Ray Kigosi: Huu ni weupe wa maji (Ununuzi wa maji waongezeka mjini)

Hivi nyie mnafikiri anakunywa maji haya mnayoyafahamu!!mtakunywa hadi mpasuke matumbo,muulizeni kwa kina!!
 
Tafadhari mkuu ingekuwa vyema kama ungeedit bandiko na kuliondoa hilo neno zeru zeru...hili neno huwa linawafedhehesha ndugu zetu wenye ulemavu wa ngozi....kwani limekaa kiuzalilishaji....alafu vile vile ule sio weupe bali ni ulemavu....

Samahani kama nimekukwaza mkuu....
 
Mtu mweupe akinywa maji Kwa wingi atakuwa Mweusi pia... Ray hajadanfanya kabisa
 
Mm nakunywa ila nachanganya na sabuni ya unga na jiki ili nitakate haraka
 
Hahahahah..
 
Mimi nina mawazo tofauti kidogo. Hivi kama background yako ilikuwa kushinda na kutembea juani,then mambo yanabadilika unaanza kutembea na kukaa kwenye gari,ofisi,nyumba full AC unafikiri utakuwa na rangi ile ile ya kupigwa na jua??? Hamjaona watu wakitoka bongo na kwenda mtoni wakirudi wanakuwaje?

Mimi binafsi nikiangalia picha zangu wakati niko mtoni na sasa hivi ni tofauti kabisa, nimekuwa mweusi pamoja na kwamba sitembei hovyo juani ila mazingira tu ya kibongobongo vumbi kibao unajikuta rangi inafifia.

My point,unaweza kuonekana mweusi ila ukiwa expsosed na mazingira fulani ngozi inang'aa bila kujichubua ni kawaida, hata nyinyi mnaopinga wengine tukiona picha zenu wakati mko vijijini sio kama mnavyong'aa leo.
 
naona atakuwa amejiunga na tiba ya za dr.MshanaJR baada ya Mzee Mzizi Mkavu kufulia
Mzizi Mkavu ameshafulia? Una uhakika? Alishusha elimu hapa jinsi ya kuchukua watu misukule weee. May be misukule yake huko aliko imechachamaa... Ha ha haaaa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…