Habari wazalendo.
Kumbe wale wasanii wawili wa bongo movie Aunt na Ray , ambao walijiondoa UKAWA hawakuwahi kujiandikisha kupiga kura na hawana kadi ya kupiga kura na hawapo katika daftari lolote la mpiga kura.
Inashangaza sana watu hao ambao hawajajiandikisha wanataka kutuambia tupigie wagombea wao kura na tusifanye mabadiliko. Ni jambo la ajabu sana. Habari hzi zimetoka kwa watu wa karibu wa masupastaa hao.
Kutokana na hili naanza kupata wasiwasi wa hao wasanii wanaotumika ktk kampeni, inawezekana wengi wao hawakujiandikisha. Pia natoa rai kwa ray na aunt watoke hadharani waoneshe kadi zao.
Tunachezewa sana akili huko majukwaani