Elius W Ndabila
JF-Expert Member
- Jul 17, 2019
- 324
- 649
Na Elius Ndabila[0768239284]
Watanzania wengi ukizungumza jina la Rashidi Matumla si geni vinywani mwao hata machoni kwani ni moja ya watanzania wachache waliolitangaza Taifa hili kwa medani ya ngumi. Matumla ambaye historia ya ngumi inamuonyesha alianza kupigana mwaka 1978 chini ya uangalizi wa baba yake alifikia hatua ya kuwa bondia wa 20 bora duniani. Matumla amewahi kushinda mapambano ya ubingwa wa dunia ya WBU, UBO na baadhi ya mikanda ya Afrika .
Pamoja na Rashidi Matumla kuwa na historia kubwa katika Taifa hili, lakini maisha ya MATUMLA ya sasa yanahitaji msaada mkubwa ili kumrudisha Matumla kwenye historia yake au kwenye darasa la kupika akina Matumla wengine. Kisa cha Matumla kinaanzia hapa;-
Matumla anasema mwaka 2005 alienda Afrika Kusini kwenye mazoezi ya kujiandaa na mashindano ya ngumi. Anasema akiwa huko na Mwalimu wake kuna chuma alichokuwa akifanyia mazoezi alikosea kukiinua juu, kitu kilichopelekea kupata maumivu ya mgongo. Anasema baada ya kupata tatizo hilo alifikiri ni tatizo la kawaida na angeweza kupona kwa muda mfupi. Yaani hakulitilia maanani sana, hivyokuendelea na kaziyake ya ngumi.
Matumla anaendelea kusimulia mkasa wake kwa kusema, alianza kushangaa kadiri miaka ilivyokuwa ikienda maumivu ya mgongo yakawa yanaongezeka na kibaya zaidi hata machoyake yakawa na shida. Anasema ilifikia mahali hata kama kuna kitu kimoja yeye anaona kama kuna vitu vitatu. Anasem hii ilimpa sana shida na ikamfanya aachane kabisa na mashindano ya ngumi kwani maumivu ya mgongo ni makali. Anaendelea kuwa kwa sasa haoni raha ya dunia.
Masimulizi ya ndugu Matumla ambayo yamejaa huzuni na simanzi, yanatutaka Watanzania wazalendo na wenye moyo wa dhati na tuliokuwa mashabiki wake hasa wapenzi wa soka kumsaidia.
Matumla anasema kwamba baada ya kuona hali yake inazidi kuwa dhofu aliamua kumtafuta Mh Jakaya Kikwete Rais wa awamu ya nne kwa kipindi hicho. Anasema juhudi za kumpata Jk zilikuwa ngumu, lakini kama bahati alifanikiwa kukutana na mototo wa Mh Kikwete ambaye alimuomba amfikishie ujumbe huo Baba yake. Anasema baadae Mzee Kikwete alimpigia simu ilikutaka kujua hali yake. Anasema alimusimulia ABCDs zote ndipo JK alipoamua kumuunganisha na Dakitari wake kwa uchunguzi. Anasema baadae mh Rais wa wakati huo Mh Kikwete alisema aende hospitali ili wakamfanyie vipimo vyote. ANASEMA Matumla
Matumla anaendelea kwa kusema baada ya kwenda hospitali alipatiwa vipimo kwa gharama ya shilingi laki nane ambazo Mh Jk alizitoa. Anasema baaa ya vipimo hivyo kutokana na hali aliyokuwa nayo alishauriwa na dakitari kuwa aende Mhimbilikupata matibabu. Anasema alirudi nyumbani ili akajipange kwa safari ya kwenda Mhimbili. Anasema kwa kuwa tiyari alikuwa yupo kwenye mdororo wa kiuchumi alitegemea kupata fedha toka kwa Mh Rais, lakini kwa bahati mbaya akawa amepoteza mawasiliano yake hivyo ikawa ngumu kumpata Mh JK[Rais kwa kipindi hicho]. Anasema baada ya kukosa mawasiliano alianza kutafuta msaada kwa wadau wengine lakini hakufanikiwa.
‘’eee Bwana ee, utu ni fedha. Bila fedha Dunia hii wewe ni takataka. Marafiki nao wanakuja ukiwa na fedha, kama huna fedha unakuwa ni wewe na taabu zako. Hivi unajua hata mke wangu wa ndoa niliyezaa naye watoto watatu alinikimbia na kuolewa kwingine baada ya kuugua? Niliamini fedha inaongeza udugu, lakini umasikini ni upanga wa kuharibu udugu’’
Rashidi Matumla anasema ili kuhakikisha anaokoa hai wake na kulea watoto wake ameshajaribu kuwatafuta baadhi ya viongozi wa serikali ambao aliamini wangeweza kumsaidia kupata matibabu ameshindwa. Anasema amejaribu kwenda kwa Rc wa DSM ili kutoa kilio chake amekuwa hafanikiwi kumfikia kila anapoenda. Anasema pia ameenda mara kadha kumuona Mh Mwakyembe lakini ameshindwa pia kumuona. Anasema Rais wa chama cha ngumi anajua kuwa sasa anaumwa na anahitaji msaada lakini hawajaweza kumsaidia.
Ni bora nikasaidiwa sasa kupata msaada nikatibiwa nikaendelea kulea wanangu. Hivi nikifa hizo rambi rambi zitanisaidia nini? Nikiumwa nikalala kitandani siwezi hata kuamka hizo pole na fedha zitasaidia nini? Ukinisaidia leo nikipona na mimi nitaendelea kulitumikia Taifa kwa njia nyingine. Sasa umarufu wangu ulikwisha. Hata watu wasiojua kuwa ninaumwa wakiniona kwenye dalala wananyosheana vidole kuwa huyu kafuata nini? Hawajui sasa mimi si Matumla wa miaka ile, ni Matumla ambaye wakati mwingine hata ukinywa chai unamshujuru Mungu., Anasema Matumla.
Matumla anasema anaomba kilio chake kimfikia Mh Rais wa Tanzania DKT John Magufuli, mzalendo wa kweli wa Taifa hili na watanzania wengine wazalendo ili aweze kupata matibabu. Anasema akipona ataendelea kuwafundisha Watanzania wengine ngumi ili kuendelea kuitangaza Tanzania katika medani ya kimataifa.
Matumla anawaasa wanandondi wengine na michezo mingine kuwa na nidhamu ya fedha wanapokuwa wanazipata. Anasema yeye sasa anaweza kuwa mwalimu. Anasisitiz kuwa umaarufu walionao na marafiki walionao ni kwa sababuya fedha, lakini bila fedha marafiki wote watawakimbia. Anatolea mfano kwake kuwa, yeye enzi zake alikuwa akipigiwa simu nyingi za ndugu, jamaa na marafiki, lakini siku hizi ni watu wachache wanampigia na wengine hata akiwapigia huwa hawapokei simu zake. Anawashauri wengine wajifunze kwake kwa kuwa na nidhamu ya maisha kwani siku ya kuanguka kwao hawaijui kama yeye ambavyo alikuwa hajui.
Matumla anaomba msaada kwa Mtanzania yeyote ili aweze kutibiwa. Namba yake ya simu ni 0672219223.
Watanzania wengi ukizungumza jina la Rashidi Matumla si geni vinywani mwao hata machoni kwani ni moja ya watanzania wachache waliolitangaza Taifa hili kwa medani ya ngumi. Matumla ambaye historia ya ngumi inamuonyesha alianza kupigana mwaka 1978 chini ya uangalizi wa baba yake alifikia hatua ya kuwa bondia wa 20 bora duniani. Matumla amewahi kushinda mapambano ya ubingwa wa dunia ya WBU, UBO na baadhi ya mikanda ya Afrika .
Pamoja na Rashidi Matumla kuwa na historia kubwa katika Taifa hili, lakini maisha ya MATUMLA ya sasa yanahitaji msaada mkubwa ili kumrudisha Matumla kwenye historia yake au kwenye darasa la kupika akina Matumla wengine. Kisa cha Matumla kinaanzia hapa;-
Matumla anasema mwaka 2005 alienda Afrika Kusini kwenye mazoezi ya kujiandaa na mashindano ya ngumi. Anasema akiwa huko na Mwalimu wake kuna chuma alichokuwa akifanyia mazoezi alikosea kukiinua juu, kitu kilichopelekea kupata maumivu ya mgongo. Anasema baada ya kupata tatizo hilo alifikiri ni tatizo la kawaida na angeweza kupona kwa muda mfupi. Yaani hakulitilia maanani sana, hivyokuendelea na kaziyake ya ngumi.
Matumla anaendelea kusimulia mkasa wake kwa kusema, alianza kushangaa kadiri miaka ilivyokuwa ikienda maumivu ya mgongo yakawa yanaongezeka na kibaya zaidi hata machoyake yakawa na shida. Anasema ilifikia mahali hata kama kuna kitu kimoja yeye anaona kama kuna vitu vitatu. Anasem hii ilimpa sana shida na ikamfanya aachane kabisa na mashindano ya ngumi kwani maumivu ya mgongo ni makali. Anaendelea kuwa kwa sasa haoni raha ya dunia.
Masimulizi ya ndugu Matumla ambayo yamejaa huzuni na simanzi, yanatutaka Watanzania wazalendo na wenye moyo wa dhati na tuliokuwa mashabiki wake hasa wapenzi wa soka kumsaidia.
Matumla anasema kwamba baada ya kuona hali yake inazidi kuwa dhofu aliamua kumtafuta Mh Jakaya Kikwete Rais wa awamu ya nne kwa kipindi hicho. Anasema juhudi za kumpata Jk zilikuwa ngumu, lakini kama bahati alifanikiwa kukutana na mototo wa Mh Kikwete ambaye alimuomba amfikishie ujumbe huo Baba yake. Anasema baadae Mzee Kikwete alimpigia simu ilikutaka kujua hali yake. Anasema alimusimulia ABCDs zote ndipo JK alipoamua kumuunganisha na Dakitari wake kwa uchunguzi. Anasema baadae mh Rais wa wakati huo Mh Kikwete alisema aende hospitali ili wakamfanyie vipimo vyote. ANASEMA Matumla
Matumla anaendelea kwa kusema baada ya kwenda hospitali alipatiwa vipimo kwa gharama ya shilingi laki nane ambazo Mh Jk alizitoa. Anasema baaa ya vipimo hivyo kutokana na hali aliyokuwa nayo alishauriwa na dakitari kuwa aende Mhimbilikupata matibabu. Anasema alirudi nyumbani ili akajipange kwa safari ya kwenda Mhimbili. Anasema kwa kuwa tiyari alikuwa yupo kwenye mdororo wa kiuchumi alitegemea kupata fedha toka kwa Mh Rais, lakini kwa bahati mbaya akawa amepoteza mawasiliano yake hivyo ikawa ngumu kumpata Mh JK[Rais kwa kipindi hicho]. Anasema baada ya kukosa mawasiliano alianza kutafuta msaada kwa wadau wengine lakini hakufanikiwa.
‘’eee Bwana ee, utu ni fedha. Bila fedha Dunia hii wewe ni takataka. Marafiki nao wanakuja ukiwa na fedha, kama huna fedha unakuwa ni wewe na taabu zako. Hivi unajua hata mke wangu wa ndoa niliyezaa naye watoto watatu alinikimbia na kuolewa kwingine baada ya kuugua? Niliamini fedha inaongeza udugu, lakini umasikini ni upanga wa kuharibu udugu’’
Rashidi Matumla anasema ili kuhakikisha anaokoa hai wake na kulea watoto wake ameshajaribu kuwatafuta baadhi ya viongozi wa serikali ambao aliamini wangeweza kumsaidia kupata matibabu ameshindwa. Anasema amejaribu kwenda kwa Rc wa DSM ili kutoa kilio chake amekuwa hafanikiwi kumfikia kila anapoenda. Anasema pia ameenda mara kadha kumuona Mh Mwakyembe lakini ameshindwa pia kumuona. Anasema Rais wa chama cha ngumi anajua kuwa sasa anaumwa na anahitaji msaada lakini hawajaweza kumsaidia.
Ni bora nikasaidiwa sasa kupata msaada nikatibiwa nikaendelea kulea wanangu. Hivi nikifa hizo rambi rambi zitanisaidia nini? Nikiumwa nikalala kitandani siwezi hata kuamka hizo pole na fedha zitasaidia nini? Ukinisaidia leo nikipona na mimi nitaendelea kulitumikia Taifa kwa njia nyingine. Sasa umarufu wangu ulikwisha. Hata watu wasiojua kuwa ninaumwa wakiniona kwenye dalala wananyosheana vidole kuwa huyu kafuata nini? Hawajui sasa mimi si Matumla wa miaka ile, ni Matumla ambaye wakati mwingine hata ukinywa chai unamshujuru Mungu., Anasema Matumla.
Matumla anasema anaomba kilio chake kimfikia Mh Rais wa Tanzania DKT John Magufuli, mzalendo wa kweli wa Taifa hili na watanzania wengine wazalendo ili aweze kupata matibabu. Anasema akipona ataendelea kuwafundisha Watanzania wengine ngumi ili kuendelea kuitangaza Tanzania katika medani ya kimataifa.
Matumla anawaasa wanandondi wengine na michezo mingine kuwa na nidhamu ya fedha wanapokuwa wanazipata. Anasema yeye sasa anaweza kuwa mwalimu. Anasisitiz kuwa umaarufu walionao na marafiki walionao ni kwa sababuya fedha, lakini bila fedha marafiki wote watawakimbia. Anatolea mfano kwake kuwa, yeye enzi zake alikuwa akipigiwa simu nyingi za ndugu, jamaa na marafiki, lakini siku hizi ni watu wachache wanampigia na wengine hata akiwapigia huwa hawapokei simu zake. Anawashauri wengine wajifunze kwake kwa kuwa na nidhamu ya maisha kwani siku ya kuanguka kwao hawaijui kama yeye ambavyo alikuwa hajui.
Matumla anaomba msaada kwa Mtanzania yeyote ili aweze kutibiwa. Namba yake ya simu ni 0672219223.