Rasmi: Eliud Kipchonge atunukiwa Udaktari wa Heshima

Rasmi: Eliud Kipchonge atunukiwa Udaktari wa Heshima

Horseshoe Arch

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2009
Posts
13,403
Reaction score
12,775
Chuo Kikuu cha Laikipia kilichopo mjini Eldoret nchini Kenya, kimemtunuku Mwanariadha bingwa wa dunia wa mbio ndefu Eliud Kipchoge, Shahada ya Udaktari wa Heshima (Honoris causa) kutokana na kuipeperusha vema bendera ya Kenya kimataifa kupitia riadha.

Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Joseph Kibet Rotich amesema uamuzi huo ulifikiwa na Baraza la taaluma la chuo hicho (University senate) kwa mujibu wa hati ya chuo hicho (University Charter) Sehemu ya 3, Kifungu cha 21.4(k) ambacho kinatoa mamlaka kwa Chuo hicho kumtunuku udaktari wa heshima mtu yeyote aliyefanya jambo kubwa lenye mchango chanya katika jamii.

eliudi.jpg
 
Wenzetu wanathamini sana michango wanayotoa raia wa nchi zao ambayo inaleta sifa kwa taifa ila hapa kwetu jambo linaloweza kukupa sifa tena kwa muda tu ni siasa na siasa zenyewe ni sharti ulambe miguu ya watawala! Bravo Kenya, mmepiga hatua kwenye mambo mengi ambayo sisi hata kujifunza kutambaa bado!
 
Wenzetu wanathamini sana michango wanayotoa raia wa nchi zao ambayo inaleta sifa kwa taifa ila hapa kwetu jambo linaloweza kukupa sifa tena kwa muda tu ni siasa na siasa zenyewe ni sharti ulambe miguu ya watawala! Bravo Kenya, mmepiga hatua kwenye mambo mengi ambayo sisi hata kujifunza kutambaa bado!
Kwa maoni yako hapa Tanzania ni nani alistahili kutunukiwa?.
 
Wenzetu wanathamini sana michango wanayotoa raia wa nchi zao ambayo inaleta sifa kwa taifa ila hapa kwetu jambo linaloweza kukupa sifa tena kwa muda tu ni siasa na siasa zenyewe ni sharti ulambe miguu ya watawala! Bravo Kenya, mmepiga hatua kwenye mambo mengi ambayo sisi hata kujifunza kutambaa bado!

Upumbavu tu, Watu wote wangeruhusu mihemko itawale vichwa vyao leo kungekiwa na kina Prof Christiano Ronaldo, Imagine Prof John Cena, au Dr Diego Maradona,
 
Hio PhD sio ya kusomea kwa hivyo sio title , Unaweza ukaitwa Prof,au Dr Kama degree yako ya uzamifu umeisomea lakini hii ya honorary anapewa mtu ku appreciate mchango wake katika jamii.
Upumbavu tu, Watu wote wangeruhusu mihemko itawale vichwa vyao leo kungekiwa na kina Prof Christiano Ronaldo, Imagine Prof John Cena, au Dr Diego Maradona,
 
Back
Top Bottom