Najiuliza hiv inakuaje msanii Kama Rayvanny ameshindwa kumalizana na Diamond hadi kaamua kumpeleka Diamond BASATA. Hivi anadhani mikataba inaweza kuvunjwa kirahisi tu na BASATA. Afate masharti ya mkataba basata hawataweza msaidia Kitu.
Ajifunze Kwa Harmonize mwenzake hakuhangaika na BASATA alilipa alichotakiwa na kusepa vyema, ikiwemo kuachiwa akaunti zake za mitandao ya jamii kama YouTube.
Ajifunze pia Kwa Mavoko hta alipompeleka Diamond basata bado akaunti yake ya YouTube hadi leo inamilikiwa na wasafi Kwa Sababu hakuheshimu mkataba na ikambidi afungue akaunti nyingine ya billionaire kid.
Rayvanny zingatia mkataba basata yeye ni mlezi tu hawez kamwe kushurutisha Diamond akusamehe kirahisi na ukumbuke Diamond Yuko na mtu mbad Sana Sallam Sk, so ndugu yatakukuta ya Mavoko usipoheshimu kuvunja mkataba wako Kwa mujibu wa Sheria.
- Tunachokijua
- Madai ya kuwa msanii Raymond Shaban Mwakyusa maarufu kama Rayvanny kumpeleka msanii aliyekuwa akimsimamia Nassib Abdul (Diamond) yalizuka punde tu baada ya kuondoka katika label ya WCB na kuhamia katika label yake ya Next Level Music (NLM) katika Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA).
Baadhi ya tetesi zinadai kuwa msanii huyo amempeleka Diamond BASATA kwa madai yanayotokana na baadhi ya matukio likiwemo la kupata jina ndani ya WCB hivyo kama ameamua kujitenga ni lazima alipie gharama kwa kuvunja mikataba ya kikazi inayowaongoza jambo lililopelekea kwa madai ya tetesi kuandikiwa kulipa kiasi cha shilingi za kitanzania 800,000,000/= kama fidia.
Katika kuthibitisha madai hayo vyombo vya habari mbalimbali vimejaribu kufuatilia madai hayo ya BASATA na kuonesha ni kweli walionekana katika eneo la BASATA 27/ 07/2022 hilo lakini hakukuwa na Ushahidi unaoonesha kuwa walienda kwa sababu ya madai hayo kulingana na jambo hilo kutokuwekwa hadharani