Rasmi Premier League yapitisha dili la Todd Boehly kuinunua Chelsea

Rasmi Premier League yapitisha dili la Todd Boehly kuinunua Chelsea

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Bodi ya Ligi Kuu ya England ‘Premier League’ umethibitishwa rasmi kupitisha mchakato wa Klabu ya Chelsea kuuzwa kwa paundi bilioni 4.25, ambapo mnunuzi ni Bilionea Todd Boehly.

Klabu hiyo iliwekwa sokoni na aliyekuwa mmiliki wake, Roman Abramovich ambaye amewekewa vikwazo kutokana na ukaribu wake na Rais wa Urusi, Vladimir Putin.

Kilichobaki baada ya tamko hilo ni mchakato wa Serikali ya Uingereza katika kuhalaliza leseni ya manunuzi, ambapo baada ya hapo utafanyika utaratibu wa mwisho kukamilisha mauzo.

Kwa sasa Chelsea imeruhusiwa kuendelea kujiendesha kwa lesni maalum ya Serikali hadi Mei 31, 2022.


Source: Daily Mail
 
Kweli ulaya kuna pesa, uyo jamaa nimemwangaliaaaa nikasema angekuwa mbongo unaweza sema msukuma flani tu uko choka mbaya maana picha zake zipo simple sana
 
transaction ya hizo paundi 4.5b zinakwenda kibindoni kwa nani? maana abro amewwekewa vikwazo hatakiwi uingereza??
 
Nchi za Ulaya na Marekani zina upumbavu mwingi sana. Yaani kwenye karne ya 21 bado wanafanya vitendo vya Plundering, Looting and Piracy vya karne za kale huko!

Walichokifanya kwa Abramovich na Warusi wengine ni vitendo vya kihuni! Mwanzilishi wa vita vya Ukraine ni Vladimir Putin! Sasa iweje ukawanyang'anye watu wengine mali zao? Kwa nini ukavifungie vilabu vya michezo vya Urusi kushiriki kwenye mashindano?

Putin...! Nyoosha hao mashoga wote mpaka wakufahamu wewe ni nani.
 
Naanza kuamini waingereza akili zao ni fyatu sana, kumbe kuna sababu nyingi sana Barclays kujitoa kama mdhamini mkuu wa ligi
 
Back
Top Bottom