Rasmi:Okwi ni mali ya Simba SC

Muda mfupi uliopita Okwi amesaini kandarasi ya kuitumikia Simba kwa miaka miwili.Hongera Simba fc.
 
Uyo jamaa anawachezea simba sharubu anavotaka
 
Karibu nyumbani mkali wa magoli ya mbali hah hah mbona kazi ipo!
 
Popee wote wamepiga picha na Aveva na Kaburu lakini kwa Okwiii umejipeleka wewe unajua kucheza na akili zao Hongera
 
Hongera Simba kwa kumrudisha Okwi bado Serunkuma na Owino
 
Sijaelewa kabisa kwanini Viongozi wa Simba wamemsajili Okwi? Ikumbukwe Okwi wa jana sio Okwi wa leo. Je, usajili wa Okwi una tija? " Babu Okwi " amekuja kufanya nini Sima? Ana jipya gani?
 
Ashakuwa babu huyo simba stress za ubingwa zinawafanya wajisajilie ovyo ovyo tu. Kwanza ile rufaa vipi FIFA siku zinaenda [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Okwi alishaisha hiyo ukiona mzungu kamchoka huko ulaya ujue siyo okwi Wa enzi ya TANU!tanga nao kesho kutwa wacott anaweza kutua kuna kusaini yanga!
 
Subir majibu machafu toka kwa mikia, ila mi nnachofikiri okwi Kaja kuifunga Yanga,hilo ndio hitaji kubwa la hans popo
 
Muda mfupi uliopita Okwi amesaini kandarasi ya kuitumikia Simba kwa miaka miwili.Hongera Simba fc.
SSC are confused. Wamemwona lini akicheza na kutathmini kiwango chake? Angekuwa kwenye kiwango si angeitwa timu ya taifa Uganda? Lakini hayumo. Huko Ulaya alikuwa timu daraja la chini kabisa na ameondoka kwa kukosa namba. Leo SSC wanamchukua! Kuna umakini hapo?
 
We kweli huna kumbu kumbu,hii picha mbona ya kitambo? Kama kuja aje sio kuota kama mnavyo subiri pointi 3 za fifa.
 
Kwa kiwango cha mpira wa bongo okwi bado anacheza tena huenda akasumbua sana.Suala la kuitwa au kutokuitwa kwenye timu ya taifa silipi nafasi sana mana hua inategemea na kocha husika anamchukuliaje japo na kiwango cha mchezaji pia kinamata katika kupick timu.Tusubiri muda ndio utaongea vizuri ila kwa mtazamo wangu okwi bado anaweza kucheza bongo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…