BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Mwandishi wa Vitabu na Mtabiri kutoka Nigeria, Ahunna Ejiogu Scarlet alitabiri kuhusu kifo cha Rapa AKA ambaye amefariki baada ya kupigwa Risasi jiji Durban saa chache akijandaa kusherekea Birthday yake.
Mtabiri huyo aliandika kupitia Twitter May 2, 2021 akisema “Mungu anasema: Msanii wa Rap kutoka Afrika Kusini, AKA anatakiwa kuchukua tahadhari juu ya kupigwa Risasi ambayo itachukua uhai wake. Anapaswa kuepuka marafiki wa Kimafia (Wahuni) na kujichanganya vinginevyo atakuwa mlengwa.
Hatimaye utabiri huo umetimia kama alivyoandika. Kiernan Forbes ameuawa kwenye siku yake ya kuzaliwa. RIP AKA.
Mbali na hilo, Ahunna aliwahi kutabiri kuhusu kifo cha mtoto wa Msanii wa Nigeria, Davido. Julai 13, 2021 aliandika, Mungu anasema: Mama Ifeanyo (Chef Chi) anatakiwa kumwangalia kwa ukaribu na maombi Ifeanyi kwasababu mmoja wa wazazi wenza wa Davido anapanga kumuua mtoto huyo kwa kupitia Ushirikina kwasababu atarithi mali nyingi ambazo baba yake anazo akiwa kama mtoto wa kwanza wa kiume.
Jambo hilo lilitimia kweli, mtoto wa David alifariki kwa kuzama kwenye Swimming Pool nyumbani kwa Davido na Ifeoma.