BWANKU M BWANKU
JF-Expert Member
- Jan 12, 2019
- 377
- 435
RAS GEITA NA DC CHATO WATEMBELEA BANDA LA CHATO
Na. Richard Bagolele-Nyamhongolo Mwanza
Katibu Tawala Mkoa wa Geita Prof.Godius Walter Kahyarara na Mkuu wa Wilaya ya Chato Martha Mkupasi kwa nyakati tofauti leo wametembelea banda la Halmashauri ya Wilaya ya Chato kwenye maonesho ya Nanenane 2022 Kanda ya Ziwa Magharibi yanayoendelea kwenye viwanja vya Nyamhongolo Mwanza.
Katibu Tawala Mkoa amevipongeza vikundi mbalimbali vilivyopeleka bidhaa za maonesho ambapo ameshauri vikundi hivyo kuzalisha bidhaa zenye ushindani katika masoko ya ndani na nje ya mkoa au nje ya nchi.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Chato amevishauri vikundi hivyo kuongeza ubunifu wa kuongeza mitaji ikiwemo ile ya sekta binafsi pasipo kutegemea pekee mikopo inayotolewa na serikali kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani.
Kauli mbiu ya Maonesho ya Nanenane 2022 ni "Ajenda 10/30: Kilimo ni Biashara, Shiriki Kuhesabiwa kwa Mipango Bora ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi".
Na. Richard Bagolele-Nyamhongolo Mwanza
Katibu Tawala Mkoa wa Geita Prof.Godius Walter Kahyarara na Mkuu wa Wilaya ya Chato Martha Mkupasi kwa nyakati tofauti leo wametembelea banda la Halmashauri ya Wilaya ya Chato kwenye maonesho ya Nanenane 2022 Kanda ya Ziwa Magharibi yanayoendelea kwenye viwanja vya Nyamhongolo Mwanza.
Katibu Tawala Mkoa amevipongeza vikundi mbalimbali vilivyopeleka bidhaa za maonesho ambapo ameshauri vikundi hivyo kuzalisha bidhaa zenye ushindani katika masoko ya ndani na nje ya mkoa au nje ya nchi.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Chato amevishauri vikundi hivyo kuongeza ubunifu wa kuongeza mitaji ikiwemo ile ya sekta binafsi pasipo kutegemea pekee mikopo inayotolewa na serikali kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani.
Kauli mbiu ya Maonesho ya Nanenane 2022 ni "Ajenda 10/30: Kilimo ni Biashara, Shiriki Kuhesabiwa kwa Mipango Bora ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi".