Rashid Ali Meli alitoa fedha za serikali kwa siri kufanikisha safari ya Nyerere UNO 1955

Rashid Ali Meli alitoa fedha za serikali kwa siri kufanikisha safari ya Nyerere UNO 1955

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
NATAFUTA NA NATAFITI HISTORIA YA RASHID ALI MELI NA SAFARI YA NYERERE UNO 1955

Tafadhali nitafutie watoto au ndugu wa Rashid Ali Meli hapo Zanzibar.

Kijana wa Kingazija.

Aliishi Dar katika 1950s akifanya kazi Dar es Salaam Municipal Council kama Bwana Fedha.

Ana kisa cha kusisimua sana kati yake yeye, Iddi Faiz Mafungo Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) na TANU na Ali Mwinyi Tambwe katibu wa jumuiya hiyo katika historia ya TANU na safari ya kwanza ya Julius Kambarage Nyerere UNO February 1955.

Akiishi Mtaa wa Tandamti nyumba yake ikiangalia Soko la Kariakoo.

Alikuwa mume wa Bi. Bihuri.

Kwa miaka mingi nimekuwa nikitafuta habari zake na picha yake bila mafanikio.

Rashid Ali Meli ni kati ya watu wasiozidi 20 waliohudhuria mkutano wa kwanza wa TANU Arnautoglou Hall mwezi August 1954.

Miongoni wa waliohudhuria mkutano ule walikuwa: Julius Nyerere, Abdulwahid na Ally Sykes, Dossa Aziz, John Rupia, Mshume Kiyate, Makisi Mbwana, Jumbe Tambaza, Juma Waziri, Clement Mtamila, Rajabu Diwani, Schneider Plantan, Marsha Bilali, Rashid Ali Meli, Frederick Njiliwa, Iddi Faiz Mafongo, Iddi Tulio, Denis Phombeah na wengineo.
 
Uongo waliotoa fedha Nyerere kwenda umoja wa mataifa ni familia ya Rupia na Baba yake Freeman Mbowe MATAJIRI WA KIAFRIKA MIAKA hiyo hao Waislamu wengi walikuwa choka mbaya maskini wa kutupwa.
 
Umezidi na habari za upande mmoja, sasa tuletee habari za akina Clement, Frederick na Denis.
 
Uongo waliotoa fedha Nyerere kwenda umoja wa mataifa ni familia ya Rupia na Baba yake Freeman Mbowe MATAJIRI WA KIAFRIKA MIAKA hiyo hao Waislamu wengi walikuwa choka mbaya maskini wa kutupwa.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] mkuu una uhakika?

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
 
Mzee Mohamed hebu fafanua. Nani alitoa pesa, Rupia au Meli? Nini kilijiri?
Huyu Rashid Ali Meli alikuwa mmoja kati watu takriban hawazidi 20 waliohudhuria mkutano wa kwanza wa TANU Ukumbi wa Arnautoglo.

Rashid Ali Meli alikuwa mweka fedha Dar es Salaam Municipal Council.

Ilipodhihirika kuwa mfuko wa kumpeleka Nyerere New York UNO una matatizo yeye akaenda kwenye sefu yake kazini akafungua akatoa
fedha kwa siri akamkabidhi Iddi Faiz atie katika safari ya Nyerere kwa makubaliano kuwa TANU itarejesha hizo fedha haraka.

Siku ya pili baada ya Rashid Ali Meli kutoa fedha zile na kuzipeleka TANU wakaguzi wakafika ofisini kwake kufanya ukaguzi.

Walijuaje?

Waingereza walikuwa na mtu wao katika uongozi wa juu wa TANU pale New Street akiwapa taarifa zote kila zinapotokea.

Huyu mtu wao alikuwa huyu mzee wangu.

Yako mengi sana katika historia ya TANU ya hawa, ''nyoka wa vichwa viwili.'
 
Huyu Rashid Ali Meli alikuwa mmoja kati watu takriban hawazidi 20 waliohudhuria mkutano wa kwanza wa TANU Ukumbi wa Arnautoglo.

Rashid Ali Meli alikuwa mweka fedha Dar es Salaam Municipal Council.

Ilipodhihirika kuwa mfuko wa kumpeleka Nyerere New York UNO una matatizo yeye akaenda kwenye sefu yake kazini akafungua akatoa
fedha kwa siri akamkabidhi Iddi Faiz atie katika safari ya Nyerere kwa makubaliano kuwa TANU itarejesha hizo fedha haraka.

Siku ya pili baada ya Rashid Ali Meli kutoa fedha zile na kuzipeleka TANU wakaguzi wakafika ofisini kwake kufanya ukaguzi.

Walijuaje?

Waingereza walikuwa na mtu wao katika uongozi wa juu wa TANU pale New Street akiwapa taarifa zote kila zinapotokea.

Huyu mtu wao alikuwa huyu mzee wangu.

Yako mengi sana katika historia ya TANU ya hawa, ''nyoka wa vichwa viwili.'
Aisee
 
Huyu Rashid Ali Meli alikuwa mmoja kati watu takriban hawazidi 20 waliohudhuria mkutano wa kwanza wa TANU Ukumbi wa Arnautoglo.

Rashid Ali Meli alikuwa mweka fedha Dar es Salaam Municipal Council.

Ilipodhihirika kuwa mfuko wa kumpeleka Nyerere New York UNO una matatizo yeye akaenda kwenye sefu yake kazini akafungua akatoa
fedha kwa siri akamkabidhi Iddi Faiz atie katika safari ya Nyerere kwa makubaliano kuwa TANU itarejesha hizo fedha haraka.

Siku ya pili baada ya Rashid Ali Meli kutoa fedha zile na kuzipeleka TANU wakaguzi wakafika ofisini kwake kufanya ukaguzi.

Walijuaje?

Waingereza walikuwa na mtu wao katika uongozi wa juu wa TANU pale New Street akiwapa taarifa zote kila zinapotokea.

Huyu mtu wao alikuwa huyu mzee wangu.

Yako mengi sana katika historia ya TANU ya hawa, ''nyoka wa vichwa viwili.'
Shukrani kwa ufafanuzi Mzee wangu.
 
Huyu Rashid Ali Meli alikuwa mmoja kati watu takriban hawazidi 20 waliohudhuria mkutano wa kwanza wa TANU Ukumbi wa Arnautoglo.

Rashid Ali Meli alikuwa mweka fedha Dar es Salaam Municipal Council.

Ilipodhihirika kuwa mfuko wa kumpeleka Nyerere New York UNO una matatizo yeye akaenda kwenye sefu yake kazini akafungua akatoa
fedha kwa siri akamkabidhi Iddi Faiz atie katika safari ya Nyerere kwa makubaliano kuwa TANU itarejesha hizo fedha haraka.

Siku ya pili baada ya Rashid Ali Meli kutoa fedha zile na kuzipeleka TANU wakaguzi wakafika ofisini kwake kufanya ukaguzi.

Walijuaje?

Waingereza walikuwa na mtu wao katika uongozi wa juu wa TANU pale New Street akiwapa taarifa zote kila zinapotokea.

Huyu mtu wao alikuwa huyu mzee wangu.

Yako mengi sana katika historia ya TANU ya hawa, ''nyoka wa vichwa viwili.'
special branch
 
Umezidi na habari za upande mmoja, sasa tuletee habari za akina Clement, Frederick na Denis.
Gunst,
Hivyo ninavyoandika ndivyo historia ilivyokuwa na ikiwa unafadhaika kwa kuwa unasoma majina ya Kiislamu hii ni bahati mbaya kwako.

Wako waliojaribu kukwepa historia ya kweli kwa sababu ya hofu kama yako kwa kuona majina mengi katika historia ya uhuru wa Tanganyika ni ya Kiislamu.

Hatuwezi kubadilisha historia.

Habari ni za upande mmoja chembelecho kwani hivyo ndivyo ilivyokuwa.
 
Huyu Rashid Ali Meli alikuwa mmoja kati watu takriban hawazidi 20 waliohudhuria mkutano wa kwanza wa TANU Ukumbi wa Arnautoglo.

Rashid Ali Meli alikuwa mweka fedha Dar es Salaam Municipal Council.

Ilipodhihirika kuwa mfuko wa kumpeleka Nyerere New York UNO una matatizo yeye akaenda kwenye sefu yake kazini akafungua akatoa
fedha kwa siri akamkabidhi Iddi Faiz atie katika safari ya Nyerere kwa makubaliano kuwa TANU itarejesha hizo fedha haraka.

Siku ya pili baada ya Rashid Ali Meli kutoa fedha zile na kuzipeleka TANU wakaguzi wakafika ofisini kwake kufanya ukaguzi.

Walijuaje?

Waingereza walikuwa na mtu wao katika uongozi wa juu wa TANU pale New Street akiwapa taarifa zote kila zinapotokea.

Huyu mtu wao alikuwa huyu mzee wangu.

Yako mengi sana katika historia ya TANU ya hawa, ''nyoka wa vichwa viwili.'
Na huyo Mzee wako aliyekua akiwapa habari wakoloni ndio baadae alikuja kua Mbunge wa Temeke, Meya wa Jiji la Dar Es Salaam na akijidai kupigania sana haki za Waislamu
 
Na huyo Mzee wako aliyekua akiwapa habari wakoloni ndio baadae alikuja kua Mbunge wa Temeke, Meya wa Jiji la Dar Es Salaam na akijidai kupigania sana haki za Waislamu
Sesten...
Ukitaka kuwa na mjadala na mtu yeyote na mjadala ustawi muhimu sana mtu kuonyesha heshima na uungwana.

"Na huyo mzee wako..." sentensi hadi mwisho inaonyesha umeghadhibika.

Mimi ninapoona mtu kakasirika husitisha mjadala kama njia ya kumtuliza atulie na hasira ziondoke.

Sasa ikiwa atatulia akarejea kwenye mjadala akiwa na maneno mazuri basi tutaendelea na mazungumzo katika hali ya kuheshimiana.

Hivi mjadala unakuwa na tija kwa wote wanaoufuatilia na sote tunajifunza yale ambayo hatukuwa tunayajua.

Binafsi nimejifunza mengi hapa JF.

Huyu "mole" wa Serikali ya Kiingereza ndani ya TANU jina lake ni Ali Mwinyi Tambwe na alikuwa secretary wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika).

Hakupata kuwa mbunge mahali popote lakini alishika nyadhifa nyingi za juu katika serikali baada ya uhuru.

Ali Mwinyi na Abdul Sykes ndiyo walikwenda Nansio, Ukerewe kwa Hamza Mwapachu 1953 kabla ya mkutano wa mwaka wa TAA kupata kauli ya mwisho ya Mwapachu kumuingiza Nyerere ndani ya TAA na kumchagua rais kisha mwaka unaofuatia waunde TANU.

Hiki ni kisa kirefu na muhimu kinachotaka sana utulivu wa fikra.
 
Sesten...
Ukitaka kuwa na mjadala na mtu yeyote na mjadala ustawi muhimu sana mtu kuonyesha heshima na uungwana.

"Na huyo mzee wako..." sentensi hadi mwisho inaonyesha umeghadhibika.

Mimi ninapoona mtu kakasirika husitisha mjadala kama njia ya kumtuliza atulie na hasira ziondoke.

Sasa ikiwa atatulia akarejea kwenye mjadala akiwa na maneno mazuri basi tutaendelea na mazungumzo katika hali ya kuheshimiana.

Hivi mjadala unakuwa na tija kwa wote wanaoufuatilia na sote tunajifunza yale ambayo hatukuwa tunayajua.

Binafsi nimejifunza mengi hapa JF.

Huyu "mole" wa Serikali ya Kiingereza ndani ya TANU jina lake ni Ali Mwinyi Tambwe na alikuwa secretary wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika).

Hakupata kuwa mbunge mahali popote lakini alishika nyadhifa nyingi za juu katika serikali baada ya uhuru.

Ali Mwinyi na Abdul Sykes ndiyo walikwenda Nansio, Ukerewe kwa Hamza Mwapachu 1953 kabla ya mkutano wa mwaka wa TAA kupata kauli ya mwisho ya Mwapachu kumuingiza Nyerere ndani ya TAA na kumchagua rais kisha mwaka unaofuatia waunde TANU.

Hiki ni kisa kirefu na muhimu kinachotaka sana utulivu wa fikra.
Sheikh Mohamed, uniwiye radhi Mzee wangu. Haikua niya wala kusudio langu kutoa maneno ya kukuudhi wala kukuvunjia hishma.

Baada ya kupitia tena bandiko langu kisha nikajiweka kwenye nafasi yako, nakiri kuwa maneno nilotumia yalikua na ukakasi na hakika sikupaswa kufanya hivyo

Kosa jengine nilofanya, niliyemfikiria kama ndio "mole" wa serikali ya Muingereza aliye "muuza" Rashid Ali Meli kumbe siye nawe umetutajia bayana huyo culprit.

Bilashaka nitapata msamaha na radhi zako Mzee wangu
 
Sheikh Mohamed, uniwiye radhi Mzee wangu. Haikua niya wala kusudio langu kutoa maneno ya kukuudhi wala kukuvunjia hishma.

Baada ya kupitia tena bandiko langu kisha nikajiweka kwenye nafasi yako, nakiri kuwa maneno nilotumia yalikua na ukakasi na hakika sikupaswa kufanya hivyo

Kosa jengine nilofanya, niliyemfikiria kama ndio "mole" wa serikali ya Muingereza aliye "muuza" Rashid Ali Meli kumbe siye nawe umetutajia bayana huyo culprit.

Bilashaka nitapata msamaha na radhi zako Mzee wangu
Sesten,
Wewe muungwana.

Sijapata mimi kukutana na mtu mfano wako hapa barzani.

Kaka hayo yamepita.
Tuendelee na mazungumzo.
 
Huyu Rashid Ali Meli alikuwa mmoja kati watu takriban hawazidi 20 waliohudhuria mkutano wa kwanza wa TANU Ukumbi wa Arnautoglo.

Rashid Ali Meli alikuwa mweka fedha Dar es Salaam Municipal Council.

Ilipodhihirika kuwa mfuko wa kumpeleka Nyerere New York UNO una matatizo yeye akaenda kwenye sefu yake kazini akafungua akatoa
fedha kwa siri akamkabidhi Iddi Faiz atie katika safari ya Nyerere kwa makubaliano kuwa TANU itarejesha hizo fedha haraka.

Siku ya pili baada ya Rashid Ali Meli kutoa fedha zile na kuzipeleka TANU wakaguzi wakafika ofisini kwake kufanya ukaguzi.

Walijuaje?

Waingereza walikuwa na mtu wao katika uongozi wa juu wa TANU pale New Street akiwapa taarifa zote kila zinapotokea.

Huyu mtu wao alikuwa huyu mzee wangu.

Yako mengi sana katika historia ya TANU ya hawa, ''nyoka wa vichwa viwili.'
Huyo alikuwa mwizi fisadi hastahili heshima hata nyerere angejua ni pesa za wizi angezikataa
 
Huyo alikuwa mwizi fisadi hastahili heshima hata nyerere angejua ni pesa za wizi angezikataa
Mdukuzi,
Labda mimi nimefanya makosa ya kutoeleza kisa kizima.

Mfuko wa safari ya Mwalimu Nyerere UNO ulikuwa unasimamiwa na Mweka Hazina wa TANU Iddi Faiz Mafungo ambae pia alikuwa Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika).

Katika kuchangisha fedha hizi Iddi Faiz alitoa fedha za Al Jamiatul akazitia katika mfuko wa safari ya Mwalimu Nyerere.

Rashid Ali Meli akachukua fedha kutoka Dar es Salaam Municipal Council akampa Iddi Faiz kwa makubaliano kuwa zitatejeshwa.

Hii ilikuwa muhimu ili Nyerere awahi kikao New York.

Bahati mbaya siku ya pili tu wakaguzi wakafika kwake kukagua mahesabu.

Sijui imekuwaje umeruka na kufikia kwenye tuhuma ya kumwita Rashid Ali Meli ni mwizi na fisadi kwa kuhangaika kufanikisha safari muhimu sana ya Nyerere wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.

Kadi 1000 za TANU za kwanza Ali Sykes alinunua kutokana na fedha zake binafsi na kadi 2000 nyingine alinunua kutoka fedha za Tanganyika Government Servant Association (TAGSA) ambako yeye alikuwa Secretary.

Huwezi kusema huu ni ufisadi au wizi kwani hizo fedha zimetolewa na zitarejeshwa.
 
Mdukuzi,
Labda mimi nimefanya makosa ya.kutoeleza kisa kizima.

Mfuko wa safari ya Mwalimu Nyerere UNO ulikuwa unasimamiwa na Mweka Hazina wa TANU Iddi Faiz Mafungo ambae pia alikuwa Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika).

Katika kuchangisha fedha hizi Iddi Faiz alitoa fedha za Al Jamiatul akazitia katika mfuko wa safari ya Mwalimu Nyerere.

Rashid Ali Meli akachukua fedha kutoka Dar es Salaam Municipal Council akampa Iddi Faiz kwa makubaliano kuwa zitatejeshwa.

Hii ilikuwa muhimu ili Nyerere awahi kikao New York.

Bahati mbaya siku ya pili tu wakaguzi wakafika kwake kukagua mahesabu.

Sijui imekuwaje umeruka na kufikia kwenye tuhuma ya kumwita Rashid Ali Meli ni mwizi na fisadi kwa kuhangaika kufanikisha safari muhimu sana ya Nyerere wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.

Kadi 1000 za TANU za kwanza Ali Sykes alinunua kutokana na fedha zake binafsi na kadi 2000 nyingine alinunua kutoka fedha za Tanganyika Government Servant Association (TAGSA) ambako yeye alikuwa Secretary.

Huwezi kusema huu ni ufisadi au wizi kwani hizo fedha zimetolewa na zitarejeshwa.
Hapo tumeelewana
 
Back
Top Bottom