Rasmi timu 15 ligi kuu kuvaa nembo ya GSM

Rasmi timu 15 ligi kuu kuvaa nembo ya GSM

Dabil

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2021
Posts
6,823
Reaction score
15,293
Kwenye kikao kilichofanyika kati ya bodi ya ligi na vilabu 15 vya ligi kuu vimeafiki kuvaa nembo ya mdhamini mwenza wa ligi kuu GSM .

Kwa maana hiyo Simba tu haitavaa hiyo nembo na pia mabango ya GSM hayatatikiwa kwenye mechi za Simba.
 
Kwenye kikao kilichofanyika kati ya bodi ya ligi na vilabu 15 vya ligi kuu vimeafiki kuvaa nembo ya mdhamini mwenza wa ligi kuu GSM .

Kwa maana hiyo Simba tu haitavaa hiyo nembo na pia mabango ya GSM hayatatikiwa kwenye mechi za Simba.
Nahisi hata Azam
 
Hii ligi nayo kachumbali zimekuwa nyingi,mbona waliokuwa wakitoa pesa misimu kadhaa kama KCB walikuwa hawapati mambo kama haya au mikataba yao inakuwa na melezo tofauti kulingana na dau?
 
Hii ligi nayo kachumbali zimekuwa nyingi,mbona waliokuwa wakitoa pesa misimu kadhaa kama KCB walikuwa hawapati mambo kama haya au mikataba yao inakuwa na melezo tofauti kulingana na dau?

Nadhani KCB hawakuegemea upande wowote, hakukuwa na mgongano wa maslahi baina ya timu na timu au/mwekezaji mmoja na mwingine.

We hujiulizi kwanini Azam TV anatoa mpunga mkubwa tu na Azam Fc inashiriki League hii hii lakini hapigiwi kelele!?

Unakumbuka Patrice Motsepe owner na Aliyekuwa Rais wa Mamelodi Sundown alipotaka kugombea U-Rais wa CAF aliambiwa kitu gani!?

Akili kumkichwa.
 
Timu isiyovaa nembo ya mdhamini italipa faini ya m 10 kwa kila match itakayogoma kuvaa kwa match 3,baada ya hapo kama itaendelea kugoma itashushwa daraja,tunajua leo mmeleta kisingizio cha kuumwa baada ya bodi ya ligi kugoma kuyaondoa mabango ya mdhamini kule kagera mkaona mzushe mnaumwa,tunawasubiri game ijayo mtasingizia nini
 
Mfano
Bilioni 1 ya GSM iende moja kwa moja vilabu 16 ,
Ni sawa Tsh 62,500,000/-
Wakati Emirates Aluminium anailipa Simba Tsh 300,000,000/- kwa mwaka
Sasa ung'oe mdhamini wa milioni 300 uweke begani mdhamini wa milioni 62.5
Ni uchizi [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Tofauti ya NBC na GSM kwenye udhamini wao ni m 300 tu
 
Kwenye kikao kilichofanyika kati ya bodi ya ligi na vilabu 15 vya ligi kuu vimeafiki kuvaa nembo ya mdhamini mwenza wa ligi kuu GSM .

Kwa maana hiyo Simba tu haitavaa hiyo nembo na pia mabango ya GSM hayatatikiwa kwenye mechi za Simba.
Hata kutokuvaa au kutoweka mabango, BADO NI AINA YA KUITANGAZA GSM
 
Nadhani KCB hawakuegemea upande wowote, hakukuwa na mgongano wa maslahi baina ya timu na timu au/mwekezaji mmoja na mwingine.

We hujiulizi kwanini Azam TV anatoa mpunga mkubwa tu na Azam Fc inashiriki League hii hii lakini hapigiwi kelele...
Kweli! sema haya mambo uswahili nao shida sana,sasa hii ligi TFF si kuna siku wataigawa kimatabaka au hili ni jambo la kawaida tu?
 
Timu isiyovaa nembo ya mdhamini italipa faini ya m 10 kwa kila match itakayogoma kuvaa kwa match 3,baada ya hapo kama itaendelea kugoma itashushwa daraja,tunajua leo mmeleta kisingizio cha kuumwa baada ya bodi ya ligi kugoma kuyaondoa mabango ya mdhamini kule kagera mkaona mzushe mnaumwa,tunawasubiri game ijayo mtasingizia nini
Mkuu, sijajua kama nitakua naleta ubishani au itakua ni katika kujenga ufahamu wa kila mmoja wetu.

Simba atahusika na branding ya uwanja kwenye mechi ambazo yeye ni mwenyeji tu. Kwahivyo, Simba hahusiki chochote na mabango ya kwenye uwanja ambao yeye si mwenyeji, mwenye shughuli yake leo alikua ni Kagera Sugar.

Yeye (Kagera Sugar) ndiye anaamua aweke bango lipi, asiweke lipi.

Labda vinginevyo unambie kwamba taratibu zimebadilika, au unambie kwamba Simba ndiye alikua mwenyeji wa mechi ya leo pale Kaitaba.
 
Simba hawavai mpaka maswali yao yajibiwe, mambo ya kiswahili kwenye mpira wetu yakomeshwe, TFF na bodi ya ligi wasitumie njaa ya vilabu vyetu kama sababu ya kuingia mikataba isiyofuata sheria na kanuni.
 
Kweli! sema haya mambo uswahili nao shida sana,sasa hii ligi TFF si kuna siku wataigawa kimatabaka au hili ni jambo la kawaida tu?

TFF wameteleza kidogo, GSM kama mdhamini mkuu wa Young Africans malengo yao makubwa ni kuhakikisha timu wanayoidhamini inatwaa ubingwa wa Ligi Kuu, watu hao hao hawatakiwi kudhamini Ligi Kuu maana hakutakuwa na mashindano ya haki.

Hizi kelele huwezi kusikia zinaelekezwa kwa Azam, NBC na hata kipindi kile Vodacom pamoja na wadhamini wengine .

Mama yako anapopewa tenda ya kugawa chakula kwenye sherehe ambayo hata wewe ni mualikwa unajua nini kinakwenda kutokea.
 
Timu isiyovaa nembo ya mdhamini italipa faini ya m 10 kwa kila match itakayogoma kuvaa kwa match 3,baada ya hapo kama itaendelea kugoma itashushwa daraja,tunajua leo mmeleta kisingizio cha kuumwa baada ya bodi ya ligi kugoma kuyaondoa mabango ya mdhamini kule kagera mkaona mzushe mnaumwa,tunawasubiri game ijayo mtasingizia nini
hiyo Sheria ni kwa nembo ya mdhamini mkuu tu mkuu
 
Mfano
Bilioni 1 ya GSM iende moja kwa moja vilabu 16 ,
Ni sawa Tsh 62,500,000/-
Wakati Emirates Aluminium anailipa Simba Tsh 300,000,000/- kwa mwaka
Sasa ung'oe mdhamini wa milioni 300 uweke begani mdhamini wa milioni 62.5
Ni uchizi [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kwani NBC ametoa kiasi gani
 
Kwenye kikao kilichofanyika kati ya bodi ya ligi na vilabu 15 vya ligi kuu vimeafiki kuvaa nembo ya mdhamini mwenza wa ligi kuu GSM .

Kwa maana hiyo Simba tu haitavaa hiyo nembo na pia mabango ya GSM hayatatikiwa kwenye mechi za Simba.
Kwenye aya ya mwisho hapo inapaswa kuwa "Simba hatavaa nembo, na pia mabango ya GSM hayatakiwi kwenye mechi ambazo Simba ni mwenyeji"

Branding ya uwanja inamhusu timu mwenyeji tu.

Simba hawezi kumpangia Kagera Sugar aweke bango gani na bango gani asiweke pale Kaitaba, hawezi kumpangia Azam aweke bango gani pale Chamazi, vivyo hivyo kwa Mtibwa Sugar pale Manungu, Namungo pale Kassim Majaliwa, Mbeya City pale Sokoine, n.k
 
Tofauti ya NBC na GSM kwenye udhamini wao ni m 300 tu

Na Tofauti nyingine NBC ni mdhamini Mkuu ana haki zote za kukaa bega la kulia kama kanuni za ligi zinavyojieleza.Haya tueleze huyo GSM anataka awekwe kwa bega la kushoto la Simba kwa kanuni ipi?
 
Back
Top Bottom