Rangi Tatu za Mbagala ni zipi?

Chanazi

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2010
Posts
212
Reaction score
64
Nasikia sikia tu, Mbagala Rangi Tatu ila najiuliza hizo rangi tatu ni zipi? Naomba kufahamishwa.
 
Sikuona sababu ya kuidharau thread hii nikajaribu kupata maelezo ya nini hasa asili ya jina hili nilifika Mbagala Rangi Tatu nikamuona Mzee mmoja nikajifanya ni mwenyeji wa eneo lile ili asije akaniona kwanini namuuliza kuhusu Mbagala ili hali natoka mbali sana, nikamuuliza hivi rangi tatu hapa Mbagala zilikuwa wapi???

Aliniambia kuwa usidhani rangi hizo zilikuwa zimepakwa kwenye kuta la hasha. Akaanza kunipa jibu.
Eneo hili lilikaliwa na Wamakonde, kama unavyojua wamakonde wanautamaduni wa kujichanja nyuso zao. Kulikuwa na aina tatu zilizowatofautisha hawa wamakonde. Kuna Wamakonde ambao asili yao ni Mtwara uchanjaji wao wa chale ulitofautiana na wale ambao asili yao ni kutoka Msumbiji ambao nao walikuwa ni wa aina mbili tofauti. Kuna Wamakonde ambao asili yao ni Msumbiji na wale ambao Mreno alijaribu kuiga uchanjaji akaleta style ya aina yake tofauti kidogo na Wamakonde asilia wa Msumbiji. Kwa hiyo utakuta kutoka Msumbiji kulikuwa na Wamakonde aina mbili kwa chale zao na wale ambao asili yao ni Mtwara walipokuja hapa Mbagala wakawa ni kabila moja lenye matawi matatu, wakaita Mbagala Rangi Tatu.




 
asante sana mwana. Umewazidi wote ambao walitoa majibu ya mtaani! Mimi kwangu ni Mbagala, nashukuru and I am going to do a simple research on it. Asante sana. I wsill come back to you when I am through!
 
asante sana mwana. Umewazidi wote ambao walitoa majibu ya mtaani! Mimi kwangu ni Mbagala, nashukuru and I am going to do a simple research on it. Asante sana. I wsill come back to you when I am through!

tupe majibu ya utafiti wako Mkuu!
 
tupe majibu ya utafiti wako Mkuu!

No bado sijaufanya maana siishi Dar. Mpaka nije Dar niende mbagala! I have a small hurt at Mbagala Majimatitu. Pale nitawahoji wazee wa miaka mingi pale!
 
Aisee... Halafu kumbe Dar kuna Mtongani mbili. Sijui ilikuaje ikawa hivi
 
shukrani mzee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…