Rashid Makwiro (Chid Benz) hali yake ni tete kutokana na matumizi makubwa ya madawa ya kulevya

Kumuionea huruma mtu asiyejionea huruma yeye, ni aina nyingine hai ya ukichaa
 
Kwann Police isimkamate ikamtia ndani ata mwaka tu uku akipewa tiba na lamsingi akiwataja wanamtandao wote wanaofanya biashara ya Unga....Muda ambayo wamemuweka LEMA Rumande nadhani wangewaweka mateja wote Rumande kwa muda wa miezi 3 hadi 6 wakipewa matibabu nadhani hii biashara itarudi nyuma ata kufa kabisa....Tunahitaji Rais km Duterte wa Philipino ili apambane na Waunza Sembe
 
Nimepost hii habari ya kumwembe kumbe tayari ipo humu


Eddo kaandika kwa hisia sana habari hii
 
siana uhakika sana,hivi kutumia madawa ya kulevya sio kosa kisheria? kama ndio kwa nini huyu asichukuliwe hatua kwa sbb ushahidi upo waziwazi?
 
Serikali ikazie mkazo zaid uingizaj wa madawa ya kulevya nchini na izuie..yanamaliza nguvu kazi ya taifa letu
 
Huyu zuzu alimtukana Lowassa wacha akome
Vipi kuhusu Chairman? Si alimwita kibaka, Vipi kuhusu Mchungaji? Si alisema wote wanaomshadadia huyu mzee wakapimwe akili, Vipi kuhusu yule aliyesema kumtukana huyu mzee ni jambo jema hata Mungu anapenda. Vipi kuhusu matusi ya Dr. Slaa kule Arumeru Kuhusu huyu mzee? Vipi kuhusu wakili msomi na matusi yake kwa huyu Mzee? Au umesahau ya yule mbunge wa ubungo hadi akamwagiwa tindikali, Vipi kuhusu yule wa Kibamba ambaye hadi leo anamuonea aibu huyu mzee na anashindwa hata kumuangalia usoni. Vipi kuhusu list of shame ya pale Mwembe Yanga? Au yalikuwa maigizo yote yale ya kutaka madaraka kwa kuamini watanzania ni Mbumbumbu? Chidi Benz ni msanii tu kama alivyo Dudu Baya au Sungu.
 
wale wanaokula methadone pale mwananyamala mbona changes naziona? wako smart siku hizi na kazi wanafanya

kama ray c kashindwa nadhani chid kama mwanaume ataweza kula dozi kwa usahihi na kurudi kwenye hali yake

aamue tu
Ray c karudia nae?
 
Chid Benzi anatushangaa tunavyomshangaa

Na Edo Kumwembe
NI zaidi ya kujikuta juu ya kitanda na msichana unayempenda kuliko wote duniani. Ni zaidi ya kutazama bao la ushindi la timu yako katika dakika za majeruhi katika mechi muhimu. Yote haya hayazidi starehe ya kubwia unga.

Sahau kuhusu bia, sigara, Sahau kuhusu kila starehe. Inatajwa kuwa hakuna starehe kama unga. Na sasa Watanzania wanaendelea kumshangaa mtu anayeitwa Chid Benz. Mwanamuziki hodari wa kizazi hiki katika zile staili za vijana za muziki wa kufokafoka.

Chid anateketea. Mwili wake kwa sasa ni kama mahindi ya shambani yaliyoliwa na nzige. Mwili wake ni kama kama gari lililoungua likaisha. Amebaki mifupa tu. Unaweza kupishana naye bila ya kumfahamu kama bado kichwani unatembea na taswira ya yule Chid Benzino mwenye mashavu manene, miwani usoni, na taulo shingoni.

Wasichofahamu watu wengi ni ukweli kwamba wakati sisi tukiendelea kumshangaa Chid, kumbe yeye ndiye anatushangaa zaidi sisi. Anatushangaa kwanini hatuungani naye katika starehe yake tamu. Anatushangaa kwanini hatupo katika safari yake ya kubembea.

Kwanini anatushangaa? Ninesema hapo juu hakuna starehe tamu zaidi ya unga. Kitu cha muhimu hili ni kutoonja starehe yenyewe. Ukionja hautabaki. Hata Chid si ajabu zamani alikuwa analaani wala unga. Kosa kubwa alilifanya katika kuonja tu. Ukionja ni vigumu kutoka katika mtego.

Ni hapo ndipo lilipo tatizo la Chid na watumiaji wengine. Kikubwa wanachotakiwa kukifanya kuachana na unga hawawezi kukifanya. Kitu cha kwanza kabisa ni kuukana utamu wake. Kuukana utamu wake ni kama kuikana nafsi yako. Hapa ndipo ilipo vita kubwa ya kuacha.

Kwanza inabidi uone mapungufu makubwa ya unga lakini kama ukilegeza moyo kamwe hauwezi. Kwa mfano, leo Chid hajioni mchafu, hajioni amekonda, hajioni amepoteza nuru. Utamu wa unga umezidi akili ya kujitafakari (self assessment). Ikifika hapo kazi inakuwa nzito zaidi.

Kumpeleka Chid katika vituo vya matibabu (rehabilitation centres) ni kupoteza muda mpaka pale moyo wake utakapoanza kujifanyia self assessment kuwa amepotea, anahitaji msaada na anachukia unga. Akifika hapo atashinda vita.

Chukulia kwamba familia yako imekuomba mtoke out na uwape muda wa kuwa na wewe. Wanaweza na tabia yako ya kupenda mpira kuliko wewe. Unawakubalia walichokuomba. Lakini wanakupeleka katika hoteli ambayo watu wanatazama mpira. Lazima moyo wako utakuwa unafuatilia kwa karibu matokeo huku mwili wako ukiwa mezani na familia.

Kitu cha aina hiki kinaitwa addiction. Ndipo alipofika Chid. Kama ambavyo wewe unashangaa kwanini mtu hapendi mpira au muziki, basi na ndivyo Chid anavyotushangaa kwanini na sisi wengine hatupendi unga. Alipofikia yeye na sisi wengine wote tumefika ingawa sisi tuna starehe tofauti na yeye.

Kabla ya matibabu kitu cha msingi kwa Chid ni kukutana na mwanasaikolojia wa kumshawishi aelewe kwamba kitu anachokiona kitamu kumbe sio kitamu. Nani anaiweza kazi hii? Ni kazi ngumu. Ndio maana washkaji zake walipompeleka Bagamoyo alitoroka na kuendelea na starehe yake kwa sababu hakuwa tayari kuona utamu wake unaitwa uchungu.

Mwisho wa Chid? Sitaki kuingilia kazi ya Mwenyezi Mungu lakini mwisho wake unatabirika kiurahisi zaidi pengine kuliko mwisho wa watu wengi tunaomshangaa. Sisi tuna siku zetu za ahadi na tunaweza kuondoka mapema hapa duniani kuliko yeye, hata hivyo tutaondoka kwa vifo visivyotabirika.

Chid anaweza kufuata njia za akina Whitney Houston tu. Watu wengi wa aina yake huwa inatokea tunawaokota mtaroni au chumbani wakiwa wametangulia Mbele ya haki. Inatokea huwa wanajidunga kupitiliza, au kuliko miili yao inavyoweza kuhimili uzito wa dawa aliyotumia siku hiyo. Kwa kiingereza cha matumizi ya unga wanaita overdosing.

Hili sio la kuombea lakini maisha ya kufichana yamepita zamani jamani. Kama tunahitaji lisitokee basi ni kwa Chid mwenyewe kumjua adui yake na kupambana naye. Adui wa Chid sio unga. Adui wa Chid ni akili yake mwenyewe. Unga upo tu, lakini mbona wengi hatutumii?

Ana bahati mbaya ameangukia katika starehe ambayo inammaliza. Sisi wengine tuna matatizo kama yake ya kuendekeza starehe lakini bahati nzuri huwa hazitumalizi. Starehe ya kubishana nani zaidi ya Lionel Messi na Ronaldo haiwezi kutumaliza kwa urahisi.

FIKRA NGUMU A.K.A KILAZA
 
mamake kamharibu huyu mtoto. ni mfanyakazi pale TRA anamdekeza balaa. tujifunze kulea watoto katika maadili ili wakiwa wakubwa wasipotee.
Nilihisi labda ametokea kwenye familia duni?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…