Raus Samia hapa umepotoka, fidia ilipwe kwanza

Raus Samia hapa umepotoka, fidia ilipwe kwanza

Izia maji

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2021
Posts
2,997
Reaction score
5,385
Wakili Madeleka: Huwezi KUMVUNJIA MTU NYUMBA YAKE bila KUMLIPA FIDIA, ili ujenge BARABARA, halafu ukamwambia hayo ni “MAENDELEO YAKE”, asubiri “UTAMLIPA BAADAE”. Sasa unataka AKAISHI WAPI NA FAMILIA YAKE? Huu ni UKATILI ambao HAUKUBALIKI. Serikali ILIPE FIDIA za watu, tena STAHIKI.

Pia soma > Rais Samia: Mnaotudai fidia kuweni na subira tumalize miradi ya maendeleo kwanza ndipo tuwalipe


========

Rais Samia: Tunajua maeneo ambayo miradi inajegwa ni ameneo ya watu lakini tunachokifanya ni maendeleo ya watu, ni maendeleo yenu. Hatukatai kulipa fidia lakini tunapojenga mradi, fedha hizi ni za kudunduliza, kwahiyo tunajenga mradi kwanza wananchi wanufaike halafu tunakuja kuangalia mambo ya fidia.

Kwahiyo kwa wale wote wanaotudaia fidia zao kwa maendeleo yao wenyewe tunaomba muwe na subira, tuacheni tumalize mambo ya maendeleo wananchi wengi wafaidike, halafu tutaangalia mambo ya fidia.

Sasa kuna maeneo watu wanazuia kabisa mradi usipite kwasababu hajapewa fidia, niwaombe sana wananchi, miradi hii si kwa faida ya Serikali kuu, ni kwa faida ya Taifa letu, kwahiyo tuacheni tufanye miradi, mambo ya fidia mimi nawahakikishia hatanyimwa mtu haki yake.

Tukiwa tayari tuwalipa fidia, kwahiyo niwaombe sana wananchi acheni miradi ijengwe kwa manufaa yenu na fidia zitakuja zitalipwa.
 
Wakili Madeleka: Huwezi KUMVUNJIA MTU NYUMBA YAKE bila KUMLIPA FIDIA, ili ujenge BARABARA, halafu ukamwambia hayo ni “MAENDELEO YAKE”, asubiri “UTAMLIPA BAADAE”. Sasa unataka AKAISHI WAPI NA FAMILIA YAKE? Huu ni UKATILI ambao HAUKUBALIKI. Serikali ILIPE FIDIA za watu, tena STAHIKI.

========

Rais Samia: Tunajua maeneo ambayo miradi inajegwa ni ameneo ya watu lakini tunachokifanya ni maendeleo ya watu, ni maendeleo yenu. Hatukatai kulipa fidia lakini tunapojenga mradi, fedha hizi ni za kudunduliza, kwahiyo tunajenga mradi kwanza wananchi wanufaike halafu tunakuja kuangalia mambo ya fidia.

Kwahiyo kwa wale wote wanaotudaia fidia zao kwa maendeleo yao wenyewe tunaomba muwe na subira, tuacheni tumalize mambo ya maendeleo wananchi wengi wafaidike, halafu tutaangalia mambo ya fidia.

Sasa kuna maeneo watu wanazuia kabisa mradi usipite kwasababu hajapewa fidia, niwaombe sana wananchi, miradi hii si kwa faida ya Serikali kuu, ni kwa faida ya Taifa letu, kwahiyo tuacheni tufanye miradi, mambo ya fidia mimi nawahakikishia hatanyimwa mtu haki yake.

Tukiwa tayari tuwalipa fidia, kwahiyo niwaombe sana wananchi acheni miradi ijengwe kwa manufaa yenu na fidia zitakuja zitalipwa.
"Tukiwa tayari tuwalipa fidia"! Haya ni maneno ya mtu mwenye nyumba Kizimkazi, Dar es Salaam na Dodoma na nyingine nyingi za serikali ambazo ametengewa yeye, kwa kifupi wasipokuwa tayari hawatakulipa na wewe masikini hakikisha haufi kabla ya kulipwa haki yako kama alivyokuahidi.
Mama kaupiga mwingi.
 
Raisi katoa boko.. Mie nina kibanda changu, kazi nishastaafu, mmekivunja kisha mnasema tanilipa mradi ukiisha miradi yenyewe hii ya kusua sua kukamilika. 🤔
 
TUUNDE TUME YA HAKI JINAI IMCHUNGUZE chief hangaya.

Mchengerwa, haya NDIO unayomshauri mama mkwe??!!
 
Back
Top Bottom