Rasimu inayopendekezwa ishindanishwe na rasimu ya pili ya jaji warioba

Rasimu inayopendekezwa ishindanishwe na rasimu ya pili ya jaji warioba

jsekiku

Member
Joined
Jan 12, 2009
Posts
25
Reaction score
7
KUHUSU KURA YA MAONI na muchakato mzima wa kupata katiba mpya inayokubalika

Nimepata wazo jipya, badala ya kusema tunapigia kura rasimu ya katiba inayopendekezwa, kura ya ndiyo au hapana, Afadhali kuwekwe rasimu ya katiba inayopendekezwa ishindanishe au ipigiwe kura na rasimu ya katiba ya warioba. Hii itatupa wananchi fursa ya kuchagua tunachokitaka badala ya kutuwekea hii moja. Upande moja kuna inayopendekezwa upande mwingine, kuwepo na giza? Ni kama chaguzi zilizokuwa zikiendeshwa enzi za mwalimu Nyerere kila walipokwenda kumpigia kura, huku hakuwa na mshindani.

Kwa kuwa katiba inayopendekezwa inayo makundi mawili yanayoshindana: ya wale wa HAPANA, na wale wa NDIYO, mchakato huu ikiachwa ukiendelea kama ilivyo kwa sasa, itakuwa vigumu kupata katiba inayokubalika. Suala la katiba si suala la nani mwenye nguvu. Suala la katiba ni makubaliano ya kila moja jinsi wanavyotaka kutawaliwa au kuongozwa.

Kwa kuwa tayari yapo makundi mawili yanayopingana, naona kuwa tunaelekea kuunda katiba mbili katika Taifa moja. Hata hivyo, tunaelekea kuwa na katiba 3 kwani Zanzibara wanayo katiba yao, na huku Tanzania bara, tunataka kuwa na katiba mbili tofauti.

Kwa watakao kuwa na kura ya HAPANA, Je watakubali kutawaliwa na katiba wasiokubali AU serikali itatumia nguvu kuwalazimisha walioikata?

Nashauri kwa kura ya maoni kuwa nzuri, heri tusema kuwa: siku ya kupiga kura ya maoni, kuwepo katiba inayopendekezwa na upande wa pili kuwepo na rasimu ya katiba ya warioba. Wananchi waamue wanataka ipi. Nafikiri hii tamaliza matatizo.
 
Daaa yaani nakuonea huruma na kukupa pole, lakini sio wewe ni uelewa mdogo ulio nao umeshindwa kuelewa kuwa mchakato wa kutunga Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umefikia hatua ya wananchi kuipigia kura Katiba Inayopendekezwa, iliyopitishwa na Bunge Maalum tarehe 4 Oktoba, 2014.

Awali, Tume ya Mabadiliko ya Katiba ilitoa Rasimu ya Kwanza tarehe 3 Juni, 2013 na Rasimu ya Pili ilitolewa tarehe 30 Desemba, 2014 na kuwasilishwa kwenye Bunge Maalum tarehe 21 Februari, 2014. Baada ya Bunge Maalum kukamilisha majukumu kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011, tunda lililozaliwa ni KATIBA INAYOPENDEKEZWA.

Hatua inayofuata ni ya wananchi kuipigia kura Katiba Inayopendekezwa.Baada ya Bunge Maalum kukamilisha majukumu kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011, tunda lililozaliwa ni KATIBA INAYOPENDEKEZWA. Hatua inayofuata ni ya wananchi kuipigia kura Katiba Inayopendekezwa. Hivyo basi, kwa mujibu wa sheria, wananchi ndiyo wenye uamuzi na kauli ya mwisho juu ya upatikanaji wa Katiba Mpya. KWA KIPINDI TULICHONACHO HAPA RASIMU YA WARIOBA HAINA NAFASI.
 
KUHUSU KURA YA MAONI na muchakato mzima wa kupata katiba mpya inayokubalika

Nimepata wazo jipya, badala ya kusema tunapigia kura rasimu ya katiba inayopendekezwa, kura ya ndiyo au hapana, Afadhali kuwekwe rasimu ya katiba inayopendekezwa ishindanishe au ipigiwe kura na rasimu ya katiba ya warioba. Hii itatupa wananchi fursa ya kuchagua tunachokitaka badala ya kutuwekea hii moja. Upande moja kuna inayopendekezwa upande mwingine, kuwepo na giza? Ni kama chaguzi zilizokuwa zikiendeshwa enzi za mwalimu Nyerere kila walipokwenda kumpigia kura, huku hakuwa na mshindani.

Kwa kuwa katiba inayopendekezwa inayo makundi mawili yanayoshindana: ya wale wa HAPANA, na wale wa NDIYO, mchakato huu ikiachwa ukiendelea kama ilivyo kwa sasa, itakuwa vigumu kupata katiba inayokubalika. Suala la katiba si suala la nani mwenye nguvu. Suala la katiba ni makubaliano ya kila moja jinsi wanavyotaka kutawaliwa au kuongozwa.

Kwa kuwa tayari yapo makundi mawili yanayopingana, naona kuwa tunaelekea kuunda katiba mbili katika Taifa moja. Hata hivyo, tunaelekea kuwa na katiba 3 kwani Zanzibara wanayo katiba yao, na huku Tanzania bara, tunataka kuwa na katiba mbili tofauti.

Kwa watakao kuwa na kura ya HAPANA, Je watakubali kutawaliwa na katiba wasiokubali AU serikali itatumia nguvu kuwalazimisha walioikata?

Nashauri kwa kura ya maoni kuwa nzuri, heri tusema kuwa: siku ya kupiga kura ya maoni, kuwepo katiba inayopendekezwa na upande wa pili kuwepo na rasimu ya katiba ya warioba. Wananchi waamue wanataka ipi. Nafikiri hii tamaliza matatizo.
Rubbish hujui hata unachokiongea hata sheria ya mabadiliko ya katiba hujui.....wewe ni mmoja ya watu waliofeli darasani hasa kwa kutojua swali linataka nini unaingia kichwakichwa....unaweka utopia wako kwenye mtihani mwisho wa siku unaangukia puaaaaa........
 
Rubbish hujui hata unachokiongea hata sheria ya mabadiliko ya katiba hujui.....wewe ni mmoja ya watu waliofeli darasani hasa kwa kutojua swali linataka nini unaingia kichwakichwa....unaweka utopia wako kwenye mtihani mwisho wa siku unaangukia puaaaaa........


KAZI YAKE ILIKUWA NI KUPIGA CHABO TU CLASS HUYO NDO MAAAN HATA KWENYE PEPA ANAJIBU KINYUME NA MAELEKEZO. Hajielewi huyo msamehe bureee
 
Back
Top Bottom