Ray Kigosi: Thus Why I'm So Wonders

Hajui kiingereza ila ana maisha mazuri karibia mara 3 ya wanaomcheka.. Thats life...

Nnachoshangaa ni hiki kitu, mbona mastaa wakubwa Duniani hawajui ngeli na wala sio habari, mfano mzuri Lionel messi mchezaji bora mara nne wa mchezo unaopendwa zaidi duniani, hazungumzi kiingereza hata Ray anampita ila, ina ana utajiri wa zaidi bilioni 200 za kibongo, sio msomi na wala haiwezi kuwa habari kule kwao argentina eti messi hajui english... Haipo hiyo..

Ila kwetu tunajua kabisa wasanii wetu english siyo lugha yao ya kwanza, na wengi hawajapata nafasi ya kujifunza lugha hiyo ila anapokosea kitu tunabreak the internet,,, hataree
 
He didnt go to school as much as u, its not fair to hiss him. His acquisitive should be encouraged, English is equidistant to education. Sasa akae kimya au aache kabisa kuigiza, sio jambo la kucheka.
Aongee kiswahili tena fasaha kinachowakilisha, hizo ngonjera zake hakika ni jambo la kucheka na kudhihakiwa!
 
Waswahili tunavyojua kuchekana na kuzodoana kuhusu kiingereza utadhani tunakijua. Kumbe wote tukipewa fursa ya kukiongea au kukiandika tunaishia na "the" "the" "the" na "you know" tu.
 

Sasa kama hajui si awe kama messi tu, aongee lugha ya kwao,au kiswahili ni dhambi?
 

Kama hajui aongee kiswahili kwani lazima aongee chiingeredha?
 
Enewei Ray kwani yeye hagombei ubunge? wenzake wema sepetu, steve nyerere na Irene uwoya wanajitosa mjengon
 
Kama hajui aongee kiswahili kwani lazima aongee chiingeredha?

Watu wana Ile dhana ukiongea kiingereza basi wewe ni msomi....so kila mtu anajitutumua ili mradi aonekane kasoma.
 
Kama falsafa ya enzi za utotoni kuwa ukianguka na baiskeli ndio umejua.Kazi kwelikweli.
 
Kama ni hivyo hana haja ya kutumia lugha ambayo haijui! Mbona Mondi hajakwenda shule lakini anabomoka umombo wa ukweli?

Ni kweli kabisa maana kuna watu kama kina milard Ayo huwa cjawahi ona ameandika ung'eng'e kwenye habari yeyote japo anajua
 
He didnt go to school as much as u, its not fair to hiss him. His acquisitive should be encouraged, English is equidistant to education. Sasa akae kimya au aache kabisa kuigiza, sio jambo la kucheka.

Wenyewe wana cliché yao inayosema wao ni kioo cha jamii so kila wanachofanya lazima kimulikwe ...hakuna haja ya kuongea lugha usio ijua kufikishe ujumbe,matokeo yake anajipotezea soko na popularity
 
Huwa nawashangaa sana watu wanaohangaika kutazama maigizo ya kitanzania 'bongo movies'...

Huo muda wa kukaa na kutazama hayo maruerue ni bora niutumie kwenda kuhonga mdudu...

Bongo Movies ishatoweka chief.
 

Mastaa wa juu kama hawajui kiingereza huongea lugha zao kiufasaha, na wachache wao inapowabidi huongea kiingereza lkn sio broken hii ya Im so wonderz...
Lol
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…