madaraka na kuwa DCI.

Nchi ii huwezi jua.

Sasa kwa mapungufu yale tuliyoyaona yanaweza kuambukiza jeshi zima la Polisi na likawa watu wanaofanya kazi bila weledi wala taaluma.

Idara ya DCI ambayo ndiyo inafanya criminal investigations zote nchini lazima iwe na weledi wa kitaaluma.

Kwa kuanzia namshauri DCI mpya asome masomo ya ziada ya GPO.
 
Mh GPO ?
Tunapanga safu mheeshimiwa mengine baadae ndugu yangu so unajua mtihani ni 2025 sio mbali saaana ni karibu tu Ni Nani Alie mkali zaidi kuruka na paper? Hahahaha mengine baadae saaana.j
 
Nadhani tuna tatizo kubwa katika kanuni na mifumo yetu.
Kingai HAFAI kuwamo kuendelea kuwamo kwenye uongozi wa juu wa jeshi la polisi.
Anatakiwa kushushwa cheo halafu ndio akasome upya. Raisi amekosea, arekebishe kwa faida ya taifa hili.
 
Hii nchi Kila mtu mjuaji, ona sasa ulivyodhalilika kwa hiki kituko (GPO) ulichoandika instead of (PGO). Wakati mwingine tusiige mkumbo wa maneno ya mtaani badala yake jikite kwenye kile unachokifahamu hata ukiandika uwe na confidence kwa content unayoiwasilisha.
 
Hii nchi Kila mtu mjuaji, ona sasa ulivyodhalilika kwa hiki kituko (GPO) ulichoandika instead of (PGO). Wakati mwingine tusiige mkumbo wa maneno ya mtaani badala yake jikite kwenye kile unachokifahamu hata ukiandika uwe na confidence kwa content unayoiwasilisha.
Lakini si umeelewa?
Kwani ukiisoma backwards maana yake inabadilika?
Jiongeze kukariri si kuzuri.
 
Ulichoandika hata hukijui alafu unataka kutoa maoni
GPO ni nn? Huoni kama.unajichoresha? Imenichukua muda sana kugundua humu JF kuna vilaza wengi sana alafu ndio mabingwa wa kuanzisha nyuzj
 
Hii nchi Kila mtu mjuaji, ona sasa ulivyodhalilika kwa hiki kituko (GPO) ulichoandika instead of (PGO). Wakati mwingine tusiige mkumbo wa maneno ya mtaani badala yake jikite kwenye kile unachokifahamu hata ukiandika uwe na confidence kwa contet unayoiwasilisha.
Labda alitaka kuandika GPA.
 
Back
Top Bottom