Rasimu ya katiba mpya: Maraisi watatu kwenye nchi moja " big no"

Rasimu ya katiba mpya: Maraisi watatu kwenye nchi moja " big no"

sirjimmy

Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
14
Reaction score
9
Maoni yangu kama ningekuwa karibu na warioba. Naunga mkono serikali tatu ila kuwe na raisi mmoja wa jamhuri wa muungano, kuwe na waziri mkuu wa tz bara na waziri mkuu wa zenji. Raisi wa muungano atachaguliwa na wapiga kura wa tz bara na visiwani, mawaziri wakuu watachaguliwa na wapiga kura wa nchi husika. Hakuna haja ya kuwa na marais watatu kwenye nchi moja
 
Sijui tutakaaje
971508_537375292991330_146115531_n.jpg
 
Maoni yangu kama ningekuwa karibu na warioba .
Naunga mkono serikali tatu ila kuwe na raisi mmoja wa jamhuri wa muungano,
kuwe na waziri mkuu wa tz bara na waziri mkuu wa zenji.
Raisi wa muungano atachaguliwa na wapiga kura wa tz bara na visiwani,
mawaziri wakuu watachaguliwa na wapiga kura wa nchi husika.
Hakuna haja ya kuwa na marais watatu kwenye nchi moja

Wazanzibari wanahitaji Zanzibar iwe nchi kamili. Kwa maana iwe na Rais wake. Hao wakishasema kitu, ndio msimamamo wao. Vinginevyo unatafuta tafaruku. Wanasema 66% ya Wazanzibar wanataka Zanzibar itambulike kama nchi kamili. Maoni yangu ni kwamba, tukubali Tanganyika iwe nchi kamili na Zanzibar vivyo hivyo halafu tujadiliane upya namna ya kuungana upya.
 
Maoni yangu kama ningekuwa karibu na warioba .
Naunga mkono serikali tatu ila kuwe na raisi mmoja wa jamhuri wa muungano,
kuwe na waziri mkuu wa tz bara na waziri mkuu wa zenji.
Raisi wa muungano atachaguliwa na wapiga kura wa tz bara na visiwani,
mawaziri wakuu watachaguliwa na wapiga kura wa nchi husika.
Hakuna haja ya kuwa na marais watatu kwenye nchi moja
Kama sio serikali tatu basi iwe moja lakini serikali mbili ni 'big NO!' Hicho unachopendekeza cha mawaziri wakuu ni mfumo kama wa serikali moja.
 
Maoni yangu kama ningekuwa karibu na warioba .
Naunga mkono serikali tatu ila kuwe na raisi mmoja wa jamhuri wa muungano,
kuwe na waziri mkuu wa tz bara na waziri mkuu wa zenji.
Raisi wa muungano atachaguliwa na wapiga kura wa tz bara na visiwani,
mawaziri wakuu watachaguliwa na wapiga kura wa nchi husika.
Hakuna haja ya kuwa na marais watatu kwenye nchi moja


Tatizo nini, tulishakuwa nao wawili mmoja kuongezeka si tatizo. Kama ilivyokuwa kwenye Katiba hii Rais wa Muungano atakuwa hana mamlaka kwa mambo yasiyokuwa ya Muungano, yake ni yale machache tu.
 
Nchi ni mbili yaani Tanganyika na Zanzibar. Maraisi watakuwa watatu yaani wa Tanganyika, Zanzibar na wa muungano yeye atakuwa kama co -ordinator tu!
 
hata kukiwa na marais 100, mimi maskini wa huku kijijini sitimbwi sijali,
ninachotaka ni waniondolee umaskini wangu,
 
Kutokana na mapendekezo ya rasimu ya katiba mpya kuwa kuwe na serikali tatu yaani ya Tanganyika, Zanzibar na Muungano, mimi natoa mapendekezo yafuatayo kuhusiana na ikulu za serikali hizo endapo itapitishwa
1. Ikulu ya Dar es Salaam(Magogoni) iwe ni ya serikali ya Tanganyika
2. Serikali ya Zanzibar kwasababu ipo na ina ikulu tayari iendelee kutumia ikulu yake ya sasa
3. Serikali ya muungano au ya shirikisho isiwe na ikulu ya kudumu kati ya Tanganyika na Zanzibar. Mimi napendekeza serikali hii iwe inabadilisha makao yake kati ya Tanganyika na Zanzibar kwa zamu kila baada ya miaka mitano. Kwa sasa napendekeza kutolewe majengo au kujengwe ikulu Zanzibar ambako serikali ya muungano itaanzia kwa kuwa toka nchi hizi zilipoungana makao makuu ya serikali ya muungano yamekuwa Dar es Salaam katika ikulu ya Magogoni na wakati huo huo ikisimamia mambo ya Tanganyika. Baada ya miaka mitano serikali ya muungano itakayochaguliwa itahamia Tanganyika ambako itapewa majengo ya ikulu popote ingawa mimi napendekeza iwe Dodoma au kama itakuwa Dar, Ikulu ya serikali ya Tanganyika iwe Dodoma! Mtindo huu wa kupokezana ikulu ya serikali ya muungano kwa zamu utasaidia kuleta usawa katika Shirikisho au muungano hivyo kufanya kila upande wa muungano kupata nafasi ya kuihudumia serikali hiyo.

Haya ni maoni yangu na ninaunga mkono kuwa na serikali tatu hivyo kupelekea kufufuka kwa TANGANYIKA yetu!
 
kila kitu lazima kiwe na changamoto zake kawa hiyo muundo wowote ule utakuwa na changamoto.
 
sisi tunataka tanganyika yetu. baada ya hapo hata zanzibar wakitaka watoe marais wa muungano miaka 20 sawa tu. srlikali ya tanganyika ni ukombozi. na yeyeyote anayepinga serikali ya tanganyika ni fisadi kwani anafaidika na mfumo wa ajabu wa serikali mbili ambao ni kiini macho
 
Maoni yangu kama ningekuwa karibu na warioba. Naunga mkono serikali tatu ila kuwe na raisi mmoja wa jamhuri wa muungano, kuwe na waziri mkuu wa tz bara na waziri mkuu wa zenji. Raisi wa muungano atachaguliwa na wapiga kura wa tz bara na visiwani, mawaziri wakuu watachaguliwa na wapiga kura wa nchi husika. Hakuna haja ya kuwa na marais watatu kwenye nchi moja
Hilo si jina tuu "waziri mkuu". Sala ni anapatikanaje na majumu yake ni nini. sio lazima aitwe hata waziri mkuu. anaweza itwa chief Senetor au Mwagoda wa Tanganyika. Muundo wa sasa una serikali tatu, lakini unafiki umetuzidi.
 
Mimi nawashangaa watu, mbona walikuwa wawili kwanini hamkupiga kelele??
 
watu hamsomi wala rasimu yoyote tena unasema umeskiaaa huu n umburura...
raisi mmmoja waliobak n magavana tu
 
Wazanzibari wanahitaji Zanzibar iwe nchi kamili. Kwa maana iwe na Rais wake. Hao wakishasema kitu, ndio msimamamo wao. Vinginevyo unatafuta tafaruku. Wanasema 66% ya Wazanzibar wanataka Zanzibar itambulike kama nchi kamili. Maoni yangu ni kwamba, tukubali Tanganyika iwe nchi kamili na Zanzibar vivyo hivyo halafu tujadiliane upya namna ya kuungana upya.

Tungekua na viongozi wenye akili kama zako tungekua mbali sana, me nadhani kila mmoja asimame kwa miguu yake huu Muungano hauna haja sana tueke makubaliano ya kuishi kwa amani tu.
 
Hilo si jina tuu "waziri mkuu". Sala ni anapatikanaje na majumu yake ni nini. sio lazima aitwe hata waziri mkuu. anaweza itwa chief Senetor au Mwagoda wa Tanganyika. Muundo wa sasa una serikali tatu, lakini unafiki umetuzidi.

miaka 50 tumekua na maraisi wawili kwa sasa huyo wa muungano hana haja tena raisi asimamie mambo 7 tu kupoteza pesa za walipa kodi.
 
Hilo si jina tuu "waziri mkuu". Sala ni anapatikanaje na majumu yake ni nini. sio lazima aitwe hata waziri mkuu. anaweza itwa chief Senetor au Mwagoda wa Tanganyika. Muundo wa sasa una serikali tatu, lakini unafiki umetuzidi.

Unachosema ni kweli.
Hati ya Muungano ina vipengele :
(a) a separate legislature and executive in and for Zanzibar from time to time constituted in accordance with the existing law of Zanzibar and having exclusive authority within Zanzibar for matters other than those reserved to the Parliament and Executive of the united Republic;.......

And the said Parliament and Executive shall have exclusive authority in such matters throughout and for the purposes of the united Republic and in addition exclusive authority in respect of all other matters in and for Tanganyika.(v) The existing laws of Tanganyika and of Zanzibar shall remain in force in their respective territories subject-
Muundo wa sasa uko hivi:
Zitakuwepo serikali tatu, Serikali ya mambo ya Tanganyika, serikali ya mambo ya Zanzibar na serikali ya mambo ya Muungano.
Ili kubana matumizi kwa maoni ya Mwalimu, Serikali ya mambo ya Tanganyika itajihifadhi ndani ya Serikali ya Muungano. Hivyo kimwonekano, serikali ya Muungano ni serikali mbili zilizounganishwa pamoja.Kwa lugha ya kisheria,Serikali ya Tanganyika imekasimisha mamlaka yake kwa Serikali ya Muungano. Kwa hiyo Serikali ya muungano ni Serikali iliyojikusanyia mamlaka mbili kwa pamoja. Mamlaka ya mambo ya Muungano na Mamlaka ya mambo ya Tanganyika.
Ipo serikali ya mambo ya Zanzibar inayoitwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Mfumo/Muundo huu ndio wanaoulalamikia Zanzibar kwa kusema Tanganyika imejivalisha koti la Muungano.

Serikali mbili zinaonekana na moja iko nyuma ya pazia na mamlaka tatu za kisheria;mamlaka ya mambo ya Tanganyika(Tz bara),mamlaka ya mambo ya Muungano na mamlaka ya mambo ya Zanzibar.

"Kwa hiyo mimi nilipinga mfumo wa Serikali Moja. Shirikisho la Serikali Tatu lingekuwa nigharama kubwa mno kwa Tanganyika. Zanzibar ingeendesha Serikali yake na kuchangiagharama za kuendesha Serikali ya Shirikisho; na Tanganyika ingefanya vivyo hivyo.Lakini ni dhahiri kwamba mchango wa Tanganyika ndio hasa ungeendesha SerikaIi yaShirikisho. Kwa hiyo Tanganyika ingeendesha Serikali yake ya watu 12, 000, 000 na piandiyo ingetoa sehemu kubwa ya kuendesha Serikali ya Shirikisho la watu 1...

Kwa hivyo ilitupasa tujiulize kwa nini tunataka kuibebesha Tanganyikagharama zote hizo; na hasa kwa nini tunataka Serikali ya Tanganyika? Hivituna hofu ya kwamba Tanganyika, bila kuwa na SerikaIi yake, itaoekanakuwa imemezwa na Zanzibar? Hofu yetu ni kwamba tukiwa na SerikaliMoja Tanganyika itaonekana kuwa imeimeza Zanzibar. Basi na tutafutemfumo ambao utaiondolea Zanzibar hofu hii ya kumezwa, bila kuibebesha Tanganyika mzigo wa kuendesha Serikalli mbili zenye uzito unaolingana" uk 10-11
link
Uongozi Wetu Na Hatma Ya Tanzania (by Nyerere)

 
Wazanzibari wanahitaji Zanzibar iwe nchi kamili. Kwa maana iwe na Rais wake. Hao wakishasema kitu, ndio msimamamo wao. Vinginevyo unatafuta tafaruku. Wanasema 66% ya Wazanzibar wanataka Zanzibar itambulike kama nchi kamili. Maoni yangu ni kwamba, tukubali Tanganyika iwe nchi kamili na Zanzibar vivyo hivyo halafu tujadiliane upya namna ya kuungana upya.

Kama watanganyika wote watakuwa na akili zako basi watanganyika wa leo wangekuwa wanajadili kwenda mwezini kutafiti mambo ya huko,ahhh!lakini wapi kila kukicha mawazo yao yote ni kuikaba koo zanzibar .
 
Back
Top Bottom