Rasmi Urusi na Marekani wakutana Saudi Arabia kumaliza vita ya Ukraine, Zelensky hajaitwa kuhudhuria kikao

Rasmi Urusi na Marekani wakutana Saudi Arabia kumaliza vita ya Ukraine, Zelensky hajaitwa kuhudhuria kikao

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Kipindi akiwa kwenye kampeni za kutafuta Urais mwaka 2024, Rais wa Marekani Donald Trump aliahidi kumaliza mgogoro kati ya Ukraine na Urusi

Mwezi takribani mmoja baada ya kuapishwa, tayari mazungumzo yameanza kufanyika ili vita hiyo iliyoanza rasmi mwaka 2022 imalizike

Jumanne ya leo Russia na Marekani walikutana Saudi Arabia ili kujadili namna watakavyoboresha mahusiano kati ya nchi hizo mbili pamoja na kumaliza vita vya Ukraine.

Mkutano huo, uliofanyika katika Ikulu ya Diriyah, Riyadh, ulihudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio, na Waziri wa Russia, Sergey Lavrov.

Mazungumzo haya ni juhudi za serikali ya wa Trump kubadili sera ya Marekani dhidi ya Russia na ni mazungumzo muhimu kuandaa mkutano kati ya Trump na Putin.

Pamoja na mazungumzo hayo kuhusisha vita ya Ukraine hata hivyo, Ukraine haikushiriki, na Rais Volodymyr Zelenskyy amesema hatakubali matokeo ya mazungumzo hayo ikiwa Kyiv haitahusishwa.

Mazungumzo haya yanaashiria mwanzo mpya kati ya Marekani na Russia kwani mara ya mwisho nchi hizo kukaa kuzungumza ilikuwa ni miaka 3 iliyopita


Viongozi wa Ulaya pia wameonekana kukereketwa na kitendo cha kutokuhusishwa kwenye mazungumzo hayo ikiwemo Waziri wa Uingereza Keir Starmer ambaye siku chache zilizopita alitishia kupeleka Jeshi la Uingereza nchini Ukraine.


==========================================================



Senior officials from Russia and the U.S. met in Saudi Arabia on Tuesday to begin talks on improving ties and negotiating an end to the war in Ukraine.

Delegations led by U.S. Secretary of State Marco Rubio and Russian Foreign Minister Sergey Lavrov met at the Diriyah Palace in Riyadh. The meeting marks another pivotal step by the Trump administration to reverse U.S. policy on isolating Russia and is meant to pave the way for a meeting between U.S. President Donald Trump and Russian President Vladimir Putin.

Trump earlier this month upended U.S. policy toward Ukraine and Russia by saying he and Putin had agreed to begin negotiations on ending the war.

Ukrainian officials aren’t taking part in the meeting, and Ukrainian President Volodymyr Zelenskyy said Monday that his country won’t accept the outcome if Kyiv doesn’t take part.

Rubio was accompanied by U.S. national security adviser Mike Waltz and Special Envoy Steve Witkoff, while Lavrov sat next to the Kremlin’s foreign affairs adviser, Yuri Ushakov. Saudi Foreign Minister Faisal bin Farhan and national security adviser Musaed al Alban joined Rubio, Lavrov and others for the start of the meeting but were expected to leave early in the talk

Source: BBC, AP News
 
Waache unafiki, palestina imekaliwa kimabavu wanashabikia ila Ukraine ikikaliwa kimabavu ndio wanalialia?Aiseee haya mazungumzo ndio mwisho wa Ukraine maana ataambiwa asurrender baadhi ya maeneo yake yanayokaliwa kwa sasa na Urusi!!
 
Kuna watu wana zarau sana
Hapana hawa wanastahili, Trump anajuwa hawana lolote bila USA ndio maana juzi VP tu kaenda pale Munich kawashambulia ulaya mpaka waziri wa Germany katoa machozi. Baada ya hapo anasema huu ni uingiliaji wa mambo yetu ya ndani, ala leo ndio wanajuwa mambo yetu, wao kutwa kuingilia mambo yetu ya kutaka turuhusu ushoga wamesahau. Sasa wamekutana na kichaa Trump atawanyosha. Kwa bahati mbaya serikali yote ya USA Trump ndio kidogo afadhali wengine ndio vichaa kabisa hasa VP, wataisoma number miaka hii 4. Mkutano Saudia... wala sio Brussels.
 
Hivyo dunia ilivyo na lazima iende hivi.

Lazima wajinga wawepo, lazima wakali wawepo, lazima wapole wawepo, lazima wababe wawepo, lazima watu makini wawepo n.k

Jambo la msingi ni kujua sisi Tanzania tumeamua kuwa upande gani ? Ni huu huu wa kipuuzi ama tutaamua kubadilika na kuishi jinsi dunia inavyotaka ama tumeridhika na hali zetu ?

Dunia hii hakuna anaye jali kuhusu sijui Congo,Ukraine,Israel,Palestine,Syria,Sudan ni maslahi tu ndio mataifa yanajali
 
Hivyo dunia ilivyo na lazima iende hivi.

Lazima wajinga wawepo, lazima wakali wawepo, lazima wapole wawepo, lazima wababe wawepo, lazima watu makini wawepo n.k

Jambo la msingi ni kujua sisi Tanzania tumeamua kuwa upande gani ? Ni huu huu wa kipuuzi ama tutaamua kubadilika na kuishi jinsi dunia inavyotaka ama tumeridhika na hali zetu ?

Dunia hii hakuna anaye jali kuhusu sijui Congo,Ukraine,Israel,Palestine,Syria,Sudan ni maslahi tu ndio mataifa yanajali
Hii si kiinchi tu, inaanzia chini kwenye serikali za familia kuja za mitaa.
 
Hii si kiinchi tu, inaanzia chini kwenye serikali za familia kuja za mitaa.
Ni kweli kila mtu yuko busy na mambo yake hakuna aliye na huruma na mtu.

Watu wanatazama maslahi yao tu
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Zelesky anaenda kuuwawa coz putini anataka kuondoa kabisa aidia au mentality za zelesky pale Ukraine, na Putin sio wa mchezo mchezo
 
Mkutano huo, uliofanyika katika Ikulu ya Diriyah, Riyadh, ulihudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio, na Waziri wa Russia, Sergey Lavrov.
Pamoja na mazungumzo hayo kuhusisha vita ya Ukraine hata hivyo, Ukraine haikushiriki, na Rais Volodymyr Zelenskyy amesema hatakubali matokeo ya mazungumzo hayo ikiwa Kyiv haitahusishwa.
Viongozi wa Ulaya pia wameonekana kukereketwa na kitendo cha kutokuhusishwa kwenye mazungumzo hayo ikiwemo Waziri wa Uingereza Keir Starmer ambaye siku chache zilizopita alitishia kupeleka Jeshi la Uingereza nchini Ukraine.
Ndio wakati wa waTanzania na Afrika kote kuelewa kuwa dunia hii ina wenyewe. Wengine ni chawa tu hutumika kubwatabwata tu, lakini kwenye maamuzi hata kiti hampewi.

Eti unakwenda Ubelgiji ukidhani wanakusikiliza kubadili uchumi wa nchi yako. We acha tu, hilo kwa wenzetu halipo. Ndio maana baada ya kumaliza kuwafanyia kazi- Galang, Savimbi, Mabutu walivurumishwa kama toilet P.

Maendeleo ya Afrika yataletwa na waafrika wenyewe, japo ni polepole. Ukitaka haraka ndio hayo ya Ukraine.

Leo kweli hata Ulaya hina kiti, hata mwenye matatizo kaambiwa kaa pembeni. Eti tubadilishane Ardhi! Weeee!
 
Ndio wakati wa waTanzania na Afrika kote kuelewa kuwa dunia hii ina wenyewe. Wengine ni chawa tu hutumika kubwatabwata tu, lakini kwenye maamuzi hata kiti hampewi.

Eti unakwenda Ubelgiji ukidhani wanakusikiliza kubadili uchumi wa nchi yako. We acha tu, hilo kwa wenzetu halipo. Ndio maana baada ya kumaliza kuwafanyia kazi- Galang, Savimbi, Mabutu walivurumishwa kama toilet P.

Maendeleo ya Afrika yataletwa na waafrika wenyewe, japo ni polepole. Ukitaka haraka ndio hayo ya Ukraine.

Leo kweli hata Ulaya hina kiti, hata mwenye matatizo kaambiwa kaa pembeni. Eti tubadilishane Ardhi! Weeee!
Waafrika wabadipi fikra, masuala ya kusma tunalalia upande fulani, halaf hao hao mnaodhani ni maadui ndio wanakutana.

Kweli wengi ni chawa
 
Kipindi akiwa kwenye kampeni za kutafuta Urais mwaka 2024, Rais wa Marekani Donald Trump aliahidi kumaliza mgogoro kati ya Ukraine na Urusi

Mwezi takribani mmoja baada ya kuapishwa, tayari mazungumzo yameanza kufanyika ili vita hiyo iliyoanza rasmi mwaka 2022 imalizike

Jumanne ya leo Russia na Marekani walikutana Saudi Arabia ili kujadili namna watakavyoboresha mahusiano kati ya nchi hizo mbili pamoja na kumaliza vita vya Ukraine.

Mkutano huo, uliofanyika katika Ikulu ya Diriyah, Riyadh, ulihudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio, na Waziri wa Russia, Sergey Lavrov.

Mazungumzo haya ni juhudi za serikali ya wa Trump kubadili sera ya Marekani dhidi ya Russia na ni mazungumzo muhimu kuandaa mkutano kati ya Trump na Putin.

Pamoja na mazungumzo hayo kuhusisha vita ya Ukraine hata hivyo, Ukraine haikushiriki, na Rais Volodymyr Zelenskyy amesema hatakubali matokeo ya mazungumzo hayo ikiwa Kyiv haitahusishwa.

Mazungumzo haya yanaashiria mwanzo mpya kati ya Marekani na Russia kwani mara ya mwisho nchi hizo kukaa kuzungumza ilikuwa ni miaka 3 iliyopita


Viongozi wa Ulaya pia wameonekana kukereketwa na kitendo cha kutokuhusishwa kwenye mazungumzo hayo ikiwemo Waziri wa Uingereza Keir Starmer ambaye siku chache zilizopita alitishia kupeleka Jeshi la Uingereza nchini Ukraine.

==========================================================



Senior officials from Russia and the U.S. met in Saudi Arabia on Tuesday to begin talks on improving ties and negotiating an end to the war in Ukraine.

Delegations led by U.S. Secretary of State Marco Rubio and Russian Foreign Minister Sergey Lavrov met at the Diriyah Palace in Riyadh. The meeting marks another pivotal step by the Trump administration to reverse U.S. policy on isolating Russia and is meant to pave the way for a meeting between U.S. President Donald Trump and Russian President Vladimir Putin.

Trump earlier this month upended U.S. policy toward Ukraine and Russia by saying he and Putin had agreed to begin negotiations on ending the war.

Ukrainian officials aren’t taking part in the meeting, and Ukrainian President Volodymyr Zelenskyy said Monday that his country won’t accept the outcome if Kyiv doesn’t take part.

Rubio was accompanied by U.S. national security adviser Mike Waltz and Special Envoy Steve Witkoff, while Lavrov sat next to the Kremlin’s foreign affairs adviser, Yuri Ushakov. Saudi Foreign Minister Faisal bin Farhan and national security adviser Musaed al Alban joined Rubio, Lavrov and others for the start of the meeting but were expected to leave early in the talk

Source: BBC, AP News
Hamna suluhisho hapo.
 
Mkubwa mkubwa tu

Ukiona unaitwa kwenye fursa za mikopo ,ujue wewe ndo fursa ya riba mzigo
 
Trump kazingua sana kwenye hii issue, amemdharau sana Zelesky.
Trump hajazingua, bali kaionyesha Dunia jinsi matatizo yanavyoshughulikiwa na wakubwa. Wengine hupeti-peti lakini Trump anakupa live. Kuwa hivi ndio tunashughulikia matatizo.
Hata Zelensky aliingia kwenye vita sio kama kwenye mjadala wa kufanya hivyo alikuwepo, bali aliambiwa tu 1) Utapata Urais. 2) Tutakupa silaha 3) utajiunga na NATO na EU. 4) Tutaweka vikwazo vya uchumi kwa Rasia na itakufa kiuchumi. Akaingia kwenye 18 bila kujua wenzake hasa wanachokitaka ni nini kwake?

Bahati mbaya uchumi wa marekani na EU umedorola. Mbaya zaidi wafaidika wakubwa wa vita hivyo ni mahasidi wa Marekani ni pamoja na China, India na Uturuki. Hawa walipenda vita iendelee angalau kwa miaka miwili mingine. Kuanzishwa kwa BRICS ndiko kulikomliza Trump na hasa pale Saudia ilipoonyesha nia ya kujiunga na Brics.
 
Back
Top Bottom